< 1 Tessalonicenses 5 >

1 Porém, irmãos, ácerca dos tempos e das estações, não necessitaes de que se vos escreva;
Sasa, kwa habari ya muda na nyakati, ndugu, hamna haja kwamba kitu chochote kiandikwe kwenu.
2 Porque vós mesmos sabeis muito bem que o dia do Senhor virá como o ladrão de noite;
Kwa kuwa ninyi wenyewe mwajua kwa usahihi ya kuwa siku ya Bwana inakuja kama mwizi ajapo usiku.
3 Pois que, quando disserem: Ha paz e segurança; então lhes sobrevirá repentina destruição, como as dôres de parto áquella que está gravida; e de modo algum escaparão.
Pale wasemapo kuna “Amani na usalama”, ndipo uharibifu huwajia ghafla. Ni kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba. Hawataepuka kwa njia yeyote.
4 Mas vós, irmãos, já não estaes em trevas, para que aquelle dia vos surprehenda como um ladrão.
Lakini ninyi, ndugu hampo kwenye giza hata ile siku iwajie kama mwizi.
5 Todos vós sois filhos da luz e filhos do dia: nós não somos da noite nem das trevas.
Kwa maana ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi siyo wana wa usiku au wa gizani.
6 Não durmamos pois, como os demais, mas vigiemos, e sejamos sobrios.
Hivyo basi, tusilale kama wengine walalavyo. Bali tukeshe na kuwa makini.
7 Porque os que dormem dormem de noite, e os que se embebedam embebedam-se de noite.
Kwa kuwa wanaolala hulala usiku na wanao lewa hulewa usiku.
8 Mas nós, que somos do dia, sejamos sobrios, vestindo-nos da couraça da fé e da caridade, e tendo por capacete a esperança da salvação.
Kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, tuwe makini. Tuvae ngao ya imani na upendo, na, kofia ya chuma, ambayo ni uhakika wa wokovu wa wakati ujao.
9 Porque Deus não nos tem designado para a ira, mas para a acquisição da salvação, por nosso Senhor Jesus Christo.
Kwa kuwa Mungu hakutuchagua mwanzo kwa ajili ya gadhabu, bali kwa kupata wokovu kwa njia ya Bwana Yesu Kristo.
10 O qual morreu por nós, para que, quer vigiemos, quer durmamos, vivamos juntamente com elle.
Yeye ndiye aliyetufia ili kwamba, tukiwa macho au tumelala, tutaishi pamoja naye.
11 Pelo que exhortae-vos uns aos outros, e edificae-vos uns aos outros, como tambem o fazeis.
Kwa hiyo, farijianeni na kujengana ninyi kwa ninyi, kama ambavyo tayari mnafanya.
12 E rogamo-vos, irmãos, que reconheçaes os que trabalham entre vós e que presidem sobre vós no Senhor, e vos admoestam:
Ndugu, twawaomba muwatambue wale wanaotumika miongoni mwenu na wale walio juu yenu katika Bwana na wale wanao washauri.
13 E tende-os em grande estima e amor, por causa da sua obra. Tende paz entre vós.
Tunawaomba pia muwatambue na kuwapa heshima katika upendo kwa sababu ya kazi yao. Muwe na amani miongoni mwenu ninyi wenyewe.
14 Rogamo-vos tambem, irmãos, que admoesteis os desordeiros, consoleis os de pouco animo, sustenteis os fracos, e sejaes pacientes para com todos.
Twawasihi, ndugu: muwaonye wasio kwenda kwa utaratibu, watieni moyo walio kata tamaa, Wasaidieni walio wanyonge, na muwe wavumilivu kwa wote.
15 Vêde que ninguem dê a outrem mal por mal, mas segui sempre o bem, assim uns para com os outros, como para com todos.
Angalieni asiwepo mtu yeyote anayelipa baya kwa baya kwa mtu yeyote. Badala yake, fanyeni yaliyo mema kwa kila mmoja wenu na kwa watu wote.
16 Regozijae-vos sempre.
Furahini siku zote.
17 Orae sem cessar.
Ombeni bila kukoma.
18 Em tudo dae graças; porque esta é a vontade de Deus em Christo Jesus para comvosco.
Mshukuruni Mungu kwa kila jambo, kwa sababu hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Yesu Kristo.
19 Não apagueis o Espirito.
Msimzimishe Roho.
20 Não desprezeis as prophecias.
Msiudharau unabii.
21 Examinae todas as coisas; retende o bem.
Yajaribuni mambo yote. Mlishike lililo jema.
22 Abstende-vos de toda a apparencia do mal.
Epukeni kila mwonekano wa uovu.
23 E o mesmo Deus de paz vos sanctifique em tudo; e todo o vosso sincero espirito, e alma, e corpo, sejam conservados irreprehensiveis para a vinda de nosso Senhor Jesus Christo.
Mungu wa amani awakamilishe katika utakatifu. Roho, nafsi na mwili vitunzwe pasipo mawaa katika kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
24 Fiel é o que vos chama, o qual tambem o fará.
Yeye aliyewaita ni mwaminifu, naye ndiye mwenye kutenda.
25 Irmãos, orae por nós.
Ndugu, tuombeeni pia.
26 Saudae a todos os irmãos em osculo sancto.
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
27 Pelo Senhor vos conjuro que esta epistola se leia a todos os sanctos irmãos.
Nawasihi katika Bwana kwamba barua hii isomwe kwa ndugu wote.
28 A graça de nosso Senhor Jesus Christo seja comvosco. Amen.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi.

< 1 Tessalonicenses 5 >