< II Samuela 20 >
1 I znalazł się tam przypadkiem człowiek Beliala imieniem Szeba, syn Bikriego, Beniaminita. Ten zadął w trąbę i powiedział: Nie mamy działu w Dawidzie ani nie mamy dziedzictwa w synu Jessego. Każdy do swojego namiotu, o Izraelu!
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 Odstąpili więc od Dawida wszyscy ludzie Izraela [i poszli] za Szebą, synem Bikriego. Ale ludzie Judy, od Jordanu aż do Jerozolimy, trzymali się swego króla.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 I Dawid przyszedł do swego domu w Jerozolimie. Wtedy król wziął dziesięć kobiet, nałożnic, które pozostawił, aby strzegły domu, umieścił je w strzeżonym domu i utrzymywał, ale nie obcował z nimi. Pozostały one zamknięte aż do dnia swej śmierci, jakby we wdowieństwie.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 Potem król powiedział do Amasy: Zbierz mi mężczyzn Judy w ciągu trzech dni, ty także się staw.
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 Poszedł więc Amasa, by zebrać lud Judy. Lecz przekroczył termin, który mu wyznaczył.
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 I Dawid powiedział do Abiszaja: Teraz Szeba, syn Bikriego, uczyni nam gorzej niż Absalom. Weź [więc] sługi twego pana i ścigaj go, by nie znalazł sobie obronnych miast i nie wymknął się nam.
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 Wtedy wyszli z nim ludzie Joaba oraz Keretyci, Peletyci i wszyscy dzielni wojownicy. Wyruszyli z Jerozolimy w pościg za Szebą, synem Bikriego.
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 A gdy byli przy wielkim kamieniu, który [jest] w Gibeonie, Amasa wyszedł im naprzeciw. A Joab miał na sobie przepasaną szatę, a na niej pas z mieczem w pochwie przypasany do bioder. Gdy on się zbliżał, [miecz] wypadł mu.
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 I Joab zapytał Amasę: Czy masz się dobrze, mój bracie? I Joab ujął Amasę prawą ręką za brodę, jakby miał go pocałować.
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 Lecz Amasa nie zwrócił uwagi na miecz, który [był] w ręce Joaba. Ten uderzył go nim pod piąte żebro i wylał jego wnętrzności na ziemię bez [zadawania] drugiego ciosu, i [Amasa] umarł. A Joab i jego brat Abiszaj puścili się w pogoń za Szebą, synem Bikriego.
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 Wtedy stanął przy nim jeden ze sług Joaba i powiedział: Ktokolwiek sprzyja Joabowi i ktokolwiek [jest] za Dawidem, niech idzie za Joabem.
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 Tymczasem Amasa tarzał się we krwi na środku drogi. A gdy ten człowiek zobaczył, że cały lud zatrzymuje się, usunął Amasę z drogi na pole i zarzucił na niego szatę. Zauważył bowiem, że każdy, kto obok niego przechodzi, zatrzymuje się.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 A gdy usunięto go z drogi, wszyscy szli za Joabem, by ścigać Szebę, syna Bikriego.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 Ten przeszedł przez wszystkie pokolenia Izraela aż do Abel i Bet-Maaka, a wszyscy Berici zebrali się i poszli za nim.
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 A kiedy tam nadciągnęli, oblegli go w Abel Bet-Maaka i usypali wał przeciw miastu, tak że stali przed murem, i cały lud, który był z Joabem, uderzał, by zburzyć mur.
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 Wtedy [pewna] mądra kobieta zawołała z miasta: Słuchajcie, słuchajcie! Powiedzcie, proszę, do Joaba: Zbliż się tutaj, a porozmawiam z tobą.
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 Gdy zbliżył się do niej, kobieta zapytała: Czy ty jesteś Joab? Odpowiedział: Jestem. Wtedy powiedziała: Słuchaj słów twojej służącej. Odpowiedział: Słucham.
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 Ona mówiła dalej: W dawnych czasach mówiono: Koniecznie należy radzić się w Abelu – i tak sprawa się zakończyła.
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 Ja jestem [jednym] ze spokojnych i wiernych w Izraelu, a ty chcesz zniszczyć miasto i matkę w Izraelu. Dlaczego chcesz zburzyć dziedzictwo PANA?
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 Joab odpowiedział jej: Nie daj, nie daj Boże, abym miał zburzyć albo zniszczyć.
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 Nie tak ma się sprawa. Tylko pewien człowiek z góry Efraim imieniem Szeba, syn Bikriego, podniósł rękę przeciw królowi Dawidowi. Wydajcie jego samego, a odstąpię od miasta. Kobieta odpowiedziała Joabowi: Oto jego głowa zostanie ci rzucona przez mur.
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 Kobieta poszła więc do całego ludu w swojej mądrości. Ścięto głowę Szebie, synowi Bikriego, i rzucono ją do Joaba. Ten zaś zadął w trąbę i [wszyscy] rozeszli się spod miasta, każdy do swojego namiotu. A Joab wrócił do króla do Jerozolimy.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 I Joab był dowódcą całego wojska Izraela. A Benajasz, syn Jehojady, [dowódcą] Keretytów i Peletytów.
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 Adoram był poborcą daniny, a Jehoszafat, syn Ahiluda, kronikarzem.
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 Szewa – pisarzem, a Sadok i Abiatar [byli] kapłanami.
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 Również Ira Jairyta był naczelnym dostojnikiem u Dawida.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.