< I Królewska 10 >
1 A gdy królowa Saby usłyszała o sławie Salomona [i] o imieniu PANA, przybyła, aby go przez zagadki poddać próbie.
Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni na uhusiano wake na jina la Bwana, akaja kumjaribu kwa maswali magumu.
2 Przybyła do Jerozolimy z bardzo wielkim orszakiem, z wielbłądami niosącymi wonności, bardzo dużo złota i drogocenne kamienie. Gdy przyszła do Salomona, rozmawiała z nim o wszystkim, co leżało jej na sercu.
Alifika Yerusalemu akiwa na msafara mkubwa sana: pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani; alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
3 Salomon zaś odpowiedział na wszystkie jej pytania. Nie było nic nieznanego królowi, czego nie mógłby jej odpowiedzieć.
Solomoni akamjibu maswali yake yote, hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwa mfalme asiweze kumwelezea.
4 Gdy więc królowa Saby ujrzała całą mądrość Salomona i dom, który zbudował;
Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
5 A także potrawy jego stołu, siadanie jego sług, stawanie jego służących, ich szaty, jego podczaszych oraz schody, po których wstępował do domu PANA, dech zamarł jej [w piersi];
chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika hekalu la Bwana, alipatwa na mshangao.
6 Wtedy przemówiła do króla: Prawdziwa była ta wieść, którą słyszałam w swojej ziemi o twoich dziełach i twojej mądrości.
Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
7 Jednak nie wierzyłam tym słowom, aż przybyłam i zobaczyłam [to] na własne oczy. I oto nie powiedziano mi nawet połowy. Twoja mądrość i [twój] dobrobyt są większe od sławy, o której słyszałam.
Lakini sikuamini mambo haya hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana ile taarifa niliyoisikia.
8 Błogosławieni twoi ludzie, błogosławieni twoi słudzy, którzy zawsze stoją przed tobą i słuchają twojej mądrości.
Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
9 Niech będzie błogosławiony PAN, twój Bóg, który cię sobie upodobał, aby cię posadzić na tronie Izraela; a ponieważ PAN umiłował Izraela na wieki, ustanowił cię królem, abyś czynił sąd i sprawiedliwość.
Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe na kukuweka juu ya kiti cha ufalme cha Israeli. Kwa sababu ya upendo wake Bwana wa milele ajili ya Israeli, amekufanya mfalme, ili kudumisha haki na uadilifu.”
10 Następnie dała królowi sto dwadzieścia talentów złota i bardzo wiele wonności oraz drogocennych kamieni. Nigdy więcej nie przyniesiono tyle wonności, ile królowi Salomonowi dała królowa Saby.
Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa sana cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa tena vikolezi vingi hivyo kuletwa kama vile malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
11 Ponadto okręty Hirama, które przywoziły złoto z Ofiru, przywiozły także z Ofiru wielką ilość drewna sandałowego i drogocennych kamieni.
(Meli za Hiramu zilileta dhahabu kutoka Ofiri; tena kutoka huko zilileta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
12 Z tego drzewa sandałowego król wykonał schody do domu PANA i do domu królewskiego oraz harfy i cytry dla śpiewaków. Nigdy nie sprowadzono takiego drzewa sandałowego i nie widziano aż do dziś.
Mfalme akatumia miti ya msandali kuwa nguzo ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa au kuonekana humo tangu siku ile.)
13 Król Salomon zaś dał królowej Saby wszystko, czego zapragnęła [i] o co poprosiła, nie licząc [tego], co jej dał ze swojej królewskiej hojności. Potem odjechała i wróciła do swojej ziemi razem ze swoimi sługami.
Mfalme Solomoni akampa malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, kando na vile mfalme alivyokuwa amempa kwa ukarimu wake wa kifalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
14 A waga złota, które wpływało do Salomona w ciągu jednego roku, wynosiła sześćset sześćdziesiąt sześć talentów złota;
Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
15 Nie licząc tego, [co dostawał] od kupców i handlarzy wonności, i od wszystkich królów arabskich oraz namiestników ziemi.
mbali na mapato kutoka kwa wafanyabiashara na wachuuzi, na kutoka kwa wafalme wote wa Kiarabu na watawala wa nchi.
16 Król Salomon wykonał więc dwieście tarcz z kutego złota. Na każdą tarczę wychodziło sześćset [syklów] złota.
Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa; kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
17 [Wykonał] także trzysta puklerzy z kutego złota, używając po trzy miny złota na każdy puklerz. Król umieścił je w domu lasu Libanu.
Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
18 Król również sporządził wielki tron z kości słoniowej i pokrył go czystym złotem.
Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
19 Tron [miał] sześć stopni i okrągły szczyt z tyłu. Po obu stronach siedzenia były poręcze, a przy poręczach stały dwa lwy.
Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na egemeo la nyuma lilikuwa la mviringo kwa juu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
20 Dwanaście lwów stało na tych sześciu stopniach po obu stronach. Czegoś takiego nie uczyniono w żadnym [innym] królestwie.
Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
21 Wszystkie naczynia, których król Salomon używał do picia, były ze złota, a także wszystkie naczynia domu lasu Libanu [były] ze szczerego złota. Nie było nic ze srebra, gdyż nie uważano go za cenne w czasach Salomona.
Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo siku za Solomoni.
22 Królewska flota Tarszisz [była] bowiem na morzu wraz z flotą Hirama. Raz na trzy lata przypływała flota Tarszisz, przywożąc złoto, srebro, kość słoniową, małpy i pawie.
Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizokuwa zikiandamana na meli za Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
23 Tak więc król Salomon przewyższał wszystkich królów ziemi bogactwem i mądrością.
Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
24 I cała ziemia pragnęła zobaczyć Salomona, aby słuchać jego mądrości, którą Bóg włożył w jego serce.
Dunia yote ikatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
25 Każdy przynosił mu swoje dary: srebrne i złote naczynia, szaty, zbroje, wonności, konie i muły, rokrocznie.
Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja alileta zawadi: vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
26 Salomon nagromadził rydwanów i jeźdźców, tak że miał tysiąc czterysta rydwanów i dwanaście tysięcy jeźdźców, których rozmieścił po miastach rydwanów oraz przy sobie w Jerozolimie.
Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
27 Król sprawił, że srebro w Jerozolimie było jak kamienie, a cedry tak liczne jak sykomory na nizinie.
Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
28 Sprowadzono też dla Salomona konie z Egiptu i nić lnianą. A kupcy królewscy brali nić lnianą za [ustaloną] cenę.
Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
29 Rydwan wywożono i sprowadzono z Egiptu za sześćset srebrników, a konia – za sto pięćdziesiąt. W ten sposób wszyscy królowie chetyccy i królowie Syrii dostawali [je] za ich pośrednictwem.
Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.