< Psalmów 146 >

1 Alleluja. Chwal, duszo moja, PANA.
Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
2 Będę chwalić PANA, póki żyję; będę śpiewał memu Bogu, póki będę istniał.
Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
3 Nie pokładajcie ufności we władcach [ani w żadnym] synu ludzkim, u którego nie ma wybawienia.
Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
4 Opuszcza go duch i wraca do swojej ziemi; w tymże dniu zginą [wszystkie] jego myśli.
Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
5 Błogosławiony ten, kogo pomocą jest Bóg Jakuba, kto nadzieję pokłada w PANU, jego Bogu;
Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
6 Który uczynił niebo i ziemię, morze i wszystko, co w nich [jest]; który dochowuje prawdy na wieki;
Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
7 Który oddaje sprawiedliwość pokrzywdzonym [i] daje chleb głodnym; PAN uwalnia więźniów.
Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
8 PAN otwiera [oczy] ślepych; PAN podnosi przygnębionych; PAN miłuje sprawiedliwych.
Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
9 PAN strzeże przychodniów, wspomaga sierotę i wdowę, ale krzyżuje drogę niegodziwych.
Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
10 PAN będzie królował na wieki, twój Bóg, o Syjonie, z pokolenia na pokolenie. Alleluja.
Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.

< Psalmów 146 >