< Rzymian 6 >
1 Cóż więc powiemy? Czy mamy trwać w grzechu, aby łaska obfitowała?
Tuseme nini basi? Je, twendelee kubaki katika dhambi ili neema ya Mungu iongezeke?
2 Nie daj Boże! My, którzy umarliśmy dla grzechu, jakże możemy jeszcze w nim żyć?
Hata kidogo! Kuhusu dhambi sisi tumekufa—tutaendeleaje kuishi tena katika dhambi?
3 Czyż nie wiecie, że my wszyscy, którzy zostaliśmy ochrzczeni w Jezusie Chrystusie, w jego śmierci zostaliśmy ochrzczeni?
Maana, mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana na Kristo Yesu, tulibatizwa na kuungana na kifo chake.
4 Zostaliśmy więc pogrzebani z nim przez chrzest w śmierci, aby jak Chrystus został wskrzeszony z martwych przez chwałę Ojca, tak żebyśmy i my postępowali w nowości życia.
Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia tuweze kuishi maisha mapya.
5 Jeśli bowiem zostaliśmy z nim wszczepieni w podobieństwo jego śmierci, to będziemy też [z nim wszczepieni] w podobieństwo zmartwychwstania;
Maana, kama sisi tumeungana naye katika kufa kama yeye, vivyo hivyo tutaungana naye kwa kufufuliwa kutoka wafu kama yeye.
6 Wiedząc o tym, że nasz stary człowiek został ukrzyżowany razem [z nim], aby ciało grzechu zostało zniszczone, żebyśmy już więcej nie służyli grzechowi.
Tunajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja na Kristo, ili hali ya dhambi iharibiwe, tusiwe tena watumwa wa dhambi.
7 Kto bowiem umarł, został uwolniony od grzechu.
Kwa maana, mtu aliyekufa, amenasuliwa kutoka katika nguvu ya dhambi.
8 Jeśli więc umarliśmy z Chrystusem, wierzymy, że też z nim będziemy żyć;
Basi, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.
9 Wiedząc, że Chrystus, powstawszy z martwych, więcej nie umiera i śmierć nad nim więcej nie panuje.
Maana, tunajua kwamba Kristo amekwisha fufuliwa kutoka wafu na hafi tena; kifo hakimtawali tena.
10 To bowiem, że umarł, raz umarł dla grzechu, a że żyje, żyje dla Boga.
Hivyo, kwa kuwa alikufa—mara moja tu—dhambi haina nguvu tena juu yake; na sasa anaishi maisha yake katika umoja na Mungu.
11 Tak i wy uważajcie siebie za martwych dla grzechu, a żywych dla Boga w Jezusie Chrystusie, naszym Panu.
Hali kadhalika nanyi lazima mjione kuwa mmekufa kuhusu dhambi, lakini kama mnaoishi katika umoja na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
12 Niechże więc grzech nie króluje w waszym śmiertelnym ciele, żebyście [mieli] mu być posłuszni w jego pożądliwościach.
Kwa hiyo, dhambi isiitawale tena miili yenu ambayo hufa, na hivyo kuzitii tamaa zake.
13 I nie oddawajcie waszych członków jako oręża niesprawiedliwości grzechowi, ale oddawajcie samych siebie Bogu jako ożywieni z martwych i wasze członki jako oręż sprawiedliwości Bogu.
Wala msitoe hata sehemu moja ya miili yenu iwe chombo cha kutenda uovu na dhambi. Badala yake, jitoleeni ninyi wenyewe kwa Mungu kama watu waliofufuliwa kutoka wafu; toeni nafsi zenu zote kwa Mungu kwa ajili ya uadilifu.
14 Grzech bowiem nie będzie nad wami panował, bo nie jesteście pod prawem, lecz pod łaską.
Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
15 Cóż więc? Będziemy grzeszyć, bo nie jesteśmy pod prawem, ale pod łaską? Nie daj Boże!
Basi, tuseme nini? Je, tutende dhambi ati kwa sababu hatuko chini ya Sheria bali chini ya neema? Hata kidogo!
16 Czyż nie wiecie, że komu oddajecie siebie jako słudzy w posłuszeństwo, komu jesteście posłuszni, [tego] jesteście sługami: bądź grzechu ku śmierci, bądź posłuszeństwa ku sprawiedliwości?
Mnajua kwamba mkijitolea ninyi wenyewe kama watumwa na kumtii fulani, mnakuwa kweli watumwa wake mtu huyo—au watumwa wa dhambi, na matokeo yake ni kifo, au wa utii, na matokeo yake ni kukubaliwa kuwa waadilifu.
17 Ale chwała Bogu, że gdy byliście sługami grzechu, usłuchaliście z serca wzoru tej nauki, której się poddaliście;
Ingawa mlikuwa watumwa wa dhambi zamani, sasa lakini—namshukuru Mungu—mmetii kwa moyo wote yale maazimio na mafundisho mliyopokea.
18 A będąc uwolnieni od grzechu, staliście się sługami sprawiedliwości.
Mlikombolewa kutoka utumwa wa dhambi, mkawa watumwa wa uadilifu.
19 Po ludzku mówię, z powodu słabości waszego ciała. Jak bowiem oddawaliście wasze członki na służbę nieczystości i nieprawości, [aby czynić] nieprawość, tak teraz oddawajcie wasze członki na służbę sprawiedliwości, abyście byli uświęceni.
(Hapa natumia lugha ya kawaida ya watu kwa sababu ya udhaifu wenu wenyewe.) Kama vile wakati fulani mlivyojitolea ninyi wenyewe kutumikia uchafu na uhalifu kwa ajili ya uovu, vivyo hivyo sasa jitoleeni nafsi zenu wenyewe kutumikia uadilifu kwa ajili ya utakatifu.
20 Dopóki bowiem byliście sługami grzechu, byliście wolni od sprawiedliwości.
Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na uadilifu.
21 Jakiż więc wówczas mieliście pożytek z tych [rzeczy], których się teraz wstydzicie? Ich bowiem końcem [jest] śmierć.
Sasa, mlipata faida gani siku zile kutokana na mambo yale ambayo mnayaonea aibu sasa? Maana, matokeo ya mambo haya ni kifo!
22 Lecz teraz, uwolnieni od grzechu, gdy staliście się sługami Boga, macie swój pożytek ku uświęceniu, a na końcu życie wieczne. (aiōnios )
Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele. (aiōnios )
23 Zapłatą bowiem za grzech [jest] śmierć, ale darem łaski Boga jest życie wieczne w Jezusie Chrystusie, naszym Panu. (aiōnios )
Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu. (aiōnios )