< Objawienie 13 >
1 I stanąłem na piasku morza. I zobaczyłem bestię wychodzącą z morza, mającą siedem głów i dziesięć rogów, a na jej rogach było dziesięć koron, a na jej głowach imię bluźnierstwa.
Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
2 A bestia, którą widziałem, podobna była do pantery, a jej łapy jak u niedźwiedzia, a jej paszcza jak paszcza lwa. I dał jej smok swoją moc, swój tron i wielką władzę.
Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
3 I zobaczyłem jedną z jej głów jakby śmiertelnie zranioną, lecz jej śmiertelna rana została uleczona. I cała ziemia zdziwiła się, i [poszła] za bestią.
Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
4 I oddali pokłon smokowi, który dał władzę bestii. Oddali też pokłon bestii, mówiąc: Któż [jest] podobny do bestii? Któż z nią może walczyć?
Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
5 I dano jej paszczę mówiącą rzeczy wielkie i bluźnierstwa. Dano jej też moc, aby działała przez czterdzieści dwa miesiące.
Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
6 I otworzyła swoją paszczę, by bluźnić przeciwko Bogu, by bluźnić jego imieniu, jego przybytkowi i tym, którzy mieszkają w niebie.
Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
7 Pozwolono jej też walczyć ze świętymi i zwyciężać ich. I dano jej władzę nad każdym plemieniem, językiem i narodem.
Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
8 Wszyscy mieszkańcy ziemi oddadzą jej pokłon, ci, których imiona nie są zapisane w księdze życia Baranka zabitego od założenia świata.
Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
9 [Jeśli] ktoś ma uszy, niech słucha!
Yeye aliye na sikio na asikie.
10 Jeśli ktoś do niewoli bierze, do niewoli pójdzie, jeśli ktoś zabija mieczem, mieczem musi zostać zabity. Tu jest cierpliwość i wiara świętych.
Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
11 Potem zobaczyłem inną bestię wychodzącą z ziemi, a miała dwa rogi podobne do Baranka, ale mówiła jak smok.
Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
12 I całą władzę pierwszej bestii sprawuje na jej oczach, i sprawia, że ziemia i jej mieszkańcy oddają pokłon pierwszej bestii, której śmiertelna rana została wyleczona.
Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
13 I czyni wielkie cuda, sprawiając, że nawet ogień zstępuje z nieba na ziemię na oczach ludzi.
Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
14 I zwodzi mieszkańców ziemi przez cuda, które jej pozwolono czynić przed bestią, mówiąc mieszkańcom ziemi, aby sporządzili wizerunek bestii, która miała ranę od miecza, ale ożyła.
Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
15 I pozwolono jej tchnąć ducha w wizerunek bestii, tak żeby przemówił wizerunek bestii i sprawił, że ci, którzy nie oddali pokłonu wizerunkowi bestii, zostali zabici.
Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
16 I sprawia, aby wszyscy, mali i wielcy, bogaci i biedni, wolni i niewolnicy, przyjęli znamię na prawą rękę lub na czoło;
Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
17 I aby nikt nie mógł kupić ani sprzedać, tylko ten, kto ma znamię, imię bestii lub liczbę jej imienia.
ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
18 Tu jest mądrość. Kto ma rozum, niech obliczy liczbę bestii, gdyż jest to liczba człowieka. A liczba jej: sześćset sześćdziesiąt sześć.
Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.