< Pieśń nad Pieśniami 2 >
1 Jestem różą Saronu i lilią dolin.
Mimi ni ua la Sharoni, yungiyungi ya bondeni.
2 Jak lilia między cierniami, tak moja umiłowana między pannami.
Kama yungiyungi katikati ya miiba ndivyo alivyo mpenzi wangu katikati ya wanawali.
3 Jak jabłoń między leśnymi drzewami, tak mój miły między młodzieńcami. Z wielkim pragnieniem usiadłam w jego cieniu, a jego owoc [jest] słodki memu podniebieniu.
Kama mti wa mtofaa miongoni mwa miti ya msituni ndivyo alivyo mpenzi wangu miongoni mwa wanaume vijana. Ninafurahia kuketi kivulini mwa mwanaume huyu, na tunda lake ni tamu kwangu.
4 Wprowadził mnie do komnaty biesiadnej, a jego chorągwią nade mną jest miłość.
Amenichukua mpaka kwenye ukumbi wa karamu, na bendera ya huyu mwanaume juu yangu ni upendo.
5 Pokrzepcie mnie bukłakami, posilcie mnie jabłkami, bo jestem chora z miłości.
Nitie nguvu kwa zabibu kavu, niburudishe kwa matofaa, kwa maana ninazimia kwa mapenzi.
6 Jego lewa ręka pod moją głową, a jego prawa ręka mnie obejmuje.
Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, na mkono wake wa kuume unanikumbatia.
7 Zaklinam was, córki Jerozolimy, na sarny i łanie polne: Nie budźcie mego umiłowanego i nie przerywajcie [jego] snu, dopóki nie zechce.
Binti za Yerusalemu, ninawaagiza kwa paa na kwa ayala wa shambani: Msichochee wala kuamsha mapenzi hata yatakapotaka yenyewe.
8 Głos mego umiłowanego! Oto idzie, skacząc po górach, a podskakując po pagórkach.
Sikiliza! Mpenzi wangu! Tazama! Huyu hapa anakuja, akirukaruka juu milimani akizunguka juu ya vilima.
9 Mój umiłowany podobny jest do sarny albo młodego jelenia. Oto stoi za naszym murem, zagląda przez okna, patrzy przez kraty.
Mpenzi wangu ni kama paa au ayala kijana. Tazama! Anasimama nyuma ya ukuta wetu, akitazama kupitia madirishani, akichungulia kimiani.
10 Mój umiłowany odezwał się i powiedział mi: Wstań, moja umiłowana, moja piękna, i chodź!
Mpenzi wangu alizungumza na kuniambia, “Inuka, mpenzi wangu, mrembo wangu, tufuatane.
11 Oto bowiem minęła zima, deszcz ustał i przeszedł.
Tazama! Wakati wa masika umepita, mvua imekwisha na ikapita.
12 Kwiatki pokazały się na ziemi, nadszedł czas śpiewania i głos synogarlicy słychać w naszej ziemi.
Maua yanatokea juu ya nchi; majira ya kuimba yamewadia, sauti za njiwa zinasikika katika nchi yetu.
13 Drzewo figowe już wypuściło swoje niedojrzałe figi, a kwitnąca winorośl wydaje swoją woń. Wstań, moja umiłowana, moja piękna, i chodź!
Mtini unatunga matunda yake ya mwanzoni, zabibu zinazochanua zaeneza harufu nzuri. Inuka, njoo mpenzi wangu. Mrembo wangu, tufuatane.”
14 Moja gołębico, [mieszkająca] w skalnych szczelinach, w stromych kryjówkach, ukaż mi swoją twarz, daj mi usłyszeć swój głos, gdyż twój głos jest słodki i twoja twarz piękna.
Hua wangu penye nyufa za majabali, mafichoni pembezoni mwa mlima, nionyeshe uso wako, na niisikie sauti yako, kwa maana sauti yako ni tamu, na uso wako unapendeza.
15 Schwytajcie nam lisy, małe lisy, które psują winnice, ponieważ nasze winnice kwitną.
Tukamatie mbweha, mbweha wale wadogo wanaoharibu mashamba ya mizabibu, mashamba yetu ya mizabibu yaliyochanua.
16 Mój umiłowany [jest] mój, a ja jestem jego. Pasie on wśród lilii.
Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake, yeye hujilisha katikati ya yungiyungi.
17 Nim zaświta dzień i znikną cienie, zawróć, mój umiłowany, bądź jak sarna albo młode jelenie na górach Beter.
Mpaka jua linapochomoza, na vivuli vikimbie, rudi, mpenzi wangu, na uwe kama paa, au kama ayala kijana juu ya vilima vya Betheri.