< II Królewska 23 >

1 Wtedy król posłał, aby zebrali się wokół niego wszyscy starsi Judy i Jerozolimy.
Hivyo mfalme akawatuma wajumbe waliokuwa wamemzunguka wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
2 Następnie król udał się do domu PANA, a wraz z nim wszyscy mężczyźni Judy, wszyscy mieszkańcy Jerozolimy, kapłani, prorocy oraz cały lud – od najmniejszych do największych. I czytał do ich uszu wszystkie słowa księgi przymierza, którą znaleziono w domu PANA.
Kisha mfalme akapanda hadi kwenye nyumba ya Yahwe, na watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na makuhani, manabii, na watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Kisha akasoma katika masikioni kwao maneno yote ya kitabu cha agano ambalo lililokuwa limepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
3 Potem król stanął przy kolumnie i zawarł przymierze przed PANEM, że będą szli za PANEM i będą przestrzegać jego przykazań, świadectw i nakazów z całego serca i całą duszą i wypełniać słowa przymierza, które zostały napisane w tej księdze. I cały lud przystąpił do przymierza.
Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yahwe, kutembea pamoja na Yahwe na kukumbuka maagizo yake, kanuni zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kuthibitisha maneno ya hili agano ambalo lililokuwa limeandikwa kwenye hiki kitabu. Hivyo watu wote wakakubaliana kusimama kwenye agano
4 Wtedy król nakazał najwyższemu kapłanowi Chilkiaszowi, kapłanom drugiego rzędu i stróżom progu wynieść ze świątyni PANA wszystkie przedmioty wykonane dla Baala, do gaju i dla całego zastępu niebieskiego. I spalił je poza Jerozolimą na polu Cedronu, i zaniósł ich popiół do Betel.
Mfalme akamwamuru Hilkia yule kuhani mkuu, makuhani chini yake, na walinzi wa lango watoe kwenye hekalu vyombo vilivyokuwa vimetengenezwa kwa ajili ya Baali na Ashera, na kwa ajili ya nyota zote za mbinguni. Akivichoma moto Yerusalimu kwenye mashamba ya bonde la Kidroni na kubeba majivu yake kwenda Betheli.
5 Zwolnił też [z urzędu] bałwochwalczych kapłanów, których ustanowili królowie Judy, aby palili kadzidło na wyżynach w miastach Judy i w okolicach Jerozolimy, oraz tych, którzy palili kadzidło Baalowi, słońcu, księżycowi, planetom i całemu zastępowi niebieskiemu.
Akawaondoa makuhani waliokuwa wanaabudu miungu ambao wafalme wa Yuda waliwachagua ili kwa ajili ya kufukiza ubani katika mahali pa juu kwenye miji ya Yuda na sehemu zinazoizunguka Yerusalemu-wale waliokuwa wanchoma ubani kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote za mbinguni.
6 Wyniósł gaj z domu PANA poza Jerozolimę, do potoku Cedron, i spalił go przy potoku Cedron, starł go na proch i rozrzucił na grobach synów ludu.
Akaiondoa Ashera kutoka kwenye hekalu la Yahwe, nje ya Yerusalemu hata bonde la Kidroni na kuichoma hapo. Akaipiga kwenye mavumbi na kuiyatupa yale mavumbi kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
7 Zburzył też domy Sodomitów, które znajdowały się przy domu PANA, gdzie kobiety tkały zasłony do gaju.
Akavisafisha vyumba vya makahaba ambao walikuwa kwenye hekalu la Yahwe, ambako wanawake waliposhonea nguo kwa ajili ya Ashera
8 I zwołał wszystkich kapłanów z miast Judy, i splugawił wyżyny, na których kapłani palili kadzidło, od Geba aż do Beer-Szeby, i zburzył wyżyny przy bramach [znajdujących się] u wejścia bramy Jozuego, namiestnika miasta, po lewej stronie, gdy się wchodzi przez bramę miejską.
Yosia akawaleta makuhani wote nje ya miji ya Yuda na kupanajisi mahali pa juu ambako makuhani walipokuwa wakichomea ubani, kutoka Geba hata Bersheba. Akapaharibu mahala pa juu kwenye malango ambayo yaliyokuwa ya kuingilia kwenda kwenye lango la Yoshua (liwali wa mji), upande wa kushoto wa lango la mji.
9 Jednakże kapłani wyżyn nie przystąpili do ołtarza PANA w Jerozolimie, ale mogli jeść przaśne chleby wśród swoich braci.
Ingawa makuhani wa mahali pa juu hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye madhabahu ya Yahwe katika Yerusalemu, wakala mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
10 Splugawił również Tofet, które było w dolinie syna Hinnom, aby nikt więcej nie przeprowadził swego syna ani córki przez ogień [ku czci] Molocha.
Yosia akainajisi Tofethi, ambayo ipo kwenye bonde la Ben Hinomu, ili kwamba mtu yeyote asimuweke mtoto wake wa kiume au binti yake kwenye moto kama sadaka kwa Molaki.
11 Usunął też konie, które królowie Judy poświęcili słońcu u wejścia do domu PANA, obok komnaty dworzanina Natanmeleka, która była na przedmieściu, a rydwany słońca spalił ogniem.
Akawachukua farasi ambao wafalme wa Yuda waliokuwa wametolewa kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye eneo la lango la uingilia kwenye hekalu la Yahwe, karibu na chumba cha Nathani Meleki, msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme. Yosia akayachoma yale magari ya farasi ya jua
12 Król zburzył także ołtarze, które znajdowały się na dachu górnej komnaty Achaza, zbudowane przez królów Judy, oraz ołtarze, które uczynił Manasses w obu dziedzińcach domu PANA. Usunął je stamtąd i wrzucił ich proch do potoku Cedron.
Yosia mfalme akayaharibu madhabahu yaliyokuwa kwenye dari ya juu ya chumba cha Ahazi, ambacho wafalme wa Yuda walikitengeneza, na madhabahu ambayo Manase aliyatengeneza kwenye behewa mbili za nyumba ya Yahwe. Yosia akazivunga vipande vipande na kuvitupa kwenye bonde la Kidroni.
13 Król splugawił wyżyny, które stały przed Jerozolimą po prawej stronie Góry Zatracenia i które zbudował Salomon, król Izraela, dla Asztarty, obrzydliwości Sydończyków, dla Kemosza, obrzydliwości Moabitów, i dla Milkoma, obrzydliwości synów Ammona.
Mfalme akapaangamiza mahali pa juu magharibi mwa Yerusalemu, kusini mwa mlima wa uharibifu ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alipajenga kwa ajili ya Ashtorithi, chukizo la Wamoabu; sanamu za karaha za Wasidoni; kwa Kemoshi, sanamu za karaha wa Moabu; na kwa Moleki, sanamu wa karaha wa watu wa Amoni.
14 I pokruszył posągi, powycinał gaje, a ich miejsca napełnił kośćmi ludzkimi.
Akazivunja nguzo za jiwe kuwa vipande vipande na kuziangusha chini nguzo za Ashera na kuzijaza zile sehemu kwa mifupa ya watu.
15 Ponadto ołtarz, który był w Betel, [i] wyżynę uczynioną przez Jeroboama, syna Nebata, który przywiódł Izraela do grzechu – także ten ołtarz i wyżynę zburzył. Spalił wyżynę, starł na proch i spalił gaj.
Yosia pia akaiteketeza kabisa madhabahu iliyokuwa Betheli na mahali pa juu ambako Yeroboamu mwana wa Nebati (ambaye aliwafanya Waisraeli kuasi) aliijenga. Pia aliichoma moto ile madhabahu na mahali pa juu na kupapiga hadi pakawa vumbi. Pia akaichoma moto nguzo ya Ashera.
16 A gdy Jozjasz odwrócił się, zobaczył groby, które były tam na górze. Posłał i zabrał kości z tych grobów, i spalił je na ołtarzu, plugawiąc go zgodnie ze słowem PANA wygłoszonym przez męża Bożego, który wypowiedział te rzeczy.
Yosia alipotazama kwenye lile eneo, akagundua kwamba yale makaburi yalikuwa juu ya mlima. Akawatuma watu kuichukua mifupa kutoka kwenye yale makaburi; kisha akaichoma kwenye madhabahu, akainajisi. Hii ilitokana na neno la Yahwe ambalo mtu wa Mungu aliliongea, yule mtu aliyekuwa ameongea haya mambo kabla.
17 I zapytał: Co to za napis, który widzę? Ludzie z tego miasta odpowiedzieli: To grób męża Bożego, który przyszedł z Judy i zapowiedział rzeczy, które wykonałeś nad ołtarzem w Betel.
Kisha akasema, “Ni ukumbusho wa nani ule ninao uona?” Mtu wa ule mji akamwambia, “Lile ni kaburi la mtu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kuongea kuhusu haya mambo ambayo ameyafanya dhidi ya madhabahu ya Betheli.”
18 Wtedy powiedział: Zostawcie go, niech nikt nie rusza jego kości. Pozostawiono więc jego kości wraz z kośćmi proroka, który przybył z Samarii.
Hivyo Yosia akasema, “Mwacheni. Mtu asihamishe mifupa yake.” Hivyo wakaacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii ambaye alikuja kutoka Samaria.
19 Jozjasz usunął też wszystkie świątynie na wyżynach, które były w miastach Samarii zbudowanych przez królów Izraela, aby drażnić [PANA]. Postąpił z nimi tak samo, jak uczynił w Betel.
Kisha Yosia akahamisha nyumba zote za mahali pa juu ambazo zilikuwa katika mji wa Samaria, ambazo wafalme wa Israeli walizokuwa wamezitengeneza, na ambazo zilizokuwa zimemgadhabisha Yahwe kwa hasira.
20 Pozabijał także wszystkich kapłanów wyżyn, którzy tam [byli] przy ołtarzach, i spalił na nich ludzkie kości. Potem wrócił do Jerozolimy.
Aliwafanyia kile ambacho kilikuwa kimefanyika katika Betheli. Aliwachinja makuhani wote wa mahali pa juu ya madhabahu na aliichoma mifupa ya watu juu yao. Kisha akarudi Yerusalemu.
21 I król nakazał całemu ludowi: Obchodźcie święto Paschy dla PANA, waszego Boga, tak jak jest napisane w księdze tego przymierza.
Kisha mfalme akawaamuru watu wote, akisema, “Itunzeni Pasaka ya Yahwe Mungu wenu, kama ilivyoandikwa kwenye hiki kitabu cha agano.”
22 Takiej Paschy nie obchodzono od czasów sędziów, którzy sądzili Izraela, i przez wszystkie dni królów Izraela i królów Judy.
Hiyo Pasaka haijawahi kufanyika tangu siku za waamuzi ambao waliiongoza Israeli, wala katika siku zote za wafalme wa Israeli au Yuda.
23 Dopiero w osiemnastym roku króla Jozjasza obchodzono taką Paschę dla PANA w Jerozolimie.
Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia hii Pasaka ya Yahwe ilisheherekewa katika Yerusalemu.
24 Jozjasz usunął również czarowników, wróżbiarzy, posągi, bożki i wszystkie obrzydliwości, które widziano w ziemi Judy i w Jerozolimie, aby wypełnić słowa prawa napisane w księdze, którą znalazł kapłan Chilkiasz w domu PANA.
Yosia pia akawafukuza wale ambao waliokuwa wameongea na wafu au na roho. Pia aliifukuza miungu ya sananmu, sanamu, na vitu vyote ambavyo ni chukizo vilivyokuwa vinaonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, hivyo kwa kuthibitisha yale maneno ya sheria ambayo iliyokuwa imeandikwa kwenye kitabu cha Hilkia yule kuhani aliyekuwa amepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
25 I nie było przed nim króla podobnego do niego, który by wrócił do PANA z całego swego serca, całą swoją duszą i z całej swojej siły, według całego Prawa Mojżesza, i po nim nie powstał nikt jemu podobny.
Kabla ya Yosia, hapakuwa na mfalme kama yeye, aliyekuwa amemwelekea yahwe kwa moyo wake wote, roho yake yote, na nguvu zake zote, ambaye alifuata sheria zote za Musa. Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye.
26 PAN jednak nie odwrócił się od zapalczywości swego wielkiego gniewu, którym zapłonął przeciwko Judzie z powodu wszelkich zniewag, którymi rozdrażnił go Manasses.
Walakini, Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya Yuda kwa waabudu wapagani wote pamoja ambao Manase aliokuwa amemgadhibisha.
27 PAN więc powiedział: Również Judę odrzucę sprzed swojego oblicza, jak odrzuciłem Izraela, i wzgardzę tym miastem, które wybrałem, Jerozolimą, i domem tym, o którym powiedziałem: Tam będzie moje imię.
Hivyo Yahwe akasema, “Pia nitaiondoa Yuda usoni kwangu, kama nilivyoiondoa Israeli, na nitautupilia mbali huu mji ambao nilio uchagua, Yerusalemu, na ile nyumba ambayo niliyokuwa nimesema, 'Jina langu litakuwa humo.”'
28 A pozostałe dzieje Jozjasza i wszystko, co czynił, czy nie są zapisane w księdze kronik królów Judy?
Kama kwa mambo mengine yanayo muhusu Yosia, kila kitu alichofanya, je vimeandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
29 Za jego dni faraon Necho, król Egiptu, wyruszył przeciwko królowi Asyrii nad rzekę Eufrat. Król Jozjasz wyruszył przeciwko niemu, a gdy ten go zobaczył, zabił go w Megiddo.
Katika siku zake, Farao Neko, mfalme wa Misri, alienda kupigana dhidi ya mfalme wa Ashuru huko mto Frati. Mfalme Yosia akaenda kuonana na Neco katika mapigano, na Neko akamuua huko Megido.
30 I jego słudzy przewieźli go zmarłego z Megiddo, sprowadzili go do Jerozolimy i pogrzebali w jego grobie. Potem lud tej ziemi wziął Jehoachaza, syna Jozjasza, namaścił go i ustanowił go królem w miejsce jego ojca.
Watumishi wa Yosia wakambeba kwenye gari la farasi akiwa amekufa kutoka Migido, kumleta Yerusalemu, na kumzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, na kumfanya kuwa mfalme katika mahali pake.
31 Jehoachaz miał dwadzieścia trzy lata, kiedy zaczął królować, i królował trzy miesiące w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Chamutal [i była] córką Jeremiasza z Libny.
Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na tatu alipoanza kutawala, na alitawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia wa Libana.
32 Czynił on to, co złe w oczach PANA, zupełnie tak, jak czynili jego ojcowie.
Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama kila kitu ambacho babu zake walichokifanya.
33 Faraon Necho uwięził go w Ribla w ziemi Chamat, aby nie królował w Jerozolimie, i nałożył na ziemię daninę w wysokości stu talentów srebra i jednego talentu złota.
Farao Neko akamfunga gerezani huko Ribla katika nchi ya Hamathi, hivyo asiweze kutawala katika Yerusalemu. Kisha Neko akaitoza Yuda talanta mia moja za fedha na talanta moja ya dhahabu.
34 Faraon Necho ustanowił królem Eliakima, syna Jozjasza, w miejsce jego ojca Jozjasza, i zmienił jego imię na Joakim, a Jehoachaza zabrał. Ten przyszedł do Egiptu i tam umarł.
Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia mfalme katika mahali pa Yosia baba yake, na kubadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua mfalme Yehoahazi kwenda Misri, na Yehoahazi akafia huko.
35 A Joakim dał faraonowi srebro i złoto, ale opodatkował ziemię, aby mógł oddać pieniądze według rozkazu faraona. Pobierał srebro i złoto od ludu ziemi, od każdego według oszacowania, aby je oddać faraonowi Necho.
Yehoyakimu akalipa fedha na dhahabu kwa Farao. Ili akutane na amri ya Farao, Yehoyakimu akaitoza nchi na kulazimisha kila mtu miongoni mwa watu wa nchi wamlipe fedha na dhahabu kulingana na makadirio yao.
36 Joakim miał dwadzieścia pięć lat, kiedy zaczął królować, i królował jedenaście lat w Jerozolimie. Jego matka miała na imię Zebidda [i była] córką Pedajasza z Rumy.
Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, na alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Zebida; alikuwa binti wa Pedaia wa Ruma.
37 Czynił on to, co złe w oczach PANA, zupełnie tak, jak czynili jego ojcowie.
Yehoyakimu akafanya yale yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama waliyoyafanya babu zake.

< II Królewska 23 >