< Dzieje 21 >
1 Po rozstaniu z nimi odpłynęliśmy i prostym kursem przybyliśmy na Kos, a nazajutrz na Rodos, stamtąd zaś do Patary.
Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
2 Znalazłszy [tam] statek, który miał płynąć do Fenicji, wsiedliśmy [na niego] i odpłynęliśmy.
Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
3 A gdy zobaczyliśmy Cypr, zostawiliśmy go po lewej stronie, popłynęliśmy do Syrii i przybyliśmy do Tyru. Tam bowiem miano wyładować towary ze statku.
Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4 Odszukawszy uczniów, pozostaliśmy tam siedem dni, a oni pod wpływem Ducha mówili Pawłowi, żeby nie szedł do Jerozolimy.
Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5 Po upływie tych dni odeszliśmy i wyruszyliśmy w drogę, a wszyscy z żonami i dziećmi odprowadzili nas za miasto. A uklęknąwszy na wybrzeżu, modliliśmy się.
Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
6 A gdy pożegnaliśmy się ze sobą, weszliśmy na statek, a oni wrócili do domu.
Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
7 Pod koniec żeglugi z Tyru przypłynęliśmy do Ptolemaidy i powitawszy braci, spędziliśmy u nich jeden dzień.
Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8 A wyszedłszy nazajutrz, Paweł i my, jego towarzysze, dotarliśmy do Cezarei. Weszliśmy do domu Filipa ewangelisty, który był jednym z siedmiu, i zatrzymaliśmy się u niego.
Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9 A miał on cztery córki, dziewice, które prorokowały.
Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
10 Kiedy tam mieszkaliśmy przez wiele dni, przyszedł z Judei pewien prorok, imieniem Agabos.
Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
11 Przybył do nas, wziął pas Pawła, związał sobie ręce i nogi i powiedział: To mówi Duch Święty: Tak Żydzi zwiążą w Jerozolimie i wydadzą w ręce pogan człowieka, do którego należy ten pas.
Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema “Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa.”
12 Gdy to usłyszeliśmy, prosiliśmy my i miejscowi [bracia], aby nie szedł do Jerozolimy.
Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13 Wtedy Paweł odpowiedział: Co czynicie, płacząc i rozdzierając mi serce? Ja bowiem dla imienia Pana Jezusa jestem gotowy nie tylko dać się związać, ale i umrzeć w Jerozolimie.
Lakini yeye alijibu, “Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu.”
14 A gdy nie dał się przekonać, ustąpiliśmy, mówiąc: Niech się stanie wola Pana.
Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: “Mapenzi ya Bwana yafanyike”
15 Po [upływie] tych dni wzięliśmy [swoje] rzeczy i ruszyliśmy do Jerozolimy.
Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
16 Szli z nami [niektórzy] uczniowie z Cezarei, prowadząc niejakiego Mnazona Cypryjczyka, starego ucznia, u którego mieliśmy się zatrzymać.
Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
17 A gdy przybyliśmy do Jerozolimy, bracia przyjęli nas z radością.
Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18 Nazajutrz Paweł poszedł z nami do Jakuba, gdzie zebrali się wszyscy starsi.
Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
19 Powitawszy ich, opowiedział im szczegółowo, czego Bóg dokonał wśród pogan przez jego posługę.
Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
20 Gdy to usłyszeli, chwalili Pana i powiedzieli: Widzisz, bracie, ile tysięcy Żydów uwierzyło, a wszyscy gorliwie trzymają się prawa.
Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
21 Lecz o tobie słyszeli, że odwodzisz od Mojżesza wszystkich Żydów, którzy są wśród pogan, mówiąc, że nie mają obrzezywać dzieci ani żyć według [swoich] zwyczajów.
Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
22 Cóż więc czynić? Z pewnością zejdzie się lud, bo usłyszą, że przybyłeś.
Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
23 Zrób zatem to, co ci mówimy. Mamy tu czterech mężczyzn, którzy złożyli ślub.
Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24 Weź ich ze sobą, poddaj się wraz z nimi oczyszczeniu i pokryj za nich koszty, aby mogli ostrzyc głowy. Wtedy wszyscy poznają, że w tym, co o tobie słyszeli, nie ma nic [z prawdy], ale że i ty sam postępujesz [porządnie], przestrzegając prawa.
Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25 A co do pogan, którzy uwierzyli, napisaliśmy, postanawiając, aby niczego takiego nie zachowywali, tylko żeby się wystrzegali tego, co ofiarowane bożkom, i krwi, i tego, co uduszone, i nierządu.
Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 Wtedy Paweł wziął ze sobą tych mężczyzn, a następnego dnia poddał się razem z nimi oczyszczeniu i wszedł do świątyni, zgłaszając wypełnienie dni oczyszczenia, aż za każdego z nich złożona zostanie ofiara.
Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 Kiedy zaś te siedem dni dobiegało końca, zobaczyli go w świątyni Żydzi z Azji, podburzyli tłum i rzucili się na niego;
Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
28 Wołając: Mężowie Izraelici, pomóżcie! To jest człowiek, który wszędzie wszystkich naucza przeciwko ludowi i prawu, i temu miejscu, a nadto jeszcze i Greków wprowadził do świątyni i splugawił to święte miejsce.
wakipiga kelele: “Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu.”
29 Przedtem bowiem widzieli z nim w mieście Trofima z Efezu i sądzili, że Paweł wprowadził go do świątyni.
Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
30 I poruszyło się całe miasto, i zbiegł się lud. A schwytawszy Pawła, wyciągnęli go ze świątyni i natychmiast zamknięto drzwi.
Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
31 A gdy usiłowali go zabić, dano znać dowódcy oddziału, że cała Jerozolima jest wzburzona.
Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32 Natychmiast wziął żołnierzy i setników i zbiegł do nich [na dół]. A kiedy zobaczyli dowódcę i żołnierzy, przestali bić Pawła.
Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Wtedy dowódca zbliżył się, zatrzymał go, kazał związać dwoma łańcuchami i wypytywał, kim jest i co zrobił.
Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, “Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?”
34 I jedni z tłumu krzyczeli tak, a drudzy inaczej. A gdy z powodu zgiełku nie mógł dowiedzieć się niczego pewnego, rozkazał zaprowadzić go do twierdzy.
Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
35 Kiedy znalazł się na schodach, doszło do tego, że żołnierze musieli go nieść z powodu naporu tłumu.
Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
36 Wielki tłum bowiem szedł za nim, wołając: Zgładź go!
Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, “Muulie mbali!”
37 A gdy Paweł miał być wprowadzony do twierdzy, zapytał dowódcę: Czy wolno mi coś do ciebie powiedzieć? A on odpowiedział: Mówisz po grecku?
Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akamjibu, “Je unajua Kigiriki?
38 Czy nie jesteś tym Egipcjaninem, który przed tymi dniami wzniecił rozruchy i wyprowadził na pustynię cztery tysiące zabójców?
Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?”
39 A Paweł powiedział: Jestem Żydem z Tarsu, obywatelem znacznego miasta w Cylicji. Dlatego proszę cię, pozwól mi przemówić do ludu.
Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
40 Gdy pozwolił, Paweł, stojąc na schodach, dał ręką znak ludowi, a gdy nastała wielka cisza, przemówił po hebrajsku:
Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.