< Hebrajczyków 12 >

1 Skoro i my mamy wokół siebie tak wielką chmurę świadków, zrzućmy z siebie wszelki ciężar i grzech, który nas tak łatwo osacza, w cierpliwości biegnijmy w wyznaczonym nam wyścigu;
Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, na dhambi ile inayotung'ang'ania. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu.
2 Patrząc na Jezusa, twórcę i dokończyciela wiary, który z powodu przygotowanej mu radości wycierpiał krzyż, nie zważając na hańbę, i zasiadł po prawicy tronu Boga.
Tumwelekee Yesu ambaye ndiye aliyeianzisha imani yetu na ambaye ataikamilisha. Kwa ajili ya furaha iliyokuwa inamngojea, yeye alivumilia kifo msalabani, bila kujali juu ya aibu yake, na sasa anaketi upande wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.
3 Pomyślcie więc o tym, który zniósł tak wielki sprzeciw wobec siebie ze strony grzeszników, abyście nie zniechęcali się w waszych umysłach i nie ustawali.
Fikirini juu ya mambo yaliyompata Yesu, jinsi alivyostahimili upinzani mkubwa kwa watu wenye dhambi. Basi, msife moyo, wala msikate tamaa.
4 Jeszcze nie stawialiście oporu aż do krwi, walcząc przeciwko grzechowi;
Maana katika kupambana na dhambi, ninyi hamjapigana mpaka kiasi cha kumwaga damu yenu.
5 I zapomnieliście o napomnieniu, które jest kierowane do was jako synów: Mój synu, nie lekceważ karania Pana i nie zniechęcaj się, gdy on cię napomina.
Je, mmesahau yale maneno ya kutia moyo ambayo Mungu anawataja ninyi kuwa wanawe? “Mwanangu, usidharau adhabu ya Bwana, wala usife moyo anapokukanya.
6 Kogo bowiem Pan miłuje, tego karze, a chłoszcze każdego, którego za syna przyjmuje.
Maana Bwana humwadhibu kila anayempenda, humpinga kila anayekubali kuwa mwanae.”
7 Jeśli znosicie karanie, Bóg obchodzi się z wami jak z synami. Jaki to bowiem syn, którego ojciec nie karze?
Vumilieni adhabu kwani ni mafundisho; Mungu huwatendea ninyi kama wanawe. Maana ni mwana gani asiyeadhibiwa na baba yake?
8 A jeśli jesteście bez karania, którego wszyscy są uczestnikami, wtedy jesteście bękartami, a nie synami.
Lakini msipoadhibiwa kama wana wengine, basi, ninyi si wanawe, bali ni wana haramu.
9 Poza tym nasi cieleśni ojcowie nas karali, a szanowaliśmy ich. Czyż nie tym bardziej powinniśmy poddać się Ojcu duchów, abyśmy żyli?
Zaidi ya hayo sisi tunawaheshimu wazazi wetu waliotuzaa hata wanapotuadhibu. Basi, tunapaswa kumtii zaidi Baba yetu wa kiroho ili tupate kuishi.
10 Tamci bowiem karali nas przez krótki czas według swego uznania. Ten zaś [czyni to] dla [naszego] dobra, abyśmy byli uczestnikami jego świętości.
Wazazi wetu hapa duniani walituadhibu kwa muda, kama wao wenyewe walivyoona kuwa vema; lakini Mungu anatuadhibu kwa ajili ya faida yetu wenyewe, tupate kuushiriki utakatifu wake.
11 A żadne karanie w danej chwili nie wydaje się radosne, ale smutne. Potem jednak przynosi błogi owoc sprawiedliwości tym, którzy przez nie byli ćwiczeni.
Kuadhibiwa si jambo la kufurahisha bali la kuhuzunisha. Lakini wale waliofunzwa kuwa na nidhamu mwishowe watavuna tuzo la amani kutoka katika maisha adili!
12 Dlatego wyprostujcie opadłe ręce i omdlałe kolana.
Basi, inueni mikono yenu inayolegea na kuimarisha magoti yenu yaliyo dhaifu.
13 Prostujcie ścieżki dla waszych stóp, aby to, co chrome, nie zeszło z drogi, ale raczej zostało uzdrowione.
Endeleeni kutembea katika njia iliyonyoka, ili kile kilicholemaa kisiumizwe, bali kiponywe.
14 Dążcie do pokoju ze wszystkimi i do świętości, bez której nikt nie ujrzy Pana.
Jitahidini kuishi kwa amani na watu wote. Ishini maisha ya utakatifu, kwa sababu hakuna mtu atakayemwona Bwana bila ya maisha kama hayo.
15 Uważajcie, żeby nikt nie pozbawił się łaski Boga, żeby jakiś korzeń goryczy, wyrastając, nie wyrządził szkody i aby przez niego nie skalało się wielu;
Jitahidini sana mtu yeyote asije akapoteza neema ya Mungu. Muwe waangalifu ili mti mchungu usizuke kati yenu na kuwaua wengi kwa sumu yake.
16 Żeby nie było żadnego rozpustnika lub bezbożnika jak Ezaw, który za jedną potrawę sprzedał swoje pierworodztwo.
Jihadharini ili miongoni mwenu pasiwe na mtu mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, aliyeuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwa mlo mmoja.
17 Wiecie przecież, że potem, gdy chciał odziedziczyć błogosławieństwo, został odrzucony. Nie znalazł bowiem miejsca na pokutę, choć ze łzami jej szukał.
Ninyi mnafahamu kwamba hata alipotaka kuipata tena ile baraka iliyokuwa yake, alikataliwa, maana hakupata tena nafasi ya kutubu, ingawa aliitafuta kwa machozi.
18 Bo nie podeszliście do góry, która da się dotknąć i płonącej ogniem, do mroku, ciemności i burzy;
Ninyi hamkuwasili mlimani Sinai, ambao unaweza kushikika kama walivyofanya watu wa Israeli, hamkufika kwenye moto uwakao, penye giza, tufani,
19 Ani do dźwięku trąby i [takiego] głosu słów, że ci, którzy go słyszeli, prosili, aby już do nich nie mówiono;
mvumo wa tarumbeta na sauti ya maneno. Wale waliosikia sauti hiyo waliomba wasisikie tena neno jingine,
20 (Nie mogli bowiem znieść tego rozkazu: Gdyby nawet zwierzę dotknęło góry, będzie ukamienowane lub przebite strzałą.
kwani hawakuweza kustahimili amri iliyotolewa: “Atakayegusa mlima huu, hata kama ni mnyama, atapigwa mawe.”
21 A tak straszne było to zjawisko, [że] Mojżesz powiedział: Jestem przerażony i drżę; )
Hayo yote yalionekana ya kutisha mno, hata Mose akasema, “Naogopa na kutetemeka.”
22 Lecz podeszliście do góry Syjon i do miasta Boga żywego, [do] niebiańskiego Jeruzalem i do niezliczonej rzeszy aniołów;
Lakini ninyi mmefika katika mlima wa Sioni, kwenye mji wa Mungu aliye hai. Mmefika Yerusalemu, mji wa mbinguni, ambapo wamekusanyika malaika elfu nyingi wasiohesabika.
23 Na powszechne zebranie, do zgromadzenia pierworodnych, którzy są zapisani w niebie, [do] Boga, sędziego wszystkich, [do] duchów sprawiedliwych uczynionych doskonałymi;
Mmefika kwenye kusanyiko kubwa la wazaliwa wa kwanza wa Mungu, ambao majina yao yameandikwa mbinguni. Mnasimama mbele ya Mungu aliye hakimu wa wote, na mbele ya roho za watu waadilifu waliofanywa kuwa wakamilifu.
24 I do pośrednika nowego przymierza, Jezusa, do krwi, którą się kropi, a która mówi lepsze rzeczy niż [krew] Abla.
Mmefika kwa Yesu ambaye ameratibisha agano jipya, na ambaye damu yake iliyomwagika inasema mambo mema zaidi kuliko ile ya Abeli.
25 Uważajcie, abyście nie odtrącili tego, który przemawia. Jeśli bowiem tamci nie uniknęli [kary], odtrąciwszy tego, który na ziemi mówił, tym bardziej my, jeśli odwrócimy się od tego, który [przemawia] z nieba;
Basi, jihadharini msije mkakataa kumsikiliza yeye ambaye anasema nanyi. Kama wale walikataa kumsikiliza yule aliyewaonya hapa duniani hawakuokoka, sisi tutawezaje kuokoka kama tukikataa kumsikiliza yule anayetuonya kutoka mbinguni?
26 Którego głos wstrząsnął wówczas ziemią, a teraz obiecuje, mówiąc: Jeszcze raz wstrząsnę nie tylko ziemią, ale i niebem.
Wakati ule sauti ilitetemesha nchi, lakini sasa ameahidi: “Nitatetemesha nchi tena, lakini si nchi tu bali pia mbingu.”
27 A słowa „jeszcze raz” ukazują usunięcie tego, co się chwieje, jako tego, co stworzone, aby pozostało to, co się nie chwieje.
Neno hili: “tena” linatuonyesha kwamba vitu vyote vilivyoumbwa vitatetemeshwa na kutoweka ili vibaki vile visivyotetemeshwa.
28 Dlatego otrzymując królestwo niezachwiane, miejmy łaskę, przez którą [możemy] służyć Bogu tak, jak mu się to podoba, z czcią i bojaźnią.
Sisi basi, na tushukuru kwani tunapokea utawala usiotikisika. Tuwe na shukrani na kumwabudu Mungu kwa namna itakayompendeza, kwa ibada na hofu;
29 Nasz Bóg bowiem jest ogniem trawiącym.
maana Mungu wetu kweli ni moto mkali unaoteketeza.

< Hebrajczyków 12 >