< Psalmów 106 >

1 Alleluja. Wysławiajcie PANA, bo [jest] dobry, bo jego miłosierdzie [trwa] na wieki.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Któż wypowie wielkie dzieła PANA i ogłosi całą jego chwałę?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Błogosławieni, którzy strzegą sądu i czynią sprawiedliwość w każdym czasie.
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Pamiętaj o mnie, PANIE, przez miłość do swego ludu; nawiedź mnie swoim zbawieniem;
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 Abym widział szczęście twoich wybranych, cieszył się radością twego narodu i chlubił się razem z twoim dziedzictwem.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Zgrzeszyliśmy wraz z naszymi ojcami, popełniliśmy nieprawość i postąpiliśmy niegodziwie.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Nasi ojcowie w Egipcie nie zrozumieli twoich cudów, nie pamiętali wielkości twego miłosierdzia, lecz buntowali się nad Morzem Czerwonym.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 A jednak ich wybawił przez wzgląd na swoje imię, aby okazać swą moc.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Zgromił Morze Czerwone i wyschło; i przeprowadził ich przez głębiny [jak] przez pustynię.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Tak wybawił ich z ręki tego, który ich nienawidził, i odkupił ich z ręki wroga.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 Wody okryły ich ciemięzców, nie został ani jeden z nich.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Wtedy uwierzyli jego słowom i śpiewali na jego chwałę.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Szybko [jednak] zapomnieli o jego dziełach, nie czekali na jego rady.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Pałali żądzą na pustyni, na próbę wystawiali Boga na pustkowiu.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 I dał im, czego żądali, lecz zesłał na ich dusze wycieńczenie.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Gdy w obozie zazdrościli Mojżeszowi i Aaronowi, świętemu PANA;
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 Otworzyła się ziemia i pochłonęła Datana, i zakryła zgromadzenie Abirama;
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 I zapłonął ogień w tym zgromadzeniu, płomień spalił niegodziwych.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Zrobili cielca na Horebie i odlanemu posągowi oddali pokłon;
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 I zamienili swą chwałę na podobieństwo wołu jedzącego trawę.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Zapomnieli o Bogu, swoim wybawcy, który dokonywał wielkich czynów w Egipcie;
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Cudownych dzieł w ziemi Chama, rzeczy strasznych nad Morzem Czerwonym.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Dlatego powiedział, że wytraciłby ich, gdyby Mojżesz, jego wybrany, nie stanął w wyłomie przed nim, aby odwrócić jego gniew, by [ich] nie wytracił.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Wzgardzili też wspaniałą ziemią, nie wierząc jego słowu.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 I szemrząc w swoich namiotach, nie byli posłuszni głosowi PANA.
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Dlatego podniósł na nich swoją rękę, aby ich wytracić na pustyni;
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 Aby ich potomstwo rozrzucić wśród pogan i rozproszyć ich po ziemiach.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Przyłączyli się też do Baal-Peor i jedli ofiary [składane] umarłym.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Tak pobudzili [Boga] do gniewu swymi postępkami, że spadła na nich plaga;
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Wtedy powstał Pinchas, dokonał sądu i plaga ustała.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Poczytano mu to za sprawiedliwość po wszystkie pokolenia, na wieki.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Rozgniewali go znowu u wód Meriba, [tak że] Mojżesz wiele ucierpiał z ich powodu;
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 Rozdrażnili bowiem jego ducha i mówił [nierozważnie] swymi ustami.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Nie wytępili narodów, jak im to PAN nakazał.
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 Lecz zmieszali się z tymi narodami i nauczyli się ich czynów;
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 I służyli ich bożkom, które stały się dla nich pułapką.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Ofiarowali bowiem demonom swoich synów i swoje córki;
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 I przelewali krew niewinną, krew swoich synów i córek, których ofiarowali bożkom Kanaanu, i ziemia została skalana rozlewem krwi.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Splamili się swymi czynami i cudzołożyli swymi postępkami.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Dlatego PAN zapłonął gniewem przeciw swemu ludowi, tak że obrzydził sobie swoje dziedzictwo.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 I wydał ich w ręce pogan, i panowali nad nimi ci, którzy ich nienawidzili.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 I uciskali ich wrogowie, ujarzmili ich swoją ręką.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Wielokrotnie ich ocalał, lecz oni rozgniewali go swymi zamysłami i zostali upokorzeni przez swoje nieprawości.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 A jednak wejrzał na ich ucisk i usłyszał ich wołanie.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 Przypomniał sobie bowiem o swoim przymierzu z nimi i pożałował według swej wielkiej litości.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Wzbudził też litość dla nich u wszystkich, którzy ich uprowadzili w niewolę.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Wybaw nas, PANIE, nasz Boże, i zgromadź nas spośród pogan, abyśmy wysławiali twoje święte imię i chlubili się twoją chwałą.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Błogosławiony PAN, Bóg Izraela, od wieków na wieki; niech cały lud powie: Amen. Alleluja.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Psalmów 106 >