< Dzieje 17 >
1 A gdy przeszli Amfipolis i Apolonię, przybyli do Tesaloniki, gdzie była synagoga żydowska.
Kwa kupitia Amfipoli na Apolonia, walisafiri mpaka Thesalonika ambako kulikuwa na sunagogi la Wayahudi.
2 Wtedy Paweł według [swego] zwyczaju wszedł do nich i przez trzy szabaty rozprawiał z nimi na podstawie Pisma;
Paulo alijiunga nao kama ilivyokuwa desturi yake akajadiliana nao Sabato tatu mfululizo, akatumia Maandiko Matakatifu.
3 Wyjaśniając i nauczając, że Chrystus musiał cierpieć i powstać z martwych oraz: Ten Jezus, którego wam głoszę, jest Chrystusem.
Aliyaeleza na kuonyesha kwamba ilimbidi Kristo kuteswa na kufufuka kutoka wafu. Akawaambia, “Yesu ambaye mimi namhubiri kwenu ndiye Kristo.”
4 I niektórzy z nich uwierzyli i przyłączyli się do Pawła i Sylasa, również mnóstwo pobożnych Greków i niemało znamienitych kobiet.
Baadhi yao walikubali wakajiunga na Paulo na Sila. Kadhalika, idadi kubwa ya Wagiriki waliomcha Mungu pamoja na wanawake wengi wa tabaka la juu, walijiunga nao.
5 Ale ci Żydzi, którzy nie uwierzyli, zdjęci zazdrością, dobrali sobie niektórych niegodziwych próżniaków, a kiedy zebrali dużą grupę, podburzyli miasto. Naszli dom Jazona i szukali ich, aby wyprowadzić ich przed lud.
Lakini Wayahudi wakaona wivu; wakawakodi wafidhuli sokoni, wakafanya kikundi na kuzusha fujo mjini kote. Wakaivamia nyumba ya Yasoni wakitumaini kuwapata humo Paulo na Sila ili wawalete hadharani.
6 Gdy jednak ich nie znaleźli, zaciągnęli Jazona i niektórych braci przed przełożonych miasta, krzycząc: Oto ci, którzy cały świat wzburzyli, przyszli [też] tutaj;
Lakini hawakuwapata na hivyo walimburuta Yasoni pamoja na ndugu wengine mpaka kwa wakuu wa mji, wakapiga kelele: “Watu hawa wamekuwa wakivuruga dunia yote na sasa wako hapa mjini.
7 A Jazon ich przyjął. Oni wszyscy postępują wbrew dekretom cesarza, mówiąc, że jest inny król, Jezus.
Yasoni amewakaribisha nyumbani kwake. Wote wanafanya kinyume cha amri ya Kaisari wakisema eti Kuna mfalme mwingine aitwaye Yesu.”
8 W ten sposób zaniepokoili lud i przełożonych miasta, którzy to słyszeli.
Kwa maneno hayo waliwatia wasiwasi wakuu wa mji na kundi la watu.
9 Ale po wzięciu poręczenia od Jazona i innych wypuścili ich.
Wakawafanya Yasoni na wenzake watoe dhamana, kisha wakawaacha waende zao.
10 Zaraz w nocy bracia wysłali Pawła i Sylasa do Berei. Kiedy tam przybyli, weszli do synagogi żydowskiej.
Usiku, wale ndugu waliwahimiza Paulo na Sila waende Berea. Mara tu walipofika huko, walikwenda katika sunagogi la Wayahudi.
11 Ci byli szlachetniejsi od tych w Tesalonice, gdyż przyjęli słowo [Boże] z całą gotowością i codziennie badali Pisma, czy tak się sprawy mają.
Watu wa huko walikuwa wasikivu zaidi kuliko wale wa Thesalonika. Waliupokea ule ujumbe kwa hamu kubwa, wakawa wanayachunguza Maandiko Matakatifu kila siku, ili kuona kama yale waliyosema Paulo na Sila yalikuwa kweli.
12 Wielu więc z nich uwierzyło, również niemało wpływowych greckich kobiet i mężczyzn.
Wengi wao waliamini na pia wanawake wa Kigiriki wa tabaka la juu na wanaume pia.
13 A gdy Żydzi z Tesaloniki dowiedzieli się, że i w Berei Paweł głosi słowo Boże, przyszli też tam i podburzali lud.
Lakini, Wayahudi wa Thesalonika walipogundua kwamba Paulo alikuwa anahubiri neno la Mungu huko Berea, walikwenda huko, wakaanza kufanya fujo na kuchochea makundi ya watu.
14 Wtedy bracia natychmiast wysłali Pawła w drogę ku morzu, a Sylas i Tymoteusz tam zostali.
Wale ndugu wakamsindikiza haraka aende pwani lakini Sila na Timotheo walibaki Berea.
15 Ci, którzy towarzyszyli Pawłowi, odprowadzili go aż do Aten i powrócili, otrzymawszy polecenie dla Sylasa i Tymoteusza, żeby jak najszybciej przyszli do niego.
Wale ndugu waliomsindikiza Paulo walikwenda pamoja naye mpaka Athene. Kisha, wakarudi pamoja na maagizo kutoka kwa Paulo kwamba Sila na Timotheo wamfuate upesi iwezekanavyo.
16 A gdy Paweł czekał na nich w Atenach, burzył się w duchu na widok miasta oddanego bałwochwalstwu.
Paulo alipokuwa anawasubiri Sila na Timotheo huko Athene, moyo wake ulighadhibika sana alipoona jinsi mji huo ulivyokuwa umejaa sanamu za miungu.
17 Rozprawiał więc w synagodze z Żydami i [ludźmi] pobożnymi oraz codziennie na rynku ze wszystkimi, których spotkał.
Alijadiliana na Wayahudi na watu wengine waliomcha Mungu katika sunagogi; na kila siku alikuwa na majadiliano sokoni pamoja na wowote wale waliojitokeza.
18 Wtedy niektórzy z filozofów epikurejskich i stoickich spierali się z nim. Jedni mówili: Co chce powiedzieć ten nowinkarz? A inni: Zdaje się, że jest zwiastunem obcych bogów. Głosił im bowiem Jezusa i zmartwychwstanie.
Wengine waliofuata falsafa ya Epikuro na Stoiki walibishana naye. Wengine walisema, “Anataka kusema nini huyu bwanamaneno?” Kwa kuwa Paulo alikuwa anahubiri juu ya Yesu na juu ya ufufuo, wengine walisema, “Inaonekana kama anahubiri juu ya miungu ya kigeni.”
19 Zabrali go, zaprowadzili na Areopag i zapytali: Czy możemy się dowiedzieć, co to za nowa nauka, którą głosisz?
Hivyo walimchukua Paulo, wakampeleka Areopago, wakasema, “Tunataka kujua jambo hili jipya ulilokuwa unazungumzia.
20 Bo przynosisz jakieś rzeczy obce naszym uszom. Chcemy więc wiedzieć, o co właściwie chodzi.
Vitu vingine tulivyosikia kwa masikio yetu vinaonekana kuwa viroja kwetu. Tungependa kujua mambo haya yana maana gani.”
21 (A wszyscy Ateńczycy i mieszkający tam cudzoziemcy nie poświęcali czasu na nic innego, tylko na opowiadanie lub słuchanie czegoś nowego).
Wananchi wa Athene na wakazi wengine wa huko walikuwa wanatumia wakati wao wote kuhadithiana na kusikiliza habari mpyampya.
22 Wtedy Paweł stanął pośrodku Areopagu i powiedział: Mężowie ateńscy, widzę, że pod każdym względem jesteście nadzwyczaj religijni.
Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, “Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba ninyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana.
23 Przechadzając się bowiem i przypatrując waszym świętościom, znalazłem też ołtarz, na którym było napisane: Nieznanemu Bogu. Ja głoszę wam tego, którego nie znając, czcicie.
Sababu yenyewe ni kwamba katika pitapita yangu niliangalia sanamu zenu za ibada nikakuta madhabahu moja ambayo imeandikwa: Kwa ajili ya Mungu yule Asiyejulikana. Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu.
24 Bóg, który stworzył świat i wszystko na nim, ten, który jest Panem nieba i ziemi, nie mieszka w świątyniach zbudowanych ręką.
Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na nchi; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu.
25 Ani nie jest czczony rękoma ludzkimi tak, [jakby] czegoś potrzebował, ponieważ sam daje wszystkim życie i oddech, i wszystko.
Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu.
26 I z jednej krwi uczynił wszystkie narody ludzkie, żeby mieszkały na całej powierzchni ziemi, określiwszy czasy wcześniej wyznaczone i zamierzone granice ich zamieszkania;
Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi.
27 Żeby szukali Pana, czy go nie znajdą po omacku, chociaż nie jest daleko od nikogo z nas.
Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu.
28 Bo w nim żyjemy, poruszamy się i jesteśmy, jak też powiedzieli niektórzy z waszych poetów: I [my] bowiem jesteśmy z jego rodu.
Kama alivyosema mtu mmoja: Ndani yake yeye sisi tunaishi, tunajimudu, na tuko! Ni kama washairi wenu wengine walivyosema: Sisi ni watoto wake.
29 Będąc więc z rodu Boga, nie powinniśmy sądzić, że Bóstwo jest podobne do złota, srebra lub kamienia, misternie wyrzeźbionych według wyobrażenia ludzkiego.
Ikiwa basi, sisi ni watoto wa Mungu, haifai kumfikiria Mungu kuwa kama dhahabu, fedha au hata jiwe lililochongwa na kutiwa nakshi na binadamu.
30 Bóg wprawdzie pomijał czasy tej nieświadomości, teraz [jednak] nakazuje wszędzie wszystkim ludziom pokutować;
Mungu alifanya kama kwamba haoni nyakati zile watu walipokuwa wajinga. Lakini sasa, anaamuru watu wote kila mahali watubu.
31 Gdyż wyznaczył dzień, w którym będzie sprawiedliwie sądził cały świat przez człowieka, którego [do tego] przeznaczył, zapewniając o tym wszystkich przez wskrzeszenie go z martwych.
Kwa maana amekwisha weka siku ambayo atauhukumu ulimwengu kwa haki kwa njia ya mtu mmoja aliyemteua. Mungu amewathibitishia wote jambo hili kwa kumfufua mtu huyo kutoka wafu!”
32 Gdy usłyszeli o zmartwychwstaniu, jedni się naśmiewali, a inni mówili: Posłuchamy cię o tym ponownie.
Walipomsikia Paulo anasema juu ya jambo la kufufuka kwa wafu, wengine wao waliangua kicheko; lakini wengine walisema, “Tunataka kukusikia tena juu ya jambo hili!”
33 I tak Paweł wyszedł spośród nich.
Hivyo, Paulo aliwaacha, akatoka barazani.
34 Lecz niektórzy ludzie przyłączyli się do niego i uwierzyli. [Był] też wśród nich Dionizy Areopagita i kobieta imieniem Damaris oraz inni z nimi.
Lakini watu kadhaa waliandamana naye, wakawa waumini. Miongoni mwao walikuwa Dionisio wa Areopago, mwanamke mmoja aitwaye Damari na wengineo.