< Ezechiela 40 >

1 W dwudziestym piątym roku naszego wygnania, na początku roku, dziesiątego [dnia] miesiąca, czternaście lat po zburzeniu miasta, w tym właśnie dniu spoczęła na mnie ręka PANA i zaprowadził mnie tam.
Katika mwaka wa ishirini na tano wa uhamisho wetu, mwanzoni mwa huo mwaka, siku ya kumi ya mwezi, katika mwaka wa kumi na nne baada ya kuanguka kwa mji, siku hiyo hiyo mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanipeleka huko.
2 W widzeniach Bożych przywiódł mnie do ziemi Izraela i postawił na bardzo wysokiej górze, na której było coś jakby budowa miasta, na południu.
Nikiwa katika maono ya Mungu alinichukua mpaka nchi ya Israeli, naye akaniweka kwenye mlima mrefu sana, ambako upande wa kusini kulikuwepo baadhi ya majengo ambayo yalionekana kama mji.
3 I zaprowadził mnie tam, a oto mąż, który z wyglądu był jakby ze spiżu, miał lniany sznur w ręku i pręt mierniczy, a stał w bramie.
Akanipeleka huko, nami nikamwona mtu ambaye kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwa shaba. Alikuwa amesimama kwenye lango akiwa na kamba ya kitani na ufito wa kupimia mkononi mwake.
4 I przemówił do mnie ten mąż: Synu człowieczy, popatrz swymi oczami, słuchaj swymi uszami i weź sobie do serca wszystko, co ci pokażę. Po to bowiem zostałeś tu przyprowadzony, aby ci to pokazać. Oznajmij wszystko, co widzisz, domowi Izraela.
Mtu huyo akaniambia, “Mwanadamu, angalia kwa macho yako na usikie kwa masikio yako nawe uzingatie kitu nitakachokuonyesha, kwa kuwa ndiyo sababu umeletwa hapa. Iambie nyumba ya Israeli kila kitu utakachoona.”
5 I oto mur otaczał dom ze wszystkich stron dokoła, a w ręku tego męża [był] pręt mierniczy na sześć łokci – liczonych jako łokieć i szerokość dłoni – i wymierzył grubość budowli – jeden pręt, i wysokość – jeden pręt.
Nikaona ukuta uliozunguka eneo lote la Hekalu. Ule ufito wa kupimia uliokuwa mkononi mwa yule mtu ulikuwa na urefu wa dhiraa ndefu sita, yaani, dhiraa ndefu ni sawa na dhiraa na nyanda nne, akapima ule ukuta. Ukuta huo ulikuwa na unene wa dhiraa ndefu sita na kimo cha dhiraa ndefu sita.
6 Potem wszedł do bramy, która była [zwrócona] ku wschodowi, wszedł po schodach i zmierzył próg bramy: jeden pręt szerokości, a drugi próg [miał] jeden pręt szerokości.
Kisha akaenda kwenye lango linaloelekea mashariki. Akapanda ngazi zake akapima kizingiti cha lango, nacho kilikuwa na kina cha huo ufito.
7 Każda wnęka miała jeden pręt długości i jeden pręt szerokości, a między wnękami był [odstęp] na pięć łokci; próg bramy obok przedsionka bramy od wewnątrz [wynosił] jeden pręt.
Vyumba vya kupumzikia vya walinzi vilikuwa na urefu wa huo ufito mmoja na upana wa huo ufito, kuta zilizogawa vyumba hivyo vya mapumziko zilikuwa na unene wa dhiraa tano. Nacho kizingiti cha lango lililokuwa karibu na ukumbi unaoelekea hekaluni ulikuwa na kina cha huo ufito.
8 I zmierzył przedsionek bramy od wewnątrz – jeden pręt.
Kisha akapima baraza ya njia ya lango,
9 Zmierzył też przedsionek bramy – osiem łokci, a jej filary – dwa łokcie. Przedsionek bramy był wewnątrz.
ambayo ilikuwa na kina cha dhiraa nane na miimo yake ilikuwa na unene wa dhiraa mbili. Baraza ya lango ilielekea Hekalu.
10 Wnęki bramy wschodniej [były] trzy z jednej i trzy z drugiej strony; wszystkie trzy miały ten sam wymiar. Jeden wymiar miały też filary po obu stronach.
Ndani ya lango la mashariki kulikuwepo vyumba vitatu vya kupumzikia kila upande, vyote vitatu vilikuwa na vipimo vilivyo sawa, nazo nyuso za kuta zilizotenganisha kila upande zilikuwa na vipimo vilivyo sawa.
11 Zmierzył też szerokość wejścia bramy – dziesięć łokci, [a] długość bramy – trzynaście łokci.
Kisha akapima upana wa ingilio la lango, ilikuwa dhiraa kumi na urefu wake ulikuwa dhiraa kumi na tatu.
12 Przed wnękami była także przegroda na jeden łokieć, jeden łokieć miała też przegroda po drugiej stronie. [Każda] wnęka miała po sześć łokci z jednej i sześć łokci z drugiej strony.
Mbele ya kila chumba cha kupumzikia kulikuwepo ukuta uliokuwa na kimo cha dhiraa moja kwenda juu, navyo hivyo vyumba vilikuwa dhiraa sita mraba.
13 Potem zmierzył bramę od dachu [jednej] wnęki aż do dachu drugiej, szerokość była na dwadzieścia pięć łokci, a drzwi [były] naprzeciwko siebie.
Kisha akapima njia ya lango kuanzia juu ya ukuta wa nyuma wa chumba kimoja cha kupumzikia hadi juu ya ukuta wa nyuma wa chumba upande wa pili; kukawa na nafasi ya dhiraa ishirini na tano kuanzia lango la ukuta mmoja hadi lango la ukuta uliokuwa upande mwingine.
14 I uczynił filary na sześćdziesiąt łokci, a każdy filar na dziedzińcu u bramy wokoło [miał jedną miarę].
Akapima pia ukumbi, urefu wa dhiraa ishirini na lango linalofuatia hiyo nguzo kila upande wa huo ukumbi.
15 A od fasady bramy wejściowej do fasady przedsionka wewnątrz bramy [było] pięćdziesiąt łokci.
Umbali kuanzia ingilio la njia ya lango hadi mwisho kabisa wa baraza yake ulikuwa dhiraa hamsini.
16 [Były] też wąskie okna we wnękach, przy filarach wewnątrz bramy dokoła, a także przy przedsionkach. Dokoła od wewnątrz były okna, a na filarach [były] palmy.
Kulikuwa na vidirisha kwenye hivyo vyumba vya walinzi na nguzo za hivyo vyumba zilikuwa kwenye mzunguko wa hilo lango, vivyo hivyo kulikuwa na madirisha yaliyozunguka kuelekeana na ua na juu ya kila nguzo kulikuwa na mapambo ya miti ya mitende.
17 Potem przyprowadził mnie na dziedziniec zewnętrzny, a oto [znajdowały] się [tam] komory i posadzka uczyniona na dziedzińcu zewsząd dokoła: trzydzieści komór [było] na tej posadzce.
Kisha akanileta katika ukumbi wa nje. Huko nikaona vyumba vingine pamoja na njia iliyokuwa imejengwa kuzunguka ukumbi wote, kulikuwa na vyumba thelathini vimepangana kando ya hiyo njia.
18 A posadzka [była] wzdłuż bram, odpowiednio do długości bram. Była to posadzka dolna.
Njia hii iliyojengwa iliambaa na lango, ikiwa na urefu sawa na lango, hii ilikuwa ni njia ya chini.
19 Potem zmierzył odległość od fasady bramy dolnej do fasady [bramy] dziedzińca wewnętrznego z zewnątrz: sto łokci w kierunku wschodnim i północnym.
Kisha akapima umbali kutoka ndani ya lango la chini mpaka nje ya ukumbi wa ndani, nao ulikuwa dhiraa mia moja upande wa mashariki na dhiraa mia moja upande wa kaskazini.
20 Zmierzył też długość i szerokość bramy północnej na dziedzińcu zewnętrznym.
Kisha akapima urefu na upana wa lango linaloelekea kaskazini, kukabili ukumbi wa nje.
21 Miała trzy wnęki z jednej i trzy z drugiej strony; jej filary i przedsionki miały taki sam wymiar jak pierwsza brama: pięćdziesiąt łokci długości i dwadzieścia pięć łokci szerokości.
Vyumba vyake vilikuwa vitatu kila upande, kuta zilizogawanya vyumba na baraza ilikuwa na vipimo sawa na zile kuta za lango la kwanza. Zilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
22 Jej okna, przedsionek i palmy [miały] taki sam wymiar jak brama wschodnia. Po siedmiu stopniach wchodziło się do niej, a jej przedsionek był tuż przed schodami.
Madirisha yake, baraza yake na nakshi yake ya miti ya mitende vilikuwa na vipimo sawasawa na vile vya lango linaloelekea mashariki. Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo.
23 Brama dziedzińca wewnętrznego była naprzeciwko bramy północnej, jak [brama] wschodnia; i zmierzył od bramy do bramy – sto łokci.
Kulikuwa na lango kwenye ukumbi wa ndani lililoelekea lile lango la kaskazini, kama vile ilivyokuwa ule upande wa mashariki. Akapima kutoka lango moja hadi lile lililo mkabala nalo, lilikuwa dhiraa mia moja.
24 Potem zaprowadził mnie w stronę południa, a oto była brama południowa; i zmierzył jej filary i przedsionek – [miały] te same wymiary.
Ndipo akaniongoza mpaka upande wa kusini, nami nikaona lango linaloelekea kusini. Akaipima miimo yake na baraza yake, navyo vilikuwa na vipimo sawa kama hivyo vingine.
25 [Miała] ona, podobnie jak jej przedsionek, okna wokoło, tak jak tamte okna. Miała pięćdziesiąt łokci długości i dwadzieścia pięć łokci szerokości.
Lango na baraza yake vilikuwa na madirisha membamba pande zote, kama madirisha ya huko kwingine. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
26 Prowadziło do niej siedem stopni, a jej przedsionek był przed nimi. Miała ona palmy na filarach z jednej i z drugiej strony.
Kulikuwa na ngazi saba za kupandia huko, pamoja na baraza yake mkabala nazo. Ilikuwa na nakshi za miti ya mitende kwenye kuta zilizogawanya vyumba kila upande.
27 Była też brama południowa na dziedzińcu wewnętrznym; i zmierzył od bramy do bramy w stronę południa – sto łokci.
Ukumbi wa ndani pia ulikuwa na lango lililoelekea kusini. Naye akapima kutoka lango hili mpaka kwenye lango la nje upande wa kusini; ilikuwa dhiraa mia moja.
28 Potem zaprowadził mnie na dziedziniec wewnętrzny przez bramę południową i zmierzył bramę południową: [miała] te same wymiary.
Kisha akanileta mpaka ukumbi wa ndani kwa kupitia lango la kusini, naye akapima lango la kusini, ambalo lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine.
29 A jej wnęki, jej filary i jej przedsionek [miały] te same wymiary. [Miała] ona również, jak i jej przedsionek, okna wokoło. Miała pięćdziesiąt łokci długości i dwadzieścia pięć łokci szerokości.
Vyumba vyake, kuta zilizogawanya vyumba na ukumbi wake zilikuwa na vipimo sawasawa na zile nyingine. Hilo lango na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Navyo vilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wa dhiraa ishirini na tano.
30 Dokoła był przedsionek na dwadzieścia pięć łokci długości i pięć łokci szerokości.
(Baraza za malango zilizozunguka ukumbi wa ndani zilikuwa na upana wa dhiraa ishirini na tano na kina cha dhiraa tano.)
31 A jej przedsionek [był] na dziedzińcu zewnętrznym, a na jej filarach [były] palmy. Prowadziło do niej osiem stopni.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
32 Zaprowadził mnie też na dziedziniec wewnętrzny w stronę wschodu i zmierzył bramę: m[iała] te same wymiary.
Kisha akanileta mpaka kwenye ukumbi wa ndani ulioko upande wa mashariki, naye akalipima lango hilo, lilikuwa na vipimo vilivyo sawasawa na yale mengine.
33 Jej wnęki, jej filary i jej przedsionek miały te same wymiary. Miała ona również, tak jak jej przedsionek, okna wokoło. Miała pięćdziesiąt łokci długości, dwadzieścia pięć łokci szerokości.
Vyumba vyake, kuta zake na baraza yake vilikuwa na vipimo vilivyo sawa na vile vingine. Lile lango pamoja na baraza yake vilikuwa na madirisha pande zote. Urefu wake ulikuwa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
34 A jej przedsionek był na dziedzińcu zewnętrznym, a na jej filarach były palmy po obu stronach. Prowadziło do niej osiem stopni.
Baraza yake ilielekea ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote. Kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
35 Potem zaprowadził mnie do bramy północnej i zmierzył ją: [miała] te same wymiary;
Kisha akanileta mpaka kwenye lango la kaskazini na kulipima. Lilikuwa na vipimo sawa na yale mengine,
36 Jej wnęki, jej filary i jej przedsionek, a także jej okna wokoło. Jej długość [wynosiła] pięćdziesiąt łokci, a jej szerokość – dwadzieścia pięć łokci.
kama vile ilivyokuwa kwa vyumba, kuta zake na baraza yake, tena kulikuwa na madirisha pande zote. Ilikuwa na urefu wa dhiraa hamsini na upana wake dhiraa ishirini na tano.
37 Jej filary były na dziedzińcu zewnętrznym, a na jej filarach były palmy po obu stronach. Prowadziło do niej osiem stopni.
Baraza yake ilielekeana na ukumbi wa nje, miimo yake ilinakshiwa miti ya mitende pande zote, kulikuwa na ngazi nane za kupandia huko.
38 [Były] też komory i wejście do nich przy filarach bram, tam obmywano ofiarę całopalną.
Kulikuwa na chumba na mlango karibu na baraza katika kila njia ya ndani ya lango ambamo sadaka za kuteketezwa zilioshwa.
39 W przedsionku bramy były dwa stoły po jednej stronie i dwa stoły po drugiej stronie, na których zabijano ofiarę całopalną, ofiarę za grzech i ofiarę za przewinienie.
Kwenye baraza ya lile lango kulikuwepo meza mbili kila upande, ambako sadaka za kuteketezwa, sadaka za dhambi na sadaka za hatia zilichinjiwa.
40 Na stronie zewnętrznej, przy wejściu bramy północnej, [były] dwa stoły, także i po drugiej stronie, która jest przy przedsionku bramy, [były] dwa stoły.
Karibu na ukuta wa nje wa baraza ya lile lango karibu na ngazi kwenye ingilio kuelekea kaskazini kulikuwa na meza mbili, nako upande mwingine wa ngazi kulikuwepo na meza mbili.
41 Cztery stoły z jednej i cztery stoły z drugiej strony, z boku bramy; [wszystkich] stołów, na których zabijano ofiary, było osiem.
Kwa hiyo kulikuwa na meza nne upande mmoja wa lango na nyingine nne upande mwingine, zote zilikuwa meza nane, ambapo dhabihu zilichinjiwa.
42 Te cztery stoły do całopalenia [były] z kamienia ciosanego, długie na półtora łokcia, szerokie na półtora łokcia i wysokie na jeden łokieć. Na nich kładziono sprzęt do zabijania ofiary całopalnej i [innych] ofiar.
Pia kulikuwa na meza nne za mawe yaliyochongwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, kila meza ilikuwa na urefu wa dhiraa moja na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu na kimo cha dhiraa moja. Juu ya meza hizo viliwekwa vyombo vya kuchinjia sadaka za kuteketezwa na dhabihu nyingine mbalimbali.
43 Wokoło [były] też przymocowane haki o grubości jednej dłoni, a mięso [leżało] na stołach dla ofiar.
Kulikuwa na kulabu, urefu wake nyanda nne, zilikuwa zimeshikizwa ukutani pande zote. Meza zilikuwa kwa ajili ya nyama za sadaka.
44 Na zewnątrz bramy wewnętrznej, na dziedzińcu wewnętrznym, były komory dla śpiewaków. [Jeden rząd był] z boku bramy północnej, zwrócony w kierunku południa, drugi rząd był z boku bramy wschodniej, zwrócony w kierunku północy.
Nje ya lango la ndani, kwenye ukumbi wa ndani, kulikuwa na vyumba viwili, kimoja upande wa lango la kaskazini nacho kilielekea kusini, kingine upande wa lango la kusini nacho kilielekea kaskazini.
45 I powiedział do mnie: Te komory, które są zwrócone w kierunku południa, są dla kapłanów, którzy pełnią straż w domu.
Akaniambia, “Chumba kinachoelekea upande wa kusini ni kwa ajili ya makuhani ambao wana usimamizi wa hekaluni,
46 [Te zaś] komory, które są zwrócone w kierunku północy, są dla kapłanów, którzy pełnią straż przy ołtarzu. Są to synowie Sadoka, którzy spośród synów Lewiego zbliżają się do PANA, aby mu służyć.
nacho chumba kinachoelekea upande wa kaskazini ni kwa ajili ya makuhani wenye usimamizi wa madhabahuni. Hawa ni wana wa Sadoki, ambao ndio Walawi pekee wanaoweza kumkaribia Bwana ili kuhudumu mbele zake.”
47 I zmierzył dziedziniec: długość wynosiła sto łokci, szerokość – sto łokci, był to kwadrat; a ołtarz [był] przed domem.
Ndipo alipopima ukumbi: nao ulikuwa mraba wa dhiraa mia moja urefu na upana. Madhabahu yalikuwa mbele ya Hekalu.
48 Potem wprowadził mnie do przedsionka domu i zmierzył filary przedsionka: pięć łokci z jednej i pięć łokci z drugiej strony. Szerokość bramy [wynosiła] trzy łokcie z jednej i trzy łokcie z drugiej strony.
Akanileta mpaka kwenye baraza ya Hekalu naye akaipima miimo ya hiyo baraza, nayo ilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande. Upana wa ingilio ulikuwa dhiraa kumi na nne na kuta zake zilikuwa na upana wa dhiraa tatu kila upande.
49 Długość przedsionka wynosiła dwadzieścia łokci, a szerokość – jedenaście łokci. Wstępowało się do niego po stopniach; [były] też kolumny przy filarach, jedna z jednej, druga z drugiej strony.
Baraza ilikuwa na dhiraa ishirini kwenda juu na dhiraa kumi na mbili kuanzia mbele hadi nyuma. Kulikuwa na ngazi kumi za kupandia huko, pia kulikuwa na nguzo kwa kila upande wa miimo.

< Ezechiela 40 >