< I Królewska 1 >

1 Gdy król Dawid zestarzał się [i] posunął w latach, to choć okrywano go szatami, nie mógł się rozgrzać.
Mfalme Daudi alipokuwa mzee umri ukiwa umesogea, hakuweza kupata joto hata walipomfunika kwa nguo.
2 Jego słudzy powiedzieli mu więc: Niech poszukają dla naszego pana, króla, młodej dziewicy, która stawałaby przed królem i pielęgnowała go. Niech kładzie się na twoim łonie, żeby nasz pan, król, mógł się rozgrzać.
Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, “Turuhusu tumtafute kijana mwanamwali bikira amhudumie mfalme na kumtunza. Anaweza kulala pembeni mwake ili bwana wetu mfalme apate joto.”
3 Szukali więc pięknej dziewczyny po wszystkich obszarach Izraela i znaleźli Abiszag Szunamitkę, i przyprowadzili ją do króla.
Kisha wakatafuta katika Israeli yote ili kumpata msichana mzuri wa sura na wakampata Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
4 Dziewczyna ta [była] bardzo piękna; pielęgnowała króla i służyła mu, ale król z nią nie obcował.
Msichana huyo alikuwa mzuri sana wa sura, akamtunza mfalme na kumhudumia, lakini mfalme hakufanya naye tendo la ndoa.
5 Lecz Adoniasz, syn Chaggity, wywyższał się, mówiąc: Ja zostanę królem. Zaopatrzył się w rydwany i jeźdźców oraz pięćdziesięciu mężczyzn, którzy biegali przed nim.
Basi Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi, akajigamba na kusema, “Mimi nitakuwa mfalme.” Hivyo akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, pamoja na watu hamsini wa kumtangulia wakikimbia.
6 Jego ojciec nigdy go nie upominał, mówiąc: Czemu to uczyniłeś? Był on też bardzo przystojny, [jego matka] urodziła go po Absalomie.
(Baba yake hakuwa ameingilia na kumuuliza, “Kwa nini unafanya hivyo?” Alikuwa pia kijana mzuri sana wa sura, na alizaliwa baada ya Absalomu.)
7 Porozumiał się z Joabem, synem Serui, i z kapłanem Abiatarem, a oni przystali z Adoniaszem i pomogli [mu].
Adoniya akashauriana pamoja na Yoabu mwana wa Seruya na kuhani Abiathari, nao wakamsaidia.
8 Lecz kapłan Sadok, Benajasz, syn Jehojady, prorok Natan, Szimei, Rei oraz dzielni wojownicy Dawida nie sprzyjali Adoniaszowi.
Lakini kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, Nathani nabii, Shimei, Rei na walinzi maalum wa Daudi hawakujiunga na Adoniya.
9 Potem Adoniasz zabił owce, woły i tuczne bydło przy kamieniu Zochelet, blisko źródła Rogel, i zaprosił wszystkich swych braci, synów króla, oraz wszystkich mężczyzn Judy, sługi króla.
Ndipo Adoniya akatoa dhabihu ya kondoo, ngʼombe na ndama walionona kwenye Jiwe la Zohelethi karibu na En-Rogeli. Akawaalika ndugu zake wote, wana wa mfalme na wanaume wote wa Yuda waliokuwa maafisa wa mfalme,
10 Lecz nie zaprosił proroka Natana, Benajasza i dzielnych wojowników oraz swego brata Salomona.
lakini hakumwalika nabii Nathani, Benaya, walinzi maalum wa mfalme, wala ndugu yake Solomoni.
11 Wtedy Natan zapytał Batszebę, matkę Salomona: Czy nie słyszałaś, że Adoniasz, syn Chaggity, króluje, a nasz pan, Dawid, [o tym] nie wie?
Ndipo Nathani akamuuliza Bathsheba, mama yake Solomoni, “Je, hujasikia kwamba Adoniya, mwana wa Hagithi, amekuwa mfalme pasipo bwana wetu Daudi kujua jambo hili?
12 Chodź więc teraz, proszę, dam ci radę, abyś ocaliła swoje życie i życie swego syna, Salomona.
Sasa basi, acha nikushauri jinsi utakavyookoa uhai wako mwenyewe na uhai wa mwanao Solomoni.
13 Idź i wejdź do króla Dawida, i powiedz mu: Czyż ty, mój panie, królu, nie przysiągłeś swojej służącej: Twój syn Salomon będzie królował po mnie i on zasiądzie na moim tronie? Dlaczego więc króluje Adoniasz?
Ingia kwa Mfalme Daudi na umwambie, ‘Bwana wangu mfalme, je hukuniapia mimi mtumishi wako: “Hakika mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi juu ya kiti changu cha ufalme”? Kwa nini basi Adoniya amekuwa mfalme?’
14 A oto gdy ty będziesz tam jeszcze rozmawiała z królem, ja wejdę za tobą i potwierdzę twoje słowa.
Utakapokuwa ukizungumza na mfalme, nitaingia na kuthibitisha hayo uliyoyasema.”
15 Batszeba weszła więc do króla do komnaty. Król już się bardzo zestarzał, a Abiszag Szunamitka usługiwała królowi.
Hivyo Bathsheba akaenda kumwona mfalme chumbani mwake mahali ambapo Abishagi, Mshunami, alikuwa akimhudumia, naye mfalme alikuwa mzee sana.
16 Wtedy Batszeba uklękła i oddała pokłon królowi, a król zapytał: Czego chcesz?
Bathsheba akasujudu na kupiga magoti mbele ya mfalme. Mfalme akauliza, “Ni nini hiki unachotaka?”
17 A [ona] mu odpowiedziała: Mój panie, ty przysiągłeś swojej służącej na PANA, swego Boga: Twój syn, Salomon, będzie królował po mnie i on zasiądzie na moim tronie.
Akamwambia, “Bwana wangu, wewe mwenyewe uliniapia mimi mtumishi wako kwa Bwana Mungu wako kwamba: ‘Solomoni Mwanao atakuwa mfalme baada yangu na ndiye atakayeketi kwenye kiti changu cha ufalme.’
18 A oto teraz Adoniasz króluje, a ty, mój panie, królu, [o tym] nie wiesz.
Lakini sasa Adoniya amekuwa mfalme, nawe, bwana wangu mfalme huna habari kuhusu jambo hilo.
19 Zabił bowiem woły, tuczne bydło i bardzo dużo owiec i zaprosił wszystkich synów króla, kapłana Abiatara oraz dowódcę wojska, Joaba, ale twego sługi Salomona nie zaprosił.
Ametoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo, naye amewaalika wana wa mfalme wote, kuhani Abiathari, na Yoabu jemadari wa jeshi, lakini hakumwalika Solomoni mtumishi wako.
20 Lecz ty, mój panie, królu, [wiesz], że oczy całego Izraela są zwrócone na ciebie, abyś im oznajmił, kto zasiądzie na tronie mego pana, króla, po nim.
Bwana wangu mfalme, macho ya Israeli yote yanakutazama wewe wajue kutoka kwako kuwa ni nani atakayeketi katika kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake.
21 W przeciwnym razie, gdy mój pan, król, zaśnie ze swymi ojcami, ja i mój syn Salomon będziemy uważani za przestępców.
Kama sivyo, mara tu bwana wangu mfalme atakapopumzishwa pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Solomoni tutatendewa kama wahalifu.”
22 A gdy jeszcze rozmawiała z królem, przyszedł prorok Natan.
Alipokuwa angali anazungumza na mfalme, nabii Nathani akafika.
23 I oznajmiono królowi: Oto prorok Natan. I gdy wszedł przed oblicze króla, pokłonił się królowi twarzą do ziemi.
Wakamwambia mfalme, “Nabii Nathani yuko hapa.” Kisha akaenda mbele ya mfalme na kumsujudia hadi uso wake ukagusa ardhi.
24 Potem Natan powiedział: Mój panie, królu, czy ty powiedziałeś: Adoniasz będzie królował po mnie i on zasiądzie na moim tronie?
Nathani akasema, “Je, bwana wangu mfalme, umetangaza kuwa Adoniya atakuwa mfalme baada yako na kwamba ataketi kwenye kiti chako cha ufalme?
25 Dziś bowiem zstąpił i zabił woły, tuczne bydło oraz bardzo dużo owiec, i zaprosił wszystkich synów króla, dowódców wojsk oraz kapłana Abiatara, a oto oni jedzą z nim i piją, i mówią: Niech żyje król Adoniasz!
Leo ameshuka na kutoa dhabihu idadi kubwa ya ngʼombe, ndama walionona na kondoo. Amewaalika wana wote wa mfalme, jemadari wa jeshi na kuhani Abiathari. Sasa hivi, wanakula na kunywa pamoja naye wakisema, ‘Aishi maisha marefu, Mfalme Adoniya!’
26 Lecz mnie, twego sługi, i kapłana Sadoka, i Benajasza, syna Jehojady, oraz twego sługi Salomona nie zaprosił.
Lakini mimi mtumishi wako, kuhani Sadoki, Benaya mwana wa Yehoyada na mtumishi wako Solomoni hakutualika.
27 Czy wyszło to od mego pana, króla, a nie oznajmiłeś swemu słudze, kto zasiądzie po nim na tronie mego pana, króla?
Je, hili ni jambo ambalo bwana wangu mfalme amelifanya pasipo kuwajulisha watumishi wake ili wapate kujua ni nani atakayeketi kwenye kiti cha ufalme cha bwana wangu mfalme baada yake?”
28 Król Dawid odpowiedział: Zawołajcie mi Batszebę. Ta weszła przed oblicze króla i stanęła przed nim.
Ndipo Mfalme Daudi akasema, “Mwite Bathsheba, aingie ndani.” Hivyo akaingia mbele ya mfalme na kusimama mbele yake.
29 Wtedy król przysiągł: Jak żyje PAN, który wybawił moją duszę z wszelkiego ucisku;
Ndipo mfalme akaapa: “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka kila taabu,
30 Jak przysiągłem ci na PANA, Boga Izraela: Twój syn Salomon będzie królować po mnie i on zasiądzie na moim tronie zamiast mnie, tak dziś uczynię.
hakika nitatekeleza leo kile nilichokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli: Mwanao Solomoni atakuwa mfalme baada yangu, naye ataketi kwenye kiti changu cha ufalme baada yangu.”
31 Batszeba schyliła się twarzą ku ziemi i pokłoniła się królowi, i powiedziała: Niech żyje mój pan, król Dawid, na wieki!
Kisha Bathsheba akasujudu akipiga magoti mbele ya mfalme uso wake ukigusa ardhi akasema, “Bwana wangu Mfalme Daudi na aishi milele!”
32 Potem król Dawid rozkazał: Zawołajcie mi kapłana Sadoka, proroka Natana i Benajasza, syna Jehojady. I [tamci] weszli przed oblicze króla.
Mfalme Daudi akasema, “Mwite kuhani Sadoki ndani, nabii Nathani na Benaya mwana wa Yehoyada.” Walipofika mbele ya mfalme,
33 A król powiedział im: Weźcie ze sobą sługi waszego pana, wsadźcie mego syna Salomona na moją mulicę i sprowadźcie go do Gichonu.
akawaambia: “Wachukueni watumishi wa bwana wenu pamoja nanyi na mkamkalishe mwanangu Solomoni juu ya nyumbu wangu mwenyewe mkamteremshe hadi Gihoni.
34 A tam niech kapłan Sadok i prorok Natan namaszczą go na króla nad Izraelem. Następnie zadmijcie w trąbę i powiedzcie: Niech żyje król Salomon!
Huko kuhani Sadoki na nabii Nathani wamtie mafuta awe mfalme juu ya Israeli. Pigeni tarumbeta na mpaze sauti, ‘Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!’
35 Potem pójdziecie za nim, a on przyjdzie i zasiądzie na moim tronie, i będzie królował na moje miejsce. Jego bowiem ustanowiłem wodzem nad Izraelem i nad Judą.
Kisha mtapanda pamoja naye, atakuja na kuketi kwenye kiti changu cha ufalme na kutawala badala yangu. Nimemweka awe mtawala juu ya Israeli na Yuda.”
36 Benajasz, syn Jehojady, odpowiedział królowi: Amen. Niech to stwierdzi PAN, Bóg mego pana, króla.
Benaya mwana wa Yehoyada akamjibu mfalme, “Amen! Bwana, Mungu wa bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
37 Jak PAN był z moim panem, królem, tak niech będzie z Salomonem i niech wywyższy jego tron nad tron mego pana, króla Dawida.
Kama vile Bwana alivyokuwa na bwana wangu mfalme, vivyo hivyo na awe na Solomoni kukifanya kiti chake cha utawala kuwa kikuu kuliko kile cha bwana wangu Mfalme Daudi!”
38 Poszli więc kapłan Sadok, prorok Natan i Benajasz, syn Jehojady, oraz Keretyci i Peletyci i wsadzili Salomona na mulicę króla Dawida, i zaprowadzili go do Gichonu.
Hivyo kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi wakampandisha Solomoni juu ya nyumbu wa Mfalme Daudi, nao wakamsindikiza hadi Gihoni.
39 Wtedy kapłan Sadok wziął róg olejku z namiotu i namaścił Salomona. Potem zadęto w trąbę, a cały lud powiedział: Niech żyje król Salomon!
Kuhani Sadoki akachukua pembe ya mafuta kutoka kwenye hema takatifu na kumtia Solomoni mafuta. Kisha wakapiga tarumbeta na watu wote wakapaza sauti wakisema, “Mfalme Solomoni aishi maisha marefu!”
40 I cały lud szedł za nim. Lud także grał na fletach i tak bardzo się radował, że ziemia drżała od jego głosu.
Na watu wote wakakwea wakimfuata, wakipiga filimbi na kushangilia sana, hata ardhi ikatikisika kwa ile sauti.
41 I usłyszeli to Adoniasz oraz wszyscy zaproszeni, którzy z nim byli, a właśnie skończyli ucztę. A gdy Joab usłyszał głos trąby, zapytał: Cóż to za krzyk poruszonego miasta?
Adoniya pamoja na wageni wote waliokuwa pamoja naye wakasikia sauti hiyo walipokuwa wakimalizia karamu yao. Waliposikia sauti ya tarumbeta, Yoabu akauliza, “Nini maana ya makelele yote haya katika mji?”
42 A gdy on jeszcze mówił, przyszedł Jonatan, syn kapłana Abiatara. Adoniasz powiedział mu: Wejdź, jesteś bowiem dzielnym człowiekiem i przynosisz dobrą nowinę.
Hata alipokuwa anasema, Yonathani mwana wa kuhani Abiathari akafika. Adoniya akasema, “Ingia ndani. Mtu mstahiki kama wewe ni lazima alete habari njema.”
43 Wtedy Jonatan odpowiedział Adoniaszowi: Nasz pan, król Dawid, ustanowił królem Salomona.
Yonathani akajibu, “La hasha! Mfalme Daudi bwana wetu amemfanya Solomoni kuwa mfalme.
44 Król bowiem posłał z nim kapłana Sadoka i proroka Natana oraz Benajasza, syna Jehojady, do tego Keretytów i Peletytów, którzy wsadzili go na mulicę króla;
Mfalme amemtuma pamoja naye kuhani Sadoki, nabii Nathani, Benaya mwana wa Yehoyada, Wakerethi na Wapelethi, nao wamempandisha juu ya nyumbu wa mfalme,
45 Następnie kapłan Sadok i prorok Natan namaścili go na króla w Gichonie. I wyruszyli stamtąd, tak się radując, że miasto zadrżało. Stąd ten krzyk, który usłyszeliście.
nao kuhani Sadoki na nabii Nathani wamemtia mafuta kuwa mfalme huko Gihoni. Kuanzia hapo wameendelea kushangilia na sauti zimeenea pote mjini. Hizo ndizo kelele unazosikia.
46 A Salomon zasiadł już na tronie królestwa.
Zaidi ya hayo, Solomoni ameketi juu ya kiti chake cha ufalme.
47 Ponadto przyszli słudzy króla, aby błogosławić naszemu panu, królowi Dawidowi, mówiąc: Niech Bóg sławniejszym uczyni imię Salomona niż twoje imię i niech wywyższy jego tron ponad twój tron. A król skłonił się na [swym] łożu.
Pia, maafisa wa mfalme wamekuja ili kumtakia heri bwana wetu Mfalme Daudi wakisema, ‘Mungu wako na alifanye jina la Solomoni kuwa mashuhuri kuliko lako na kiti chake cha ufalme kiwe na ukuu kuliko chako!’ Naye mfalme akasujudu akiabudu kitandani mwake
48 Również sam król powiedział: Błogosławiony [niech będzie] PAN, Bóg Izraela, który dał dziś zasiadającego na moim tronie, a moje oczy to widzą.
na kusema, ‘Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye ameruhusu macho yangu kuona mrithi juu ya kiti changu cha ufalme leo hii.’”
49 Wtedy zlękli się wszyscy zaproszeni, którzy byli z Adoniaszem, i wstali, i poszli każdy swoją drogą.
Katika hili, wageni wote wa Adoniya wakainuka kwa mshtuko wa hofu na kutawanyika.
50 Adoniasz także, bojąc się Salomona, wstał, poszedł i uchwycił się rogów ołtarza.
Lakini Adoniya kwa kumwogopa Solomoni, akaenda na kushika pembe za madhabahu.
51 I doniesiono o tym Salomonowi: Oto Adoniasz boi się króla Salomona i uchwycił się rogów ołtarza, mówiąc: Niech mi dziś przysięgnie król Salomon, że nie zabije swego sługi mieczem.
Kisha Solomoni akaambiwa, “Adoniya anamwogopa Mfalme Solomoni na ameshikilia pembe za madhabahu. Anasema, ‘Mfalme Solomoni na aniapie leo kwamba hatamuua mtumishi wake kwa upanga.’”
52 Wtedy Salomon odpowiedział: Jeśli okaże się godziwym człowiekiem, nie spadnie mu nawet włos na ziemię, ale jeśli znajdzie się w nim zło, poniesie śmierć.
Solomoni akajibu, “Kama akijionyesha kuwa mtu mstahiki, hakuna unywele wake utakaoanguka juu ya ardhi, lakini kama uovu ukionekana ndani yake, atakufa.”
53 Król Salomon posłał więc, aby go sprowadzono od ołtarza. Kiedy przyszedł, pokłonił się królowi Salomonowi. A powiedział mu Salomon: Idź do swego domu.
Ndipo Mfalme Solomoni akawatuma watu, nao wakamshusha kutoka madhabahuni. Naye Adoniya akaja akamwinamia Mfalme Solomoni, naye Solomoni akamwambia, “Nenda nyumbani kwako.”

< I Królewska 1 >