< Rzymian 9 >

1 Mówię prawdę w Chrystusie, nie kłamię, co mi poświadcza moje sumienie w Duchu Świętym;
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 Że odczuwam wielki smutek i nieustający ból w moim sercu.
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 Pragnąłbym bowiem sam być odłączony od Chrystusa za moich braci, za moich krewnych według ciała.
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 Są to Izraelici, do których [należy] usynowienie, chwała, przymierza, nadanie prawa, służba Boża i obietnice;
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 Do których należą ojcowie i z których według ciała [pochodzi] Chrystus, który jest nad wszystkimi, Bóg błogosławiony na wieki. Amen. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Lecz nie jest możliwe, żeby miało zawieść słowo Boże. Nie wszyscy bowiem, którzy pochodzą od Izraela, są Izraelem.
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 Nie wszyscy też przez to, że są potomstwem Abrahama, są dziećmi, ale [jest powiedziane]: W Izaaku będzie nazwane twoje potomstwo.
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 To znaczy, że nie dzieci ciała są dziećmi Bożymi, lecz dzieci obietnicy są uznane za potomstwo.
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 Takie bowiem [jest] słowo obietnicy: O tym właśnie czasie przyjdę, a Sara będzie miała syna.
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 A nie tylko to, ale i Rebeka, gdy poczęła z jednego [mężczyzny], naszego ojca Izaaka;
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 Gdy [dzieci] jeszcze się nie urodziły i nie zrobiły nic dobrego ani złego, aby zgodnie z wybraniem trwało postanowienie Boga, nie z uczynków, ale z tego, który powołuje;
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 Powiedziano jej, że starszy będzie służył młodszemu;
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 Jak jest napisane: Jakuba umiłowałem, ale Ezawa znienawidziłem.
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Cóż więc powiemy? Czy Bóg jest niesprawiedliwy? Nie daj Boże!
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 Mówi bowiem do Mojżesza: Zmiłuję się, nad kim się zmiłuję, a zlituję się, nad kim się zlituję.
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 A więc nie [zależy to] od tego, który chce, ani od tego, który zabiega, ale od Boga, który okazuje miłosierdzie.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 Pismo bowiem mówi do faraona: Po to właśnie cię wzbudziłem, aby okazać na tobie swoją moc i żeby moje imię było głoszone po całej ziemi.
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 A zatem komu chce, okazuje miłosierdzie, a kogo chce, czyni zatwardziałym.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Ale mi powiesz: Dlaczego więc jeszcze oskarża? Któż bowiem sprzeciwił się jego woli?
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 Człowieku! Kimże ty jesteś, że prowadzisz spór z Bogiem? Czy naczynie gliniane [może] powiedzieć do tego, kto je ulepił: Dlaczego mnie takim uczyniłeś?
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Czy garncarz nie ma władzy [nad] gliną, żeby z tej samej bryły zrobić jedno naczynie do [użytku] zaszczytnego, a drugie do niezaszczytnego?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 A [cóż], jeśli Bóg, chcąc okazać gniew i dać poznać swoją moc, znosił w wielkiej cierpliwości naczynia gniewu przygotowane na zniszczenie;
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 I żeby dać poznać bogactwo swojej chwały na naczyniach miłosierdzia, które [wcześniej] przygotował ku chwale;
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 [To znaczy] nas, których powołał, nie tylko z Żydów, ale i z pogan?
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 Jak też u Ozeasza mówi: Lud, który nie był mój, nazwę moim ludem, a tę, która nie była umiłowana, [nazwę] umiłowaną.
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 I stanie się [tak], że w miejscu, gdzie im mówiono: Wy nie [jesteście] moim ludem, tam będą nazwani synami Boga żywego.
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 A Izajasz woła o Izraelu: Choćby liczba synów Izraela była jak piasek morski, resztka będzie ocalona.
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 Zakończy bowiem dzieło i skróci je w sprawiedliwości. Istotnie, skróci Pan dzieło na ziemi.
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 Jak i przedtem powiedział Izajasz: Gdyby Pan zastępów nie zostawił nam potomstwa, stalibyśmy się jak Sodoma i bylibyśmy podobni do Gomory.
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 Cóż więc powiemy? To, że poganie, którzy nie szukali sprawiedliwości, dostąpili sprawiedliwości – sprawiedliwości, która jest z wiary.
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 Izrael zaś, zabiegając o prawo sprawiedliwości, nie doszedł do prawa sprawiedliwości.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 Dlaczego? Ponieważ [o nie zabiegali] nie z wiary, ale jakby [było] z uczynków prawa. Potknęli się bowiem o kamień potknięcia;
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 Jak jest napisane: Oto kładę na Syjonie kamień potknięcia i skałę zgorszenia, a każdy, kto w niego wierzy, nie będzie zawstydzony.
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Rzymian 9 >