< Jozuego 18 >

1 Wtedy całe zgromadzenie synów Izraela zebrało się w Szilo i wznieśli tam Namiot Zgromadzenia, gdyż ziemia została przez nich opanowana.
Kusanyiko lote la Waisraeli likakusanyika huko Shilo na kusimamisha Hema la Kukutania. Nchi ikawa chini ya utawala wao,
2 A pozostało wśród synów Izraela siedem pokoleń, którym nie przydzielono ich dziedzictwa.
lakini palikuwa bado makabila saba ya Israeli ambayo yalikuwa hayajapokea urithi wao.
3 Wtedy Jozue powiedział do synów Izraela: Jak długo będziecie zwlekać z tym, aby wejść i posiąść ziemię, którą dał wam PAN, Bóg waszych ojców?
Hivyo Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtasubiri hata lini ili kuingia kumiliki nchi ambayo Bwana, Mungu wa baba zenu, amewapa?
4 Wybierzcie spośród siebie po trzech mężczyzn [z każdego] pokolenia, których poślę, aby obeszli ziemię i opisali ją według ich dziedzictwa, a potem powrócą do mnie.
Chagueni watu watatu kutoka kwenye kila kabila. Nitawatuma hao watu kukagua hiyo nchi na kuniandikia mapendekezo ya mgawanyo wa urithi wa kila kabila. Nao watanirudia.
5 I podzielą ją na siedem części: Juda pozostanie w swych granicach na południu, a dom Józefa pozostanie w swych granicach na północy.
Mtaigawanya hiyo nchi katika sehemu saba. Yuda atabaki katika eneo lake upande wa kusini na nyumba ya Yosefu katika nchi yake upande wa kaskazini.
6 Sporządźcie więc opis ziemi, [dzieląc ją] na siedem części, i przynieście [go] tu do mnie, a ja rzucę dla was losy tu przed PANEM, naszym Bogiem.
Baada ya kuandika maelezo ya hizo sehemu saba za nchi, yaleteni kwangu, nami nitawapigia kura kwa kura mbele za Bwana Mungu wetu.
7 Lewici bowiem nie mają działu pośród was, gdyż ich dziedzictwem jest kapłaństwo PANA; a Gad, Ruben i połowa pokolenia Manassesa otrzymali swe dziedzictwa po wschodniej stronie Jordanu, które dał im Mojżesz, sługa PANA.
Hata hivyo, Walawi hawatakuwa na sehemu miongoni mwenu, kwa maana huduma ya ukuhani kwa Bwana ndio urithi wao. Nao Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase wameshapata urithi wao upande wa mashariki mwa Yordani, ambako Mose mtumishi wa Bwana aliwapa.”
8 Wtedy ci mężczyźni wstali i poszli, a Jozue nakazał tym, którzy szli, aby opisali ziemię: Idźcie i obejdźcie ziemię, i opiszcie ją, a potem wróćcie do mnie, a ja rzucę dla was losy przed PANEM tu, w Szilo.
Watu hao walipokuwa wanaondoka kwenda kuandika vizuri kuhusu hiyo nchi, Yoshua akawaagiza, “Nendeni mkakague hiyo nchi na mwandike maelezo kuihusu. Kisha mrudi kwangu, nami nitawapigia kura hapa Shilo mbele za Bwana.”
9 Odeszli więc ci mężczyźni i obchodzili ziemię, i opisali ją w księdze według miast, [dzieląc] na siedem części; potem wrócili do Jozuego, do obozu w Szilo.
Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.
10 I Jozue rzucił dla nich losy w Szilo przed PANEM, i tam podzielił Jozue ziemię synom Izraela według ich przydziałów.
Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.
11 I padł los dla pokolenia synów Beniamina według ich rodzin, a granica ich losu wypadła między synami Judy a synami Józefa.
Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.
12 Ich granica po stronie północnej zaczynała się od Jordanu, biegła na północne zbocze Jerycha, ciągnęła się przez góry na zachód i kończyła się przy pustyni Bet-Awen.
Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.
13 A stamtąd granica biegła do Luz, od strony południowej Luz, czyli Betel, a schodziła do Atarot-Addar pod górę, która leży na południe od dolnego Bet-Choron.
Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.
14 Potem granica skręcała obok morza na południe od góry położonej naprzeciw Bet-Choron na południu, i kończyła się w Kiriat-Baal, czyli Kiriat-Jearim, mieście synów Judy. To jest strona zachodnia.
Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.
15 Strona zaś południowa [zaczynała się] od końca Kiriat-Jearim; następnie granica biegła na zachód i dochodziła do źródła wód Neftoach.
Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.
16 I granica ta ciągnęła się do końca góry położonej naprzeciw doliny syna Hinnom, leżącej w dolinie Refaim na północy, i schodziła do doliny Hinnom po stronie Jebus na południe, i stamtąd biegła do źródła Rogiel.
Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.
17 Potem skręcała na północ i dochodziła do En-Szemesz, i dalej do Gelilot, które jest naprzeciw wzniesienia Adummim, stamtąd schodziła do kamienia Bohana, syna Rubena.
Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.
18 Następnie przebiegała ku zboczu, które było naprzeciw Araby na północ, i ciągnęła się do Araby.
Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.
19 Stamtąd granica biegła do zbocza Bet-Chogla na północy, a kończyła się przy zatoce północnej Morza Słonego, na południu od ujścia Jordanu. To [była] granica południowa.
Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.
20 Jordan zaś stanowi granicę od strony wschodniej. To było dziedzictwo synów Beniamina według otaczających jego granic, według ich rodzin.
Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.
21 A miastami pokolenia synów Beniamina według ich rodzin były: Jerycho, Bet-Chogla i dolina Kesis;
Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,
22 Bet-Araba, Semaraim, Betel;
Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,
23 Awwim, Para, Ofra;
Avimu, Para na Ofra,
24 Kefar-Ammonaj, Ofni i Geba: dwanaście miast wraz z przyległymi do nich wioskami.
Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
25 Gibeon, Rama, Beerot;
Gibeoni, Rama na Beerothi,
26 Mispa, Kefira, Mosa;
Mispa, Kefira, Moza,
27 Rekem, Jerpeel, Tarala;
Rekemu, Irpeeli, Tarala,
28 Sela, Elef, Jebus, czyli Jerozolima, Gibeat i Kiriat: czternaście miast wraz z przyległymi do nich wioskami. To było dziedzictwo synów Beniamina według ich rodzin.
Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.

< Jozuego 18 >