< II Tesaloniczan 3 >

1 Na koniec, bracia, módlcie się za nas, aby słowo Pana szerzyło się i rozsławiało jak i u was;
Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
2 I abyśmy byli wybawieni od przewrotnych i złych ludzi; nie wszyscy bowiem mają wiarę.
Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
3 Lecz wierny jest Pan, który was utwierdzi i będzie strzec od złego.
Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
4 Co do was, mamy ufność w Panu, że to, co nakazujemy, czynicie i będziecie czynić.
Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
5 Pan zaś niech skieruje wasze serca ku miłości Bożej i ku cierpliwemu oczekiwaniu Chrystusa.
Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
6 A nakazujemy wam, bracia, w imię naszego Pana Jezusa Chrystusa, abyście stronili od każdego brata, który postępuje nieporządnie, a nie według przekazanych nauk, które otrzymał od nas.
Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
7 Sami bowiem wiecie, jak należy nas naśladować, ponieważ nie żyliśmy wśród was nieporządnie;
Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
8 Ani u nikogo nie jedliśmy chleba za darmo, ale pracowaliśmy w trudzie i zmęczeniu we dnie i w nocy, aby dla nikogo z was nie być ciężarem.
wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
9 Nie jakobyśmy nie mieli do [tego] prawa, lecz żeby dać wam samych siebie za przykład do naśladowania.
Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
10 Gdy bowiem byliśmy u was, to nakazaliśmy wam: Kto nie chce pracować, niech [też] nie je.
Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
11 Bo słyszymy, że niektórzy wśród was postępują nieporządnie, wcale nie pracują, lecz zajmują się niepotrzebnymi rzeczami.
Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
12 Dlatego nakazujemy [im] i napominamy przez naszego Pana Jezusa Chrystusa, aby spokojnie pracując, własny chleb jedli.
Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
13 Wy zaś, bracia, nie bądźcie znużeni w czynieniu dobra.
Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
14 Jeśli ktoś nie posłucha naszych słów [zawartych] w [tym] liście, to zwróćcie na niego uwagę i nie przestawajcie z nim, aby się zawstydził.
Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
15 Nie uważajcie [go] jednak za nieprzyjaciela, lecz napominajcie jak brata.
Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16 A sam Pan pokoju niech was obdarza pokojem zawsze [i] na wszelki sposób. Pan [niech będzie] z wami wszystkimi.
Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
17 Pozdrowienie moją, Pawła, ręką; jest ono znakiem w każdym liście; tak piszę.
Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
18 Łaska naszego Pana Jezusa Chrystusa [niech będzie] z wami wszystkimi. Amen.
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.

< II Tesaloniczan 3 >