< Rzymian 11 >

1 Pytam więc: Czy Bóg odrzucił swój lud? Nie daj Boże! Ja bowiem [też] jestem Izraelitą, z potomstwa Abrahama, z pokolenia Beniamina.
Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2 Bóg nie odrzucił swego ludu, który przedtem znał. Czyż nie wiecie, co Pismo mówi o Eliaszu? Jak się skarży przed Bogiem na Izraela:
Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3 Panie, pozabijali twoich proroków i zburzyli twoje ołtarze; tylko ja sam pozostałem i czyhają na moje życie.
“Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?”
4 Ale cóż mu odpowiada Bóg? Zostawiłem sobie siedem tysięcy mężów, którzy nie zgięli kolan przed Baalem.
Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: “Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali.”
5 Tak i w obecnym czasie pozostała resztka według wybrania przez łaskę.
Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6 A jeśli przez łaskę, to już nie z uczynków, inaczej łaska już nie byłaby łaską. Jeśli zaś z uczynków, to już nie jest łaska, inaczej uczynek już nie byłby uczynkiem.
Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7 Cóż więc? Czego Izrael szuka, tego nie osiągnął, ale wybrani osiągnęli, a inni zostali pogrążeni w zatwardziałości;
Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8 (Jak jest napisane: Bóg dał im ducha twardego snu, oczy, aby nie widzieli, i uszy, aby nie słyszeli) aż do dziś.
kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao.”
9 A Dawid mówi: Niech ich stół stanie się sidłem i pułapką, zgorszeniem i odpłatą.
Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10 Niech zaćmią się ich oczy, aby nie widzieli, a ich grzbiet zawsze pochylaj.
Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!”
11 Pytam więc: Czy się potknęli, aby upaść? Nie daj Boże! Ale [raczej] przez ich upadek zbawienie [doszło] do pogan, aby wzbudzić w nich zawiść.
Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12 A jeśli ich upadek jest bogactwem świata, a ich pomniejszenie bogactwem pogan, o ileż bardziej ich pełnia?
Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13 Mówię bowiem do was, pogan. Na ile jestem apostołem pogan, chlubię się swoją służbą;
Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14 Może [w ten sposób] wzbudzę zawiść w [tych, którzy są] moim ciałem i zbawię niektórych z nich.
nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15 Jeśli bowiem odrzucenie ich stało się pojednaniem [dla] świata, czym [będzie] przyjęcie [ich], jeśli nie powstaniem z martwych do życia?
Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16 Ponieważ jeśli zaczyn jest święty, [to] i ciasto, a jeśli korzeń jest święty, [to] i gałęzie.
Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17 Jeśli zaś niektóre z gałęzi zostały odłamane, a ty, który byłeś dzikim drzewem oliwnym, zostałeś wszczepiony zamiast nich i stałeś się uczestnikiem korzenia i tłustości drzewa oliwnego;
Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
18 Nie wynoś się nad gałęzie. Jeśli jednak się wynosisz, [wiedz, że] nie ty podtrzymujesz korzeń, lecz korzeń ciebie.
Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19 Ale powiesz: Odłamane zostały gałęzie, abym ja został wszczepiony.
Lakini utasema: “Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake.”
20 Słusznie, z powodu niewiary zostały odłamane, ty zaś trwasz przez wiarę. Nie pysznij się, ale się bój.
Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21 Jeśli bowiem Bóg nie oszczędził naturalnych gałęzi, wiedz, że i ciebie nie oszczędzi.
Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22 Spójrz więc na dobroć i srogość Boga: srogość dla tych, którzy upadli, a dla ciebie dobroć, jeśli będziesz trwał w [tej] dobroci. W przeciwnym razie ty też będziesz wycięty.
Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23 Lecz i oni, jeśli nie będą trwali w niewierze, zostaną wszczepieni, gdyż Bóg ma moc ponownie ich wszczepić.
Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24 Jeśli bowiem ty zostałeś wycięty z dzikiego z natury drzewa oliwnego, a wbrew naturze zostałeś wszczepiony w szlachetne drzewo oliwne, o ileż bardziej ci, którzy są [gałęziami] naturalnymi, wszczepieni zostaną w swoje własne drzewo oliwne!
Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25 Nie chcę bowiem, bracia, abyście nie znali tej tajemnicy – żebyście sami siebie nie uważali za mądrych – że zatwardziałość po części przyszła na Izrael, dopóki nie wejdzie pełnia pogan.
Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26 I tak cały Izrael będzie zbawiony, jak jest napisane: Przyjdzie z Syjonu wybawiciel i odwróci bezbożność od Jakuba.
Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27 A to [będzie] moje przymierze z nimi, gdy zgładzę ich grzechy.
Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
28 Tak więc co do ewangelii są nieprzyjaciółmi ze względu na was, lecz co do wybrania są umiłowani ze względu na ojców.
Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29 Nieodwołalne są bowiem dary i powołanie Boże.
Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30 Jak bowiem wy kiedyś nie wierzyliście Bogu, ale teraz dostąpiliście miłosierdzia z powodu ich niewiary;
Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31 Tak i oni teraz stali się nieposłuszni, aby z powodu miłosierdzia wam [okazanego] i oni miłosierdzia dostąpili.
Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32 Bóg bowiem zamknął ich wszystkich w niewierze, aby się nad wszystkimi zmiłować. (eleēsē g1653)
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
33 O głębokości bogactwa zarówno mądrości, jak i poznania Boga! Jak niezbadane są jego wyroki i niedocieczone jego drogi!
Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34 Któż bowiem poznał myśl Pana albo kto był jego doradcą?
“Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35 Lub kto pierwszy mu coś dał, aby otrzymać odpłatę?
Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?”
36 Z niego bowiem, przez niego i w nim jest wszystko. Jemu chwała na wieki. Amen. (aiōn g165)
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina. (aiōn g165)

< Rzymian 11 >