< Micheasza 7 >

1 Biada mi! Jestem bowiem jak ostatki po letnich zbiorach, jak pokłosie grona po winobraniu. Nie ma żadnego grona do zjedzenia, moja dusza pragnęła pierwocin z owocu.
Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
2 Pobożny zginął z ziemi, nie ma prawego wśród ludzi. Wszyscy czyhają na krew, każdy zastawia sieci dla swego brata.
Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
3 By chętnie czynić zło obiema rękami, książę i sędzia żądają datku; zamożny [człowiek] wypowiada swoją przewrotną żądzę. I razem wszystko splatają.
Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
4 Najlepszy z nich jest jak oset; najuczciwszy – jak płot ciernisty. Nadchodzi dzień twoich stróżów [i] twojego nawiedzenia; już nastanie ich zamieszanie.
Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
5 Nie wierzcie przyjacielowi, nie ufajcie wodzowi. Strzeż bramy swoich ust przed tą, która leży na twoim łonie.
Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
6 Syn bowiem lekceważy ojca, córka powstaje przeciwko swojej matce, synowa przeciwko swojej teściowej, [a] wrogami człowieka [są] jego domownicy.
Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
7 Dlatego będę wypatrywał PANA, będę oczekiwać Boga mego zbawienia. Mój Bóg mnie wysłucha.
Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
8 Nie ciesz się z mojego powodu, moja nieprzyjaciółko! Chociaż upadłem, powstanę; choć siedzę w ciemności, PAN jest moją światłością.
Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
9 Zniosę gniew PANA, bo zgrzeszyłem przeciwko niemu, aż będzie bronił mojej sprawy i wykona dla mnie sąd. Wyprowadzi mnie na światło i ujrzę jego sprawiedliwość.
Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
10 Ujrzy to moja nieprzyjaciółka i wstyd okryje tę, która do mnie mówi: Gdzie jest PAN, twój Bóg? Moje oczy będą patrzyć na nią, gdy będzie podeptana jak błoto na ulicach.
Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
11 W [tym] dniu, kiedy będą odbudowywać twoje mury, w tym dniu dekret rozejdzie się daleko.
Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
12 W tym dniu będą przychodzić do ciebie od Asyrii aż po miasta obronne, od miast obronnych aż po rzekę, od morza aż do morza i od góry aż do góry.
Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
13 Ta ziemia jednak będzie spustoszona z powodu swoich mieszkańców, z powodu owocu ich czynów.
Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
14 Paś swój lud laską swoją, trzodę swojego dziedzictwa, która mieszka samotnie w lesie i w środku Karmelu. Niech się pasą w Baszanie i Gileadzie [jak] za dawnych dni.
Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
15 Ukażę mu cudowne rzeczy jak za dni, gdy wyszedłeś z ziemi Egiptu.
“Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
16 Ujrzą to narody i zawstydzą się całej swojej potęgi. Przyłożą rękę do ust, a ich uszy ogłuchną.
Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
17 Będą lizać proch jak wąż, wyjdą ze swoich nor jak zwierzęta pełzające do PANA, naszego Boga, ze strachem i będą się bać ciebie.
Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
18 Któż jest Bogiem jak ty, który przebacza nieprawość i daruje występek resztki swego dziedzictwa? Nie chowa swego gniewu na wieki, bo ma upodobanie w miłosierdziu.
Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
19 Odwróci się i zlituje się nad nami; pokona nasze nieprawości i wrzuci w głębiny morza wszystkie nasze grzechy.
Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
20 Pokażesz prawdę Jakubowi i [okażesz] miłosierdzie Abrahamowi, tak jak przysiągłeś naszym ojcom za dawnych dni.
Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.

< Micheasza 7 >