< Dzieje 4 >

1 A gdy mówili to do ludzi, nadeszli kapłani, dowódca straży świątynnej i saduceusze;
Petro na Yohane walipokuwa bado wanawahutubia watu, makuhani na mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na Masadukayo walifika.
2 Oburzeni, że nauczają ludzi i głoszą w Jezusie powstanie z martwych.
Walikasirika sana, maana hao mitume walikuwa wanawahubiria watu kwamba Yesu alifufuka, jambo ambalo linaonyesha wazi kwamba wafu watafufuka.
3 Schwytali ich i wtrącili do więzienia aż do następnego dnia, bo był już wieczór.
Basi, waliwatia nguvuni na kwa kuwa usiku ulikuwa umekaribia, wakawaweka chini ya ulinzi mpaka kesho yake.
4 A wielu z tych, którzy słyszeli słowo, uwierzyło. A mężczyzn było w liczbie około pięciu tysięcy.
Lakini wengi kati ya wale waliosikia ujumbe wao waliamini, na idadi ya waumini ikawa imefika karibu elfu tano.
5 Nazajutrz zebrali się w Jerozolimie ich przełożeni, starsi i uczeni w Piśmie;
Kesho yake, viongozi wa Wayahudi, wazee na walimu wa Sheria, walikusanyika pamoja huko Yerusalemu.
6 I Annasz, najwyższy kapłan, i Kajfasz, Jan, Aleksander i ilu ich było z rodu najwyższych kapłanów.
Walikutana pamoja na Anasi, Kayafa, Yohane, Aleksanda na wengine waliokuwa wa ukoo wa Kuhani Mkuu.
7 Postawili ich na środku i pytali: Jaką mocą albo w czyim imieniu to uczyniliście?
Waliwasimamisha mitume mbele yao, wakawauliza, “Ninyi mmefanya jambo hili kwa nguvu gani na kwa jina la nani?”
8 Wtedy Piotr, pełen Ducha Świętego, powiedział do nich: Przełożeni ludu i starsi Izraela;
Hapo, Petro, akiwa amejawa na Roho Mtakatifu, akawaambia, “Viongozi na wazee wa watu!
9 Jeśli my dziś mamy być przesłuchiwani z powodu dobrodziejstwa [wyświadczonego] choremu człowiekowi, dzięki czemu został on uzdrowiony;
Ikiwa mnatuuliza leo juu ya kile kitendo chema alichofanyiwa yule mtu aliyekuwa kiwete na jinsi alivyopata kuwa mzima,
10 Niech wam wszystkim i całemu ludowi Izraela będzie wiadomo, że w imieniu Jezusa Chrystusa z Nazaretu, którego wy ukrzyżowaliście, a którego Bóg wskrzesił z martwych, przez niego on stoi przed wami zdrowy.
basi, ninyi na watu wote wa Israeli mnapaswa kujua kwamba mtu huyu anasimama mbele yenu leo, mzima kabisa, kwa nguvu ya jina lake Yesu wa Nazareti ambaye ninyi mlimsulubisha, lakini Mungu akamfufua kutoka wafu.
11 On jest tym kamieniem odrzuconym przez was, budujących, który stał się kamieniem węgielnym.
Huyu ndiye ambaye Maandiko Matakatifu yanasema: Jiwe mlilokataa ninyi waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi.
12 I nie ma w nikim innym zbawienia. Nie ma bowiem pod niebem żadnego innego imienia danego ludziom, przez które moglibyśmy być zbawieni.
Wokovu haupatikani kwa mtu mwingine yeyote, kwa maana duniani pote, binadamu hawakupewa jina la mtu mwingine ambaye sisi tunaweza kuokolewa naye.”
13 Gdy zobaczyli odwagę Piotra i Jana i zrozumieli, że są ludźmi nieuczonymi i prostymi, dziwili się. Rozpoznali również, że byli z Jezusem.
Hao wazee wa baraza, wakiwa wanajua kwamba Petro na Yohane walikuwa watu wasio na kisomo wala elimu yoyote, walishangaa juu ya jinsi walivyosema kwa uhodari. Wakatambua kwamba walikuwa wamejiunga na Yesu.
14 Widząc też, że stoi z nimi uzdrowiony człowiek, nie mogli nic przeciwko [temu] powiedzieć.
Lakini walipomwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuweza kusema kitu.
15 Rozkazali im więc opuścić Radę i naradzali się między sobą.
Hivyo, waliwaamuru watoke nje ya baraza, nao wakabaki ndani wakizungumza kwa faragha.
16 Mówili: Co zrobimy z tymi ludźmi? Bo [to], że dokonali oczywistego cudu, wiadomo wszystkim mieszkańcom Jerozolimy i nie możemy temu zaprzeczyć.
Wakaulizana, “Tufanye nini na watu hawa? Kila mtu anayeishi Yerusalemu anajua kwamba mwujiza huu wa ajabu umefanyika, nasi hatuwezi kukana jambo hilo.
17 Lecz żeby się to bardziej nie rozchodziło wśród ludzi, zabrońmy im pod groźbą mówić do kogokolwiek w to imię.
Lakini ili tupate kuzuia jambo hili lisienee zaidi kati ya watu, tuwaonye wasiongee na mtu yeyote kwa jina la Yesu.”
18 A przywoławszy ich, nakazali, aby w ogóle nie mówili ani nie nauczali w imię Jezusa.
Kwa hiyo wakawaita tena ndani, wakawaonya wasiongee tena hadharani, wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19 Lecz Piotr i Jan odpowiedzieli im: Rozsądźcie, czy to sprawiedliwe w oczach Boga bardziej was słuchać niż Boga.
Lakini Petro na Yohane wakawajibu, “Amueni ninyi wenyewe kama ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumtii yeye.
20 My bowiem nie możemy nie mówić [o tym], co widzieliśmy i słyszeliśmy.
Kwa maana hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo yale tuliyoyaona na kuyasikia.”
21 A oni zagrozili [im], a nie znajdując żadnej podstawy do ich ukarania, wypuścili ich ze względu na ludzi, bo wszyscy chwalili Boga za to, co się stało.
Basi, hao wazee wa Baraza wakawaonya kwa ukali zaidi, halafu wakawaacha huru. Hawakuweza kuwapa adhabu kwa sababu watu wote walikuwa wakimtukuza Mungu kwa sababu ya tukio hilo.
22 Człowiek bowiem, na którym dokonał się cud uzdrowienia, miał ponad czterdzieści lat.
Huyo mtu aliyeponywa alikuwa na umri wa miaka zaidi ya arobaini.
23 A gdy ich wypuszczono, przyszli do swoich i opowiedzieli im wszystko, co do nich mówili naczelni kapłani i starsi.
Mara tu walipoachwa huru, Petro na Yohane walirudi kwa wenzao, wakawaeleza yale waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee.
24 A gdy oni [to] usłyszeli, jednomyślnie podnieśli swój głos do Boga i powiedzieli: Panie, ty [jesteś] Bogiem, który uczynił niebo, ziemię, morze i wszystko, co w nich jest;
Waliposikia habari hiyo waliungana pamoja katika kumwomba Mungu wakisema, “Bwana, wewe ni Muumba wa mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo!
25 Który przez usta swego sługi Dawida powiedziałeś: Dlaczego burzą się narody, a ludzie knują próżne rzeczy?
Ndiwe uliyemfanya mtumishi wako, babu yetu Daudi, aseme kwa nguvu ya Roho Mtakatifu: Kwa nini mataifa yameghadhibika? Mbona watu wamefanya mipango ya bure?
26 Królowie ziemi powstali i książęta zebrali się razem przeciw Panu i przeciw jego Chrystusowi.
Wafalme wa dunia walijiweka tayari, na watawala walikutana pamoja, ili kumwasi Bwana na Kristo wake.
27 Rzeczywiście bowiem Herod i Poncjusz Piłat z poganami i ludem Izraela zebrali się przeciwko twemu świętemu Synowi, Jezusowi, którego namaściłeś;
“Maana, kwa hakika, ndivyo Herode, Pontio Pilato, watu wa Israeli na watu wa mataifa walivyokutanika papa hapa mjini, kumpinga Yesu Mtumishi wako Mtakatifu ambaye umemtia mafuta.
28 Aby uczynić to, co twoja ręka i twój wyrok przedtem postanowiły, że ma się stać.
Naam, walikutana ili wafanye yale ambayo ulikusudia na kupanga tangu mwanzo kwa uwezo wako na mapenzi yako.
29 A teraz, Panie, spójrz na ich groźby i daj twoim sługom z całą odwagą głosić twoje słowo;
Lakini sasa, ee Bwana, angalia vitisho vyao. Utuwezeshe sisi watumishi wako kuhubiri neno lako kwa uhodari.
30 Gdy ty wyciągniesz swoją rękę, aby uzdrawiać i dokonywać znaków i cudów przez imię twego świętego Syna, Jezusa.
Nyosha mkono wako uponye watu. Fanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu Mtumishi wako Mtakatifu.”
31 A gdy oni się modlili, zatrzęsło się miejsce, na którym byli zebrani, i wszyscy zostali napełnieni Duchem Świętym, i z odwagą głosili słowo Boże.
Walipomaliza kusali, pale mahali walipokuwa wamekutanika pakatikiswa, nao wote wakajazwa Roho Mtakatifu. Wote wakaanza kuhubiri neno la Mungu bila uoga.
32 A to mnóstwo wierzących miało [jedno] serce i jedną duszę. Nikt nie nazywał swoim tego, co posiadał, ale wszystko mieli wspólne.
Jumuiya yote ya waumini ilikuwa moyo mmoja na roho moja. Hakuna hata mmoja aliyekuwa na kitu chochote akakiweka kuwa mali yake binafsi, ila waligawana vyote walivyokuwa navyo.
33 Apostołowie zaś z wielką mocą dawali świadectwo o zmartwychwstaniu Pana Jezusa i wielka łaska była nad nimi wszystkimi.
Mitume walishuhudia kwa nguvu nyingi kufufuka kwa Bwana Yesu, naye Mungu akawapa baraka nyingi.
34 Nie było też wśród nich nikogo, kto by cierpiał niedostatek, gdyż ci, którzy mieli pola albo domy, sprzedawali je i przynosili pieniądze za to, co posprzedawali;
Hakuna mtu yeyote aliyetindikiwa kitu, maana waliokuwa na mashamba au nyumba walikuwa wanaviuza
35 I kładli u stóp apostołów. Rozdzielano [to] każdemu według potrzeb.
na kuwakabidhi mitume fedha hizo, zikagawiwa kila mmoja kadiri ya mahitaji yake.
36 Także Józef, nazwany przez apostołów Barnabą – co się tłumaczy: Syn Pocieszenia – lewita rodem z Cypru;
Kulikuwa na Mlawi mmoja, mzaliwa wa Kupro, jina lake Yosefu, ambaye mitume walimwita jina Barnaba (maana yake, “Mtu mwenye kutia moyo”).
37 Sprzedał ziemię, którą posiadał, a pieniądze przyniósł i położył u stóp apostołów.
Yeye pia alikuwa na shamba lake, akaliuza; akazichukua zile fedha, akawakabidhi mitume.

< Dzieje 4 >