< Kapłańska 25 >
1 Potem PAN powiedział do Mojżesza na górze Synaj:
Yahweh akazungumza na Musa kwenye Mlima wa Sinai, akisema,
2 Przemów do synów Izraela i powiedz im: Gdy wejdziecie do ziemi, którą wam daję, wtedy ziemia będzie obchodzić szabat dla PANA.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mtakapoingia katika nchi ambayo ninawapa, kisha hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh.
3 Przez sześć lat będziesz obsiewał swoje pole i przez sześć lat będziesz obcinał swoją winnicę, i zbierał z niej plony;
Ni lazima mtapanda mazao yenu kwa miaka sita, na kwa miaka sita mtaikatia matawi mizabibu yenu na kukusanya mazao yake.
4 Lecz w siódmym roku ziemia będzie mieć szabat odpoczynku, szabat dla PANA. Nie będziesz obsiewał swego pola ani obcinał swojej winnicy.
Lakini katika mwaka wa saba, Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa, ni Sabato kwa Yahweh. Hamtapanda mashamba yenu wala kuikatia mizabibu yenu matawi yake.
5 Nie będziesz żął tego, co samo wyrośnie po twoich żniwach, ani nie będziesz zbierał winogron twojej zaniechanej winnicy. To będzie rok odpoczynku dla ziemi.
Hamtasimamia mavuno yoyote ya mazao ya mizabibu iliyojiotesha yenyewe katika mashamba yenu ya mizabibu isiyokatiwa matawi. Huu utakuwa mwaka wa pumziko lenye utulivu kwa ardhi.
6 I szabat ziemi będzie dla was pokarmem: dla ciebie, dla twego sługi, dla twojej służącej, dla twego najemnika i dla przybysza, który mieszka u ciebie.
Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa wakati wa Sabato ndicho kitakuwa chakula chako. Wewe mwenyewe, watumwa wako wa kiume na wa kike, watumishi wako wa kuajiriwa na wageni wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula.
7 Także dla twego bydła i zwierząt, które są w twojej ziemi; cały jej plon będzie służyć za pokarm.
Na wnyama wako wa kufugwa na wanyama pori waweze kula chochote ardhi itoacho.
8 Policzysz też sobie siedem lat szabatowych, [to jest] siedem razy po siedem lat; okres siedmiu szabatowych lat będzie wynosił czterdzieści dziewięć lat.
Ni lazima kwenu kuhesabu Sabato saba za miaka, yaani, saba mara miaka saba, ikifanya jumla ya miaka arobaini na tisa.
9 Wtedy [w] dziesiątym [dniu] siódmego miesiąca każesz zatrąbić w trąbę o donośnym dźwięku; w Dniu Przebłagania zatrąbicie po całej waszej ziemi.
Kisha mtapiga sauti ya tarumbeta kila mahali katika siku ya kumi ya mwezi wa saba. Katika Siku ya Upatanisho ni lazima mtapiga tarumbeta katika nchi yenu yote.
10 Poświęcicie pięćdziesiąty rok i ogłosicie wolność w ziemi wszystkim jej mieszkańcom. Będzie to dla was rok jubileuszowy. Każdy z was wróci do swojej posiadłości i do swojej rodziny.
Nanyi mtautenga mwaka wa hamsini kwa ajili ya Yahweh na mtatangaza uhuru katika nchi yote kwa wakazi wote. Kutakuwa na Yubile kwa ajili yenu, ambayo kwayo mali na watumwa ni lazima warejeshwe kwa familia zao.
11 Rok pięćdziesiąty będzie dla was rokiem jubileuszowym. Nie będziecie siać ani żąć tego, co samo wyrosło, ani zbierać winogron z winnic zaniechanych.
Mwaka wa saba kutakuwa na Yubile kwenu. Hamtapanda wala kusimamia mavuno ya kijioteshacho chenyewe, na kukusanya kichipukacho kwenye mizabibu isiyokatiwa matawi.
12 Jest to bowiem rok jubileuszowy, będzie dla was święty. Będziecie jeść to, co na polu urośnie.
Kwa sababu hiyo ni Yubile takatifu kwenu. Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani.
13 W tym roku jubileuszowym każdy z was wróci do swojej posiadłości.
Ni lazima muwarejeshe kila mmoja kwenye miliki yake katika mwaka huu wa Yubile.
14 Jeśli sprzedasz coś swemu bliźniemu albo kupisz coś od niego, niech jeden nie oszukuje drugiego.
Iwapo utauza ardhi yoyote ya jirani yako au kununua ardhi yake, ni shrti msipunjane au kutendeana kwa hila.
15 Według liczby lat po roku jubileuszowym kupisz od swego bliźniego i według liczby lat plonów on sprzeda tobie.
Iwapo unanunua ardhi kutoka kwa jirani yako, zingatia idadi ya miaka na mazao ambayo yaweza kuvunwa mpaka mwaka wa Yubile nyingine. Jirani yako anayeuza ardhi ni lazima aihesabu miaka hiyo pia.
16 Im więcej będzie lat, tym wyższa będzie cena, a im mniej będzie lat, tym niższa będzie cena, ponieważ on sprzedaje ci ilość rocznych plonów.
Miaka inapoongezeka mpaka Yubile nyingine, ataongeza thamani ya ardhi, na miaka inapokuwa michache kufikia Yubile nyingine atashusha thamani, kwa sababu idadi ya mavuno inahusiana na idadi ya miaka kabla ya Yubile nyingine.
17 Nie będziecie oszukiwać jeden drugiego, lecz będziesz się bał swego Boga, gdyż ja jestem PAN, wasz Bóg.
Msipunjane au kutendeana kwa hila, badala yake, yawapasa kumheshi Yahweh Mungu wenu.
18 Wykonujcie moje ustawy i przestrzegajcie moich praw, i wypełniajcie je, a będziecie mieszkać w tej ziemi bezpiecznie.
Kwa hiyo basi, ni lazima muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza. Nanyi mtaishi katika nchi katika usalama.
19 Ziemia wyda swój plon i będziecie jedli do syta, i będziecie bezpiecznie w niej mieszkać.
Nayo nchi itawapa mavuno yake, nanyi mtakula matunda yenu na mtaishi humo salama.
20 A jeśli powiecie: Cóż będziemy jeść w siódmym roku, jeśli nie będziemy siać ani zbierać naszych plonów?
Labda mtasema, Tutakula nini katika mwaka wa saba? Tazama, hatuwezi kupanda wala kukusanya mazao yetu.”
21 Wtedy rozkażę, żeby moje błogosławieństwo [przyszło] na was w szóstym roku i wyda plon na trzy lata.
Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu katika mwaka wa sita, nayo itatoa mavuno ya kutosha kwa miaka mitatu.
22 I będziecie siać w ósmym roku, ale będziecie jeść ze starego plonu aż do dziewiątego roku; dopóki nie nadejdą jego plony, będziecie jeść stare.
Mtapanda katika mwaka wa nane na mtaendelea kula mazao ya miaka iliyopita na kutoka kwenye ghala la chakula. Mpaka mavuno ya mwaka wa tisa yatakapofika, mtaweza kula kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa katika miaka iliyopita
23 Ziemia nie będzie sprzedawana na zawsze, gdyż ziemia należy do mnie, a wy jesteście u mnie gośćmi i przybyszami.
Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu, kwa sababu ardhi ni mali yangu. Ninyi nyote mu wageni na wakazi wa muda juu ya ardhi yangu.
24 A w całej ziemi waszej posiadłości ustanowicie dla ziemi prawo wykupu.
Ni lazima muitunze haki ya ukombozi kwa ajili ya ardhi yote mtakayoimiliki; itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi kutoka kwao.
25 Jeśli twój brat zubożeje, a sprzeda [coś] ze swojej własności i przyjdzie najbliższy krewny, mający prawo wykupu, to niech wykupi, co jego brat sprzedał.
Iwapo Mwisraeli mwenzako anakuwa masikini na kwa sababu hiyo anauza baadhi ya miliki yake, kisha jamaa yake wa karibu anaweza kuja na kuikomboa hiyo miliki ambayo jamaa yake kaiuza kwako.
26 A jeśli ktoś nie ma nikogo, kto może to wykupić, lecz sam będzie mógł i znajdzie środki na wykup;
Iwapo mtu hana jamaa wa kuikomboa mali yake, lakini ikiwa kafanikiwa na anao uwezo wa kuikomboa,
27 To odliczy lat od swojej sprzedaży, zwróci resztę temu, komu sprzedał, i wróci do swojej posiadłości.
kisha atahesabu miaka tangu ardhi hiyo ilipouzwa na kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia. Naye anaweza kuerejea kwenye miliki yake mwenyewe.
28 Lecz jeśli nie ma środków, aby zwrócić, to pozostanie to, co sprzedał, w ręku tego, który to kupił aż do roku jubileuszowego. W roku jubileuszowym zwolni mu to, a ten wróci do swojej posiadłości.
Lakini ikiwa hawezi kuirejesha kwake ardhi aliyoiuza, nayo hiyo ardhi aliyoiuza itabaki katika umiliki wa yule aliyeinunua mpaka mwaka wa Yubile. Kwenye mwaka wa Yubile, ardhi itarejeshwa kwa mtu aliyeiuza, naye mmiliki wa asili atarejea kwenye mali yake.
29 Jeśli ktoś sprzeda dom mieszkalny w mieście otoczonym murami, będzie miał prawo wykupu do końca roku sprzedaży; będzie miał prawo wykupu przez cały rok.
Ikiwa mtu anauza nyumba iliyo kwenye mji uliozungushiwa ukuta, naye anaweza kuinunua tena ndani ya mwaka baada ya kuuzwa. kwa kuwa, kwa mwaka mzima atakuwa na haki ya ukombozi.
30 A jeśli nie zostanie wykupiony do końca roku, wtedy ten dom w mieście otoczonym murami zostanie własnością na zawsze tego, który go kupił, oraz jego potomków. Nie będzie zwolniony w roku jubileuszowym.
Kama nyumba hiyo haitakombolewa kabla ya mwaka mzima, ndipo hiyo nyumba iliyoko kwenye mji uliozungushiwa ukuta itakuwa mali ya kudumu ya yule aliyeinunua, katika vizazi vyote vya uzao wake. Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa katika mwaka wa Yubile.
31 Ale domy we wsiach, które nie są otoczone murami, będą traktowane na równi z polami ziemi. Będą podlegały prawu wykupu i w roku jubileuszowym zostaną zwolnione.
Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta kuzizunguuka, zitahesabiwa kuwa shamba la nchi. Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe katika mwaka wa Yubile.
32 Co do miast Lewitów i domów w miastach ich posiadłości, to Lewitom zawsze przysługuje prawo wykupu.
Hata hivyo, nyumba zinazomilikiwa na makuhani katika miji yao zaweza kukombelewa wakati wowote.
33 A jeśli ktoś kupuje od Lewitów, to kupiony dom lub miejska posiadłość zostaną zwolnione w roku jubileuszowym, gdyż domy miast Lewitów są ich posiadłością pośród synów Izraela.
Iwapo mmoja wa makuhani haikombowi nyumba iliyozwa, kisha nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe katika mwaka wa Yubile, kwa kuwa nyumba za miji ya makuhani ni mali yao miongoni mwa watu wa Israeli.
34 Ale pole wokół ich miast nie będzie sprzedawane, gdyż jest ich wieczystą posiadłością.
Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa kwa sababu hiyo ni mali ya kudumu ya Makuhani.
35 Jeśli twój brat zubożeje i jego ręka osłabnie przy tobie, wspomożesz go, aby mógł żyć przy tobie jako gość lub przybysz.
Ikiwa mwananchi mwenzako anakuwa masikini, kiasi kwamba hawezi kujihudumia, nawe utalazimika kumsaidia kama vile ungemsaidia mgeni au mwingine yeyote kutoka nje aishie miongoni mwenu.
36 Nie bierz od niego lichwy ani odsetek, lecz bój się swego Boga, aby twój brat mógł się żywić przy tobie.
Usimtoze riba au kujaribu kunufaika kutoka kwake katika njia yoyote, bali mheshimu Mungu wako ili kwamba ndugu yako aendelee kuishi nawe.
37 Nie dasz mu swoich pieniędzy na lichwę ani nie pożyczysz mu swojej żywności dla zysku.
Hutampa mkopo wa fedha na kumtoza riba, wala hutamuuzia chakula chako ili kupata faida.
38 Ja jestem PAN, wasz Bóg, który was wyprowadził z ziemi Egiptu, aby dać wam ziemię Kanaan i być waszym Bogiem.
Mimi ndimi Yahweh Mungu wako, aliye kuleta wewe kutoka nchi ya Misri, ili kwamba Nikupe nchi ya Kanaani, na kwamba niwe Mungu wako.
39 Jeśli też zubożeje twój brat przy tobie i zaprzeda się tobie, nie będziesz go obarczał niewolniczą pracą;
Iwapo mwananchi mwenzako atakuwa masikini na kujiuza mwenyewe kwako, hutamfanyisha kazi kama mtumwa.
40 Będzie u ciebie jako najemnik i jako przybysz; aż do roku jubileuszowego będzie ci służyć.
Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa. Ni lazima awe kama yule ahudumuye nawe kwa muda mpaka mwaka wa Yubile.
41 Potem odejdzie od ciebie, on i jego dzieci z nim, i wróci do swojej rodziny i do posiadłości swoich przodków.
Kisha ataondoka kwako, yeye mwenyewe na watoto wake pamoja naye, na atarejea kwenye familia yake mwenyewe na kwenye miliki ya baba yake.
42 Oni bowiem są moimi sługami, których wyprowadziłem z ziemi Egiptu. Nie będą sprzedawani jako niewolnicy.
Kwa sababu wao ni watumishi wangu niliowaleta kutoka katika nchi ya Misri. Hawatauzwa kama watumwa.
43 Nie będziesz srogo panował nad nimi, ale będziesz się bał swego Boga.
Usitawale juu yao kwa ukatili, bali yakupasa kumheshimu Mungu wako.
44 Twój niewolnik i twoja niewolnica, których będziesz miał, [będą] z tych narodów, które są wokoło was; od nich będziecie kupować niewolnika i niewolnicę.
Kwa upande wa watumwa wako wakiume na watumwa wako wa kike, unaowezao kuwapata kutok kwa mataifa yanayokuzunguka, waweza kununua watumwa kutoka kwao.
45 Także spośród synów przybyszów mieszkających wśród was będziecie kupować i z potomstwa tych, którzy są z wami, urodzonych w waszej ziemi. Oni będą waszą własnością.
Unaweza pia kununua watumwa kutoka kwa wageni wanaoishi miongoni mwenu, yaani, kutoka familia zao waliopamoja nawe, wale wtoto waliozaliwa katika nchi yako. Wanaweza kuwa mali yako.
46 Będziecie ich przekazywać waszym dzieciom w dziedzictwie, na dziedziczną własność; będą wam służyć na zawsze. Lecz nad waszymi braćmi, synami Izraela, nikt z was nie będzie srogo panował.
Unaweza kuzalisha watumwa hao kama urithi kwa watoto wako baada yako, ili kuwamiliki kama mali. Kutoka kwao waweza kununua watumwa daima, lakini hamtawezi kutawala kwa ukali juu ya ndugu zenu walio miogoni mwa watu wa Israeli.
47 A jeśli gość lub przybysz wzbogaci się przy tobie, a twój brat zubożeje przy nim i sprzeda się gościowi lub przybyszowi przy tobie lub potomstwu rodziny przybysza;
Iwapo mgeni anayeishi nawe kwa muda anakuwa tajiri, na ikiwa mmoja wa Waisraeli amekuwa masikini na kujuza mwenyewe kwa familia ya mgeni, au kwa mtu fulani katika familia,
48 To po sprzedaniu może zostać wykupiony; ktokolwiek z jego braci może go wykupić;
baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa. Anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Iwapo anaweza kurejeshwa. Mtu fulani katika familia yake anaweza kumkomboa.
49 Albo jego stryj, albo syn jego stryja może go wykupić, albo ktokolwiek z jego bliskich krewnych z jego rodziny może go wykupić, albo jeśli go stać, sam siebie wykupi.
Anaweza kuwa mjomba wake, au mjomba wa mwanawe, anayemkomboa yeye, au yeyote aliye ndugu yake wa karibu kutoka kwa ukoo wake. Au, iwapo ni mwenye mafanikio, anaweza kujikomboa mwenyewe.
50 I rozliczy się ze swoim nabywcą od roku swego sprzedania aż do roku jubileuszowego; a pieniądze, za które się sprzedał, zostaną obliczone według liczby lat; postąpi z nim jak z najemnikiem.
Ni lazima apatane na mtu aliyemnunua, itawapasa kuhesabu miaka tangu mwaka aliojiuza kwa mnunuzi wake mpaka mwaka wa Yubile. Ile thamani ya ukombozi wake ihesabiwe kulingana na kiwango cha mshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa, kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi kwa yule aliyemnunua.
51 Jeśli zostało jeszcze wiele lat, to według ich liczby zwróci swój wykup z pieniędzy, za które został kupiony.
Endapo kutakuwa kungali na miaka mingi iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atalazimika kulipa fungu kubwa la fedha kwa ajili ya ukombozi ambao ni uwino wa idadi ya miaka hiyo.
52 A jeśli do roku jubileuszowego zostało niewiele lat, to rozliczy się z nim i według ich liczby tych lat zwróci swój wykup.
Iwapo kuna miaka michache tu iliyobaki mpaka mwaka wa Yubile, atapatana na aliyemnunua ili kuipitia idadi ya miaka iliyobaki mpaka Yubile, naye atalazimika kulipia ukombozi wake kulingana na idadi ya miaka.
53 Będzie u niego jako najemnik, rok po roku; nie będzie nad nim srogo panował na twoich oczach.
Naye atatendewa kama mtu aliyeajiriwa mwaka kwa mwaka. Utahakikisha kwamba hatendewi kwa ukali.
54 A jeśli nie zostanie wykupiony tymi sposobami, wtedy wyjdzie wolny w roku jubileuszowym, on razem ze swoimi dziećmi;
Iwapo hakukombolewa katika njia hizi, basi atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake.
55 Bo synowie Izraela są moimi sługami. Są moimi sługami, których wyprowadziłem z ziemi Egiptu. Ja jestem PAN, wasz Bóg.
Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi. Wao ni watumishi wangu ambao Niliwatoa katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.