< Kolosan 1 >

1 Paweł, apostoł Jezusa Chrystusa z woli Boga, i Tymoteusz, brat;
Mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Timotheo,
2 Do świętych i wiernych braci w Chrystusie Jezusie, którzy są w Kolosach. Łaska wam i pokój od Boga, naszego Ojca, i od Pana Jezusa Chrystusa.
tunawaandikia ninyi watu wa Mungu huko Kolosai, ndugu zetu waaminifu katika kuungana na Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
3 Dziękujemy Bogu i Ojcu naszego Pana Jezusa Chrystusa, nieustannie modląc się za was;
Daima tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, wakati tunapowaombea.
4 Odkąd usłyszeliśmy o waszej wierze w Chrystusa Jezusa i o miłości względem wszystkich świętych;
Maana tumesikia juu ya imani yenu katika Kristo Yesu na juu ya upendo wenu kwa watu wote wa Mungu.
5 Z powodu nadziei odłożonej dla was w niebie. O niej to przedtem słyszeliście w słowie prawdy ewangelii;
Wakati ujumbe ule wa kweli, yaani Habari Njema, ilipowafikieni kwa mara ya kwanza, mlipata kusikia juu ya lile tumaini linalopatikana kwake. Kwa sababu hiyo imani na upendo wenu vinategemea jambo lile mnalotumainia ambalo mmewekewa salama mbinguni.
6 Która dotarła do was, jak i na cały świat, i wydaje owoc, tak jak u was od dnia, w którym usłyszeliście i poznaliście łaskę Boga w prawdzie;
Habari Njema inazidi kuzaa matunda na kuenea ulimwenguni kote kama vile ilivyofanya kwenu ninyi tangu siku ile mliposikia juu ya neema ya Mungu na kuitambua ilivyo kweli.
7 Jak też nauczyliście się od naszego umiłowanego współsługi Epafrasa, który jest wiernym sługą Chrystusa dla was;
Mlijifunza juu ya neema ya Mungu kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetu, ambaye ni mfanyakazi mwaminifu wa Kristo kwa niaba yetu.
8 Który też oznajmił nam waszą miłość w Duchu.
Yeye alitupa habari za upendo wenu mliojaliwa na Roho.
9 Dlatego i my od tego dnia, w którym [to] usłyszeliśmy, nie przestajemy za was się modlić i prosić, abyście byli napełnieni poznaniem jego woli we wszelkiej mądrości i duchowym zrozumieniu;
Kwa sababu hiyo tumekuwa tukiwaombeeni daima tangu tulipopata habari zenu. Tunamwomba Mungu awajazeni ujuzi kamili wa mapenzi yake, awajazeni hekima yote na elimu iletwayo na Roho wake.
10 Abyście postępowali w sposób godny Pana, by podobać [mu] się we wszystkim, w każdym dobrym uczynku wydając owoc i wzrastając w poznawaniu Boga;
Hapo mtaweza kuishi kama anavyotaka Bwana na kutenda daima yanayompendeza. Maisha yenu yatakuwa yenye matunda ya kila namna ya matendo mema na mtazidi kukua katika kumjua Mungu.
11 Umocnieni wszelką mocą według jego chwalebnej potęgi, ku wszelkiej cierpliwości i wytrwałości z radością;
Mungu awajalieni nguvu kwa uwezo wake mtukufu ili mweze kustahimili kila kitu kwa uvumilivu.
12 Dziękując Ojcu, który nas uzdolnił do uczestnictwa w dziedzictwie świętych w światłości;
Na kwa furaha, mshukuruni Baba aliyewawezesha ninyi kuwa na sehemu yenu katika mambo yale Mungu aliyowawekea watu wake katika utawala wa mwanga.
13 Który nas wyrwał z mocy ciemności i przeniósł do królestwa swego umiłowanego Syna;
Yeye alituokoa katika nguvu ya giza, akatuleta salama katika ufalme wa Mwanae mpenzi,
14 W którym mamy odkupienie przez jego krew, przebaczenie grzechów.
ambaye kwa njia yake tunakombolewa, yaani dhambi zetu zinaondolewa.
15 On jest obrazem Boga niewidzialnego [i] pierworodnym wszelkiego stworzenia.
Kristo ni mfano wa Mungu asiyeonekana; ni mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Przez niego bowiem wszystko zostało stworzone, to, co w niebie i [to, co] na ziemi, [to, co] widzialne i [co] niewidzialne, czy trony, czy panowania, czy zwierzchności, czy władze. Wszystko przez niego i dla niego zostało stworzone.
Maana kwa njia yake vitu vyote viliumbwa duniani na mbinguni, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana: wenye enzi, watawala, wakuu na wenye mamlaka. Vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
17 On jest przed wszystkim i wszystko istnieje dzięki niemu.
Kristo alikuwako kabla ya vitu vyote; kwa kuungana naye, vyote vyadumu mahali pake.
18 On też jest głową ciała – kościoła; on jest początkiem [i] pierworodnym z umarłych, aby we wszystkim był pierwszy;
Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.
19 Ponieważ upodobał sobie [Ojciec], aby w nim zamieszkała cała pełnia;
Maana Mungu alipenda utimilifu wote uwe ndani yake.
20 I żeby przez niego pojednał wszystko ze sobą, czyniąc pokój przez krew jego krzyża; przez niego, [mówię], to, co jest na ziemi, jak i to, co jest w niebie.
Kwa njia yake Mungu alivipatanisha naye vitu vyote naam, viumbe vyote mbinguni na duniania; alileta amani kwa damu ya Kristo msalabani.
21 I was, którzy kiedyś byliście obcymi i wrogami umysłem w niegodziwych uczynkach, teraz pojednał;
Hapo kwanza ninyi pia mlikuwa mbali na Mungu na mlikuwa adui zake kwa sababu ya fikira zenu na matendo yenu maovu.
22 W jego doczesnym ciele przez śmierć, aby was przedstawić [jako] świętych, nieskalanych i nienagannych przed swoim obliczem;
Lakini sasa, kwa kifo cha Mwanae aliyeishi hapa duniani, Mungu amewapatanisha naye, kusudi awalete mbele yake mkiwa watakatifu, safi na bila lawama.
23 Jeśli tylko trwacie w wierze, ugruntowani i utwierdzeni, niedający się odwieść od nadziei ewangelii, którą usłyszeliście, a która jest głoszona wszelkiemu stworzeniu pod niebem, której ja, Paweł, stałem się sługą;
Mnapaswa, lakini kuendelea kuwa imara na thabiti katika imani hiyo, na msikubali kusukumwa mbali na tumaini lile mlilopata wakati mlipoisikia Habari Njema. Mimi Paulo nimekuwa mtumishi wa hiyo Habari Njema ambayo imekwisha hubiriwa kila kiumbe duniani.
24 Teraz raduję się w swoich cierpieniach dla was i tego, czego z udręk Chrystusa brakuje w moim ciele, dopełniam dla jego ciała, którym jest kościół.
Na sasa nafurahi kuteseka kwa ajili yenu, maana kwa mateso yangu hapa duniani, nasaidia kukamilisha kile kilichopungua bado katika mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, yaani kanisa.
25 Jego sługą stałem się zgodnie z zarządzeniem Boga, danym mi dla was, abym wypełnił słowo Boże;
Nami nimefanywa kuwa mtumishi wa kanisa kufuatana na mpango wake Mungu ambao alinikabidhi kwa faida yenu. Mpango wenyewe ni kuutangaza kwa ukamilifu ujumbe wake,
26 Tajemnicę, która była ukryta od wieków i pokoleń, ale teraz została objawiona jego świętym; (aiōn g165)
ambao ni siri aliyowaficha binadamu wote tangu milele, lakini sasa amewajulisha watu wake. (aiōn g165)
27 Którym Bóg zechciał oznajmić, jakie jest wśród pogan bogactwo chwały tej tajemnicy, którą jest Chrystus w was, nadzieja chwały.
Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
28 Jego to głosimy, napominając każdego człowieka i nauczając każdego człowieka we wszelkiej mądrości, aby każdego człowieka przedstawić doskonałym w Chrystusie Jezusie.
Kwa sababu hiyo tunamhubiri Kristo kwa watu wote; tunawaonya na kuwafundisha wote kwa hekima yote, ili tuweze kumleta kila mmoja mbele ya Mungu akiwa amekomaa katika kuungana na Kristo.
29 Nad tym też się trudzę, walcząc według jego mocy, która potężnie działa we mnie.
Kwa madhumuni hayo mimi nafanya kazi na kujitahidi nikiitumia nguvu kuu ya Kristo ifanyayo kazi ndani yangu.

< Kolosan 1 >