< Hioba 8 >
1 Wtedy Bildad z Szuach odpowiedział:
Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
2 Jak długo będziesz mówił takie rzeczy? [Jak długo] słowa z twoich ust [będą jak] gwałtowny wiatr?
“hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
3 Czy Bóg wypacza sąd? Czy Wszechmocny wypacza sprawiedliwość?
Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
4 Jeśli twoi synowie zgrzeszyli przeciwko niemu, a on ich odrzucił za ich nieprawość;
Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
5 Jeśli zwrócisz się pilnie do Boga i będziesz błagać Wszechmocnego;
Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
6 Jeśli jesteś czysty i prawy, wtedy na pewno obudzi się dla ciebie i poszczęści mieszkaniu twojej sprawiedliwości.
Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
7 A [choćby] twój początek był niewielki, jednak twój koniec bardzo się rozmnoży.
Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
8 Bo zapytaj, proszę, dawnych pokoleń i rozważ doświadczenie ich ojców;
Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
9 (My bowiem jesteśmy wczorajsi i nic nie wiemy, ponieważ nasze dni na ziemi są [jak] cień).
(Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
10 Czy oni nie pouczą cię i nie powiedzą ci, i czy z ich serc nie wypłyną słowa?
Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
11 Czy sitowie urośnie bez wilgoci? Czy trzcina urośnie bez wody?
Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
12 Chociaż jeszcze jest świeża i nieskoszona, prędzej usycha niż inna trawa.
Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
13 Takie [są] drogi wszystkich, którzy zapominają Boga, i [tak] zginie nadzieja obłudnika.
Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
14 Jego nadzieja zostanie podcięta, a jego ufność [będzie] jak pajęczyna.
Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
15 Oprze się o swój dom, ale się nie ostoi; uchwyci się go, ale nie przetrwa.
Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
16 Zieleni się na słońcu i w ogrodzie jego świeża latorośl wyrasta.
Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
17 Jego korzenie są splątane wśród kamieni i wyrastają spośród nich.
Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
18 Ale gdy go wyrwą z jego miejsca, wtedy miejsce to wyprze się go, [mówiąc]: Nie widziałem cię.
Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
19 Takie oto [jest] szczęście jego drogi, a z ziemi wyrosną inni.
Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
20 Oto Bóg nie odrzuci [człowieka] prawego, ale złoczyńcom nie poda ręki;
Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
21 Aż się napełnią twoje usta uśmiechem, a twoje wargi radością.
Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
22 Gdyż ci, którzy cię nienawidzą, okryją się hańbą, a namiotu niegodziwych [już] nie będzie.
Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.