< Marka 3 >

1 I wszedł znowu do synagogi. A był tam człowiek, który miał uschłą rękę.
Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
2 I obserwowali go, czy uzdrowi go w szabat, aby go oskarżyć.
Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
3 Wtedy powiedział do człowieka, który miał uschłą rękę: Wyjdź na środek!
Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, “Njoo hapa katikati.”
4 A do nich powiedział: Czy wolno w szabat czynić dobrze czy źle? Ocalić życie czy zabić? Lecz oni milczeli.
Kisha, akawauliza, “Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao hawakusema neno.
5 Wtedy spojrzał po nich z gniewem i zasmucony zatwardziałością ich serca, powiedział do tego człowieka: Wyciągnij rękę! Wyciągnął, a jego ręka znowu stała się zdrowa jak [i] druga.
Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, “Nyosha mkono wako!” Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
6 Wówczas faryzeusze wyszli i zaraz odbyli naradę z herodianami przeciwko niemu, w jaki sposób go zgładzić.
Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
7 Jezus zaś ze swymi uczniami odszedł nad morze, a wielkie mnóstwo ludzi szło za nim z Galilei i Judei;
Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
8 Z Jerozolimy, Idumei i Zajordania. Również spośród tych, którzy mieszkali w okolicach Tyru i Sydonu, przyszło do niego mnóstwo ludzi, słysząc, jak wielkie rzeczy czynił.
Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
9 I nakazał swoim uczniom, aby zawsze mieli przygotowaną łódkę, ze względu na tłum, aby nie napierał na niego.
Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
10 Wielu bowiem uzdrowił, tak że wszyscy, którzy mieli [jakieś] choroby, cisnęli się do niego, aby go dotknąć.
Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
11 A duchy nieczyste na jego widok padały przed nim i wołały: Ty jesteś Synem Bożym!
Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, “Wewe ni Mwana wa Mungu!”
12 Lecz on surowo im nakazywał, żeby go nie ujawniały.
Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13 Potem wszedł na górę i wezwał do siebie tych, których sam chciał, a oni przyszli do niego.
Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14 I ustanowił dwunastu, aby z nim byli, aby ich wysłać na głoszenie;
naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15 I aby mieli moc uzdrawiania chorób i wypędzania demonów.
na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
16 [Ustanowił] Szymona, któremu nadał imię Piotr;
Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17 Jakuba, [syna] Zebedeusza, i Jana, brata Jakuba, którym nadał przydomek Boanerges, co znaczy: Synowie Gromu;
Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake “wanangurumo”),
18 Andrzeja, Filipa, Bartłomieja, Mateusza, Tomasza, Jakuba, [syna] Alfeusza, Tadeusza, Szymona Kananejczyka;
Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
19 I Judasza Iskariotę, który go wydał.
Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
20 Potem przyszli do domu. I znowu zgromadził się tłum, tak że nie mogli nawet zjeść chleba.
Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
21 A gdy jego bliscy o tym usłyszeli, przyszli, aby go pochwycić. Mówili bowiem: Odszedł od zmysłów.
Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
22 A uczeni w Piśmie, którzy przyszli z Jerozolimy, mówili: Ma Belzebuba i przez władcę demonów wypędza demony.
Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, “Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo.”
23 I przywoławszy ich [do siebie], mówił do nich w przypowieściach: Jakże szatan może wypędzać szatana?
Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, “Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
24 Jeśli królestwo jest podzielone wewnętrznie, to takie królestwo nie może przetrwać.
Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
25 I jeśli dom jest podzielony wewnętrznie, to taki dom nie będzie mógł przetrwać.
Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
26 Jeśli [więc] szatan powstał przeciwko sobie [samemu] i jest podzielony, nie może przetrwać, ale to jego koniec.
Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
27 Nikt nie może wejść do domu mocarza i zagrabić jego własności, jeśli najpierw nie zwiąże [tego] mocarza; wtedy ograbi jego dom.
“Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
28 Zaprawdę powiadam wam: Wszystkie grzechy i bluźnierstwa, którymi bluźnią synowie ludzcy, będą im przebaczone.
“Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
29 Kto jednak bluźni przeciwko Duchowi Świętemu, nigdy nie dostąpi przebaczenia, ale podlega [karze] wiecznego potępienia. (aiōn g165, aiōnios g166)
lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Bo mówili: Ma ducha nieczystego.
(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”)
31 Wtedy przyszli jego bracia i matka, a stojąc przed domem, posłali po niego, wzywając go.
Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
32 A tłum siedział wokół niego. I powiedzieli mu: Oto twoja matka i twoi bracia [są] przed domem i szukają cię.
Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona.”
33 Lecz on im odpowiedział: Któż jest moją matką i moimi braćmi?
Yesu akawaambia, “Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?”
34 A spojrzawszy po tych, którzy siedzieli wokół [niego], powiedział: Oto moja matka i moi bracia!
Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, “Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35 Kto bowiem wypełnia wolę Boga, ten jest moim bratem, moją siostrą i [moją] matką.
Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu.”

< Marka 3 >