< Izajasza 22 >
1 Brzemię Doliny Widzenia. Co ci się stało, że cała wystąpiłaś na dachy?
Neno kuhusu Bonde la Maono: Nini kinachokutaabisha sasa, kwamba ninyi nyote mmepanda juu ya mapaa?
2 Miasto pełne wrzasku i zgiełku, miasto wesołe! Twoi zabici nie padli od miecza ani nie zginęli w bitwie.
Ewe mji uliojaa ghasia, ewe mji wa makelele na sherehe! Watu wenu waliokufa hawakuuawa kwa upanga, wala hawakufa vitani.
3 Wszyscy twoi dowódcy pierzchli razem, związani przez łuczników. Zostali związani razem ci, których znaleziono u ciebie, ci, którzy uciekli z daleka.
Viongozi wako wote wamekimbia pamoja, wamekamatwa bila kutumia upinde. Ninyi nyote mliokamatwa mlichukuliwa wafungwa pamoja, mlikimbia wakati adui alipokuwa bado mbali.
4 Dlatego powiedziałem: Odwróćcie swój wzrok ode mnie, abym gorzko zapłakał; nie próbujcie mnie pocieszać z powodu spustoszenia córki mojego ludu.
Kwa hiyo nilisema, “Geukia mbali nami, niache nilie kwa uchungu. Usijaribu kunifariji juu ya maangamizi ya watu wangu.”
5 To jest bowiem dzień ucisku, deptania i zamieszania od Pana, BOGA zastępów, w Dolinie Widzenia, [dzień] burzenia murów i wołania na góry.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, anayo siku ya ghasia, ya kukanyaga, na ya kuogofya katika Bonde la Maono, siku ya kuangusha kuta na ya kupiga kelele mpaka milimani.
6 Elam wziął kołczan z rydwanami ludu wojennego, a Kir odsłonił swoją tarczę.
Elamu analichukua podo, pamoja na waendesha magari ya vita na farasi. Kiri anaifungua ngao.
7 I stało się tak, że najpiękniejsze doliny były pełne rydwanów, a jeźdźcy ustawili się potężnie przy bramie.
Mabonde yako yaliyo mazuri sana yamejaa magari ya vita, nao wapanda farasi wamewekwa kwenye malango ya mji;
8 I odkryto osłonę Judy, i w tym dniu spoglądałeś na zbrojownię w Domu Lasu.
ulinzi wa Yuda umeondolewa. Nawe ulitazama siku ile silaha katika Jumba la Kifalme la Mwituni,
9 I spoglądaliście na wyłomy miasta Dawida – na to, że były liczne, i zgromadziliście wody Dolnej Sadzawki.
mkaona kuwa Mji wa Daudi una matundu mengi katika ulinzi wake, mkaweka akiba ya maji kwenye Bwawa la Chini.
10 Policzyliście domy w Jerozolimie i burzyliście domy, aby wzmocnić mur.
Mlihesabu majengo katika Yerusalemu nanyi mkabomoa nyumba ili kuimarisha ukuta.
11 Zrobiliście też zbiornik między dwoma murami na wodę Starej Sadzawki, ale nie spoglądaliście na jej twórcę ani nie widzieliście tego, który od dawna ją ukształtował.
Mlijenga bwawa la maji katikati ya kuta mbili kwa ajili ya maji ya Bwawa la Zamani, lakini hamkumtazama Yule aliyelitengeneza, au kuwa na heshima kwa Yule aliyeubuni tangu zamani za kale.
12 W tym dniu Pan, BÓG zastępów, wzywał do płaczu i do żałoby, do ostrzyżenia się i do przepasania się worem.
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliwaita siku ile ili kulia na kuomboleza, kungʼoa nywele zenu na kuvaa nguo ya gunia.
13 A oto radość i wesele, zabijanie wołów i owiec, spożywanie mięsa i picie wina: Jedzmy, pijmy, bo jutro umrzemy.
Lakini tazama, kuna furaha na sherehe, kuchinja ngʼombe na kuchinja kondoo, kula nyama na kunywa mvinyo! Mnasema, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa!”
14 Ale PAN zastępów objawił mi to, [mówiąc] do [mych] uszu: Na pewno ta nieprawość nie będzie wam przebaczona aż do śmierci, mówi Pan, BÓG zastępów.
Bwana Mwenye Nguvu Zote amelifunua hili nikiwa ninasikia: Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asema: “Mpaka siku ya kufa kwenu, dhambi hii haitafanyiwa upatanisho.”
15 Tak mówi Pan, BÓG zastępów: Idź, udaj się do tego skarbnika, do Szebny, przełożonego domu, i powiedz:
Hili ndilo Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Nenda ukamwambie huyu wakili Shebna, ambaye ni msimamizi wa jumba la kifalme:
16 Co ty tu masz i kogo tu masz, że wykułeś sobie w tym miejscu grób? Wykułeś sobie grób wysoko, wydrążyłeś sobie w skale swoje mieszkanie.
Unafanya nini hapa, na ni nani aliyekupa ruhusa kujikatia kaburi lako mwenyewe, ukichonga kaburi lako mahali palipo juu, na kutoboa kwa patasi mahali pako pa kupumzikia katika mwamba?
17 Oto PAN, który cię przykrył jak zacnego człowieka i który cię kosztownie przyoblekł;
“Jihadhari, Bwana yu karibu kukukamata thabiti, na kukutupa mbali, ewe mtu mwenye nguvu.
18 Tocząc cię, zwinie i rzuci jak kulę w przestronną ziemię. Tam umrzesz, tam też rydwany twojej chwały będą hańbą domu twego pana.
Atakuvingirisha uwe kama mpira na kukutupa katika nchi kubwa. Huko ndiko utakakofia, na huko ndiko magari yako ya vita ya fahari yatabakia, wewe unayeifedhehesha nyumba ya bwana wako!
19 Wypędzę cię z twego stanowiska, z twego urzędu ściągnę cię.
Nitakuondoa kutoka kazi yako, nawe utaondoshwa kutoka nafasi yako.
20 W tym dniu powołam swego sługę Eliakima, syna Chilkiasza.
“Katika siku ile, nitamwita mtumishi wangu, Eliakimu mwana wa Hilkia.
21 I ubiorę go w twoją szatę, i przepaszę go twoim pasem, i oddam w jego ręce twoją władzę; i będzie on ojcem dla mieszkańców Jerozolimy i domu Judy.
Nitamvika joho lako, nami nitamfunga mshipi wako kiunoni mwake, na kumkabidhi mamlaka yako. Yeye atakuwa baba kwa wale wanaoishi Yerusalemu na kwa nyumba ya Yuda.
22 I położę klucz domu Dawida na jego ramieniu; gdy on otworzy, nikt nie zamknie, a gdy zamknie, nikt nie otworzy.
Nitaweka mabegani mwake ufunguo wa nyumba ya Daudi. Kile afunguacho hakuna awezaye kufunga, na kile afungacho hakuna awezaye kufungua.
23 I wbiję go jak gwóźdź na miejscu pewnym, a będzie tronem chwały dla domu swego ojca.
Nitamgongomea kama kigingi kilicho mahali palipo imara, naye atakuwa kiti cha enzi cha heshima kwa ajili ya nyumba ya baba yake.
24 I zawieszą na nim całą chwałę domu jego ojca, synowie i córki, wszelkie drobne naczynia, od kubków do wszelkich dzbanów.
Utukufu wote wa jamaa yake utakuwa juu yake: Watoto wa jamaa hiyo na machipukizi yake, vyombo vyake vyote vidogo, tangu bakuli hadi magudulia yote.”
25 W tym dniu, mówi PAN zastępów, gwóźdź, który był wbity w miejscu pewnym, zostanie wyjęty i przycięty, i spadnie; a brzemię, które wisiało na nim, zostanie odcięte. Tak bowiem PAN to powiedział.
Bwana Mwenye Nguvu Zote asema, “Katika siku ile, kigingi kilichogongomewa mahali imara kitaachia njia. Kitakatwa, nacho kitaanguka na mzigo ulioningʼinia juu yake utaanguka chini.” Bwana amesema.