< Liczb 33 >

1 Oto miejsca postojów synów Izraela, którzy wyszli z ziemi Egiptu ze swymi zastępami pod wodzą Mojżesza i Aarona.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Na rozkaz PANA Mojżesz spisał ich wymarsze według etapów. A oto ich wymarsze według etapów:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Wyruszyli z Ramses w pierwszym miesiącu, piętnastego dnia tego pierwszego miesiąca; nazajutrz po święcie Paschy synowie Izraela wyszli pod potężną ręką na oczach wszystkich Egipcjan;
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 Podczas gdy Egipcjanie grzebali wszystkich pierworodnych, których PAN zabił wśród nich. Także i nad ich bogami PAN dokonał sądu.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Wyruszyli więc synowie Izraela z Ramses i rozbili obóz w Sukkot.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Wyruszyli z Sukkot i rozbili obóz w Etam, które leży na skraju pustyni.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Wyruszyli z Etam i wrócili do Pi-Hachirot, które leży naprzeciw Baal-Sefon, i rozbili obóz przed Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Wyruszyli z Pi-Hachirot, przeszli przez środek morza na pustyni i po trzech dniach drogi po pustyni Etam rozbili obóz w Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Wyruszyli z Mara i przyszli do Elim. A w Elim [było] dwanaście źródeł wody i siedemdziesiąt palm i tam rozbili obóz.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Wyruszyli z Elim i rozbili obóz nad Morzem Czerwonym.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Wyruszyli znad Morza Czerwonego i rozbili obóz na pustyni Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Wyruszyli z pustyni Sin i rozbili obóz w Dofka.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Wyruszyli z Dofka i rozbili obóz w Alusz.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Wyruszyli z Alusz i rozbili obóz w Refidim, gdzie lud nie miał wody do picia.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Wyruszyli z Refidim i rozbili obóz na pustyni Synaj.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Wyruszyli z pustyni Synaj i rozbili obóz w Kibrot-Hattaawa.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Wyruszyli z Kibrot-Hattaawa i rozbili obóz w Chaserot.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Wyruszyli z Chaserot i rozbili obóz w Ritma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Wyruszyli z Ritma i rozbili obóz w Rimmon-Peres.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Wyruszyli z Rimmon-Peres i rozbili obóz w Libnie.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Wyruszyli z Libny i rozbili obóz w Rissa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Wyruszyli z Rissa i rozbili obóz w Kehelata.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Wyruszyli z Kehelata i rozbili obóz na górze Szefer.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Wyruszyli z góry Szefer i rozbili obóz w Charada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Wyruszyli z Charada i rozbili obóz w Makhelot.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Wyruszyli z Makhelot i rozbili obóz w Tachat.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Wyruszyli z Tachat i rozbili obóz w Terach.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Wyruszyli z Terach i rozbili obóz w Mitka.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Wyruszyli z Mitka i rozbili obóz w Chaszmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Wyruszyli z Chaszmona i rozbili obóz w Moserot.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Wyruszyli z Moserot i rozbili obóz w Bene-Jaakan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Wyruszyli z Bene-Jaakan i rozbili obóz w Chor-Haggidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Wyruszyli z Chor-Haggidgad i rozbili obóz w Jotbata.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Wyruszyli z Jotbata i rozbili obóz w Abrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Wyruszyli z Abrona i rozbili obóz w Esjon-Geber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Wyruszyli z Esjon-Geber i rozbili obóz na pustyni Syn, to [jest] w Kadesz.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Wyruszyli z Kadesz i rozbili obóz na górze Hor, na granicy ziemi Edomu.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Wtedy wstąpił kapłan Aaron na górę Hor na rozkaz PANA i tam umarł w czterdziestym roku po wyjściu synów Izraela z ziemi Egiptu, w pierwszym [dniu] piątego miesiąca.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron miał sto dwadzieścia trzy lata, kiedy umarł na górze Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 A król Aradu, Kananejczyk, który mieszkał na południu w ziemi Kanaan, usłyszał, że nadciągają synowie Izraela.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Wyruszyli z góry Hor i rozbili obóz w Salmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Wyruszyli z Salmona i rozbili obóz w Punon.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Wyruszyli z Punon i rozbili obóz w Obot.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Wyruszyli z Obot i rozbili obóz w Ijje-Abarim, na granicy Moabu.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Wyruszyli z Ijjim i rozbili obóz w Dibon-Gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Wyruszyli z Dibon-Gad i rozbili obóz w Almon-Diblataim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Wyruszyli z Almon-Diblataim i rozbili obóz na górach Abarim, naprzeciwko Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Wyruszyli z gór Abarim i rozbili obóz na równinach Moabu, nad Jordanem, naprzeciw Jerycha.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 I rozłożyli się nad Jordanem, od Bet-Jeszimot aż do Abel-Szittim, na równinach Moabu.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 I PAN przemówił do Mojżesza na równinach Moabu, nad Jordanem, naprzeciw Jerycha, tymi słowy:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Przemów do synów Izraela i powiedz im: Gdy przeprawicie się przez Jordan do ziemi Kanaan;
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 Wtedy wypędzicie przed sobą wszystkich mieszkańców tej ziemi i zniszczycie wszystkie ich obrazy i wszystkie ich odlane posągi i spustoszycie wszystkie ich wyżyny.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 A wypędziwszy mieszkańców ziemi, zamieszkacie w niej, gdyż dałem wam tę ziemię w posiadanie.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 I rozdzielicie tę ziemię przez losowanie jako dziedzictwo, według waszych rodzin. Liczniejszemu dacie większe dziedzictwo, a mniej licznemu dacie mniejsze dziedzictwo. Gdzie komu los przypadnie, to będzie jego; otrzymacie dziedzictwo według pokolenia waszych ojców.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Jeśli jednak nie wypędzicie przed sobą mieszkańców tej ziemi, wtedy ci, których z nich pozostawicie, będą jak ciernie w waszych oczach i jak kolce dla waszych boków i będą was gnębić w tej ziemi, w której będziecie mieszkać.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Wtedy uczynię wam to, co zamierzałem uczynić im.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Liczb 33 >