< I Kronik 6 >

1 Synowie Lewiego: Gerszom, Kehat i Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
2 A synowie Kehata: Amram, Ishar, Chebron i Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
3 A dzieci Amrama: Aaron, Mojżesz i Miriam. Synowie Aarona: Nadab, Abihu, Eleazar i Itamar.
Amramu alikuwa na wana: Aroni, Mose, na Miriamu. Aroni alikuwa na wana: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
4 Eleazar spłodził Pinchasa, a Pinchas spłodził Abiszuę.
Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
5 Abiszua spłodził Bukkiego, a Bukki spłodził Uzziego.
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi,
6 Uzzi spłodził Zerachiasza, a Zerachiasz spłodził Merajota.
Uzi akamzaa Zerahia, Zerahia akamzaa Merayothi,
7 Merajot spłodził Amariasza, a Amariasz spłodził Achituba.
Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
8 Achitub spłodził Sadoka, a Sadok spłodził Achimaasa.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi,
9 Achimaas spłodził Azariasza, a Azariasz spłodził Jochanana.
Ahimaasi akamzaa Azaria, Azaria akamzaa Yohanani,
10 Jochanan spłodził Azariasza. On to sprawował urząd kapłański w świątyni, którą Salomon zbudował w Jerozolimie.
Yohanani akamzaa Azaria (ndiye alifanya kazi ya ukuhani katika Hekalu alilojenga Mfalme Solomoni huko Yerusalemu),
11 Azariasz spłodził Amariasza, a Amariasz spłodził Achituba.
Azaria akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
12 Achitub spłodził Sadoka, a Sadok spłodził Szalluma.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Shalumu,
13 Szallum spłodził Chilkiasza, a Chilkiasz spłodził Azariasza.
Shalumu akamzaa Hilkia, Hilkia akamzaa Azaria,
14 Azariasz spłodził Serajasza, a Serajasz spłodził Jehocadaka.
Azaria akamzaa Seraya, Seraya akamzaa Yehosadaki.
15 A Jehocadak trafił [do niewoli], gdy PAN uprowadził Judę i Jerozolimę przez Nabuchodonozora.
Yehosadaki alihamishwa wakati Bwana aliwapeleka uhamishoni watu wa Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Mfalme Nebukadneza.
16 Synowie Lewiego: Gerszom, Kehat i Merari.
Wana wa Lawi walikuwa: Gershoni, Kohathi na Merari.
17 A to [są] imiona synów Gerszoma: Libni i Szimei.
Haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni: Libni na Shimei.
18 A synowie Kehata: Amram, Ishar, Chebron i Uzziel.
Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
19 Synowie Merariego: Machli i Muszi. A to są rody Lewitów według ich ojców.
Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Zifuatazo ni koo za Walawi zilizoorodheshwa kufuatana na baba zao:
20 Od Gerszoma: jego syn Libni, jego syn Jachat, jego syn Zimma;
Wazao wa Gershoni: Gershoni akamzaa Libni, Libni akamzaa Yahathi, Yahathi akamzaa Zima,
21 Jego syn Joach, jego syn Iddo, jego syn Zerach, jego syn Jeatraj.
Zima akamzaa Yoa, Yoa akamzaa Ido, Ido akamzaa Zera, Zera akamzaa Yeatherai.
22 Synowie Kehata: jego syn Amminadab, jego syn Korach, jego syn Assir;
Wazao wa Kohathi: Kohathi akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Kora, Kora akamzaa Asiri,
23 Jego syn Elkana, jego syn Ebiasaf, jego syn Assir;
Asiri akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Ebiasafu, Ebiasafu akamzaa Asiri,
24 Jego syn Tachat, jego syn Uriel, jego syn Uzjasz, jego syn Saul.
Asiri akamzaa Tahathi, Tahathi akamzaa Urieli, Urieli akamzaa Uzia, Uzia akamzaa Shauli.
25 Synowie Elkany: Amasaj, Achimot i Elkana.
Wazao wa Elikana walikuwa: Amasai na Ahimothi,
26 Synowie Elkany: jego syn Sofaj, jego syn Nachat;
Ahimothi akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Sofai, Sofai akamzaa Nahathi,
27 Jego syn Eliab, jego syn Jerocham, jego syn Elkana.
Nahathi akamzaa Eliabu, Eliabu akamzaa Yerohamu, Yerohamu akamzaa Elikana, Elikana akamzaa Samweli.
28 Synowie Samuela: pierworodny Waszni i Abiasz.
Wana wa Samweli walikuwa: Yoeli mzaliwa wake wa kwanza, na Abiya mwanawe wa pili.
29 Synowie Merariego: Machli, jego syn Libni, jego syn Szimei, jego syn Uzza;
Wafuatao ndio wazao wa Merari: Merari akamzaa Mahli, Mahli akamzaa Libni, Libni akamzaa Shimei, Shimei akamzaa Uza,
30 Jego syn Szimea, jego syn Chaggiasz, jego syn Asajasz.
Uza akamzaa Shimea, Shimea akamzaa Hagia, Hagia akamzaa Asaya.
31 To są ci, których Dawid ustanowił do prowadzenia śpiewu w domu PANA, odkąd spoczęła [tam] arka.
Hawa ndio watu ambao Daudi aliwaweka kuwa viongozi wa uimbaji katika nyumba ya Bwana, baada ya Sanduku la Agano kuletwa ili kukaa huko.
32 I posługiwali śpiewem przed przybytkiem, [czyli] Namiotem Zgromadzenia, aż Salomon zbudował dom PANA w Jerozolimie. Stawali do swojej służby według swego porządku.
Walihudumu kwa kuimba mbele ya Maskani, Hema la Kukutania, mpaka hapo Mfalme Solomoni alipojenga Hekalu la Bwana huko Yerusalemu. Walitimiza wajibu wao kulingana na taratibu walizokuwa wamewekewa.
33 A oto ci, którzy stawali wraz ze swoimi synami: spośród synów Kehata – śpiewak Heman, syn Joela, syna Samuela;
Wafuatao ni watu waliohudumu pamoja na wana wao: Kutoka ukoo wa Kohathi walikuwa: Hemani, mpiga kinanda, alikuwa mwana wa Yoeli, mwana wa Samweli,
34 Syna Elkany, syna Jerochama, syna Eliela, syna Toacha;
mwana wa Elikana, mwana wa Yerohamu, mwana wa Elieli, mwana wa Toa,
35 Syna Sufa, syna Elkany, syna Machata, syna Amasaja;
mwana wa Sufu, mwana wa Elikana, mwana wa Mahathi, mwana wa Amasai,
36 Syna Elkany, syna Joela, syna Azariasza, syna Sofoniasza;
mwana wa Elikana, mwana wa Yoeli, mwana wa Azaria, mwana wa Sefania,
37 Syna Tachata, syna Assira, syna Ebiasafa, syna Koracha;
mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora,
38 Syna Ishara, syna Kehata, syna Lewiego, syna Izraela.
mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, mwana wa Israeli;
39 Oraz jego brat Asaf, który stawał po jego prawicy. Asaf, syn Berechiasza, syna Szimei;
na msaidizi wa Hemani alikuwa Asafu, aliyesimama mkono wa kuume: Asafu mwana wa Berekia, mwana wa Shimea,
40 Syna Mikaela, syna Baasejasza, syna Malkiasza;
mwana wa Mikaeli, mwana wa Baaseya, mwana wa Malkiya,
41 Syna Etniego, syna Zeracha, syna Adajasza;
mwana wa Ethni, mwana wa Zera, mwana wa Adaya,
42 Syna Etana, syna Zimmy, syna Szimejego;
mwana wa Ethani, mwana wa Zima, mwana wa Shimei,
43 Syna Jachata, syna Gerszoma, syna Lewiego.
mwana wa Yahathi, mwana wa Gershoni, mwana wa Lawi.
44 A ich bracia, synowie Merariego, [stawali] po lewej stronie: Etan, syn Kisziego, syna Abdiego, syna Malluka;
Na kutoka kwa walioshirikiana nao, Wamerari, mkono wake wa kushoto: Ethani mwana wa Kishi, mwana wa Abdi, mwana wa Maluki,
45 Syna Chaszabiasza, syna Amaziasza, syna Chilkiasza.
mwana wa Hashabia, mwana wa Amazia, mwana wa Hilkia,
46 Syna Amsjego, syna Baniego, syna Szamera;
mwana wa Amsi, mwana wa Bani, mwana wa Shemeri,
47 Syna Mochliego, syna Musziego, syna Merariego, syna Lewiego.
mwana wa Mahli, mwana wa Mushi, mwana wa Merari, mwana wa Lawi.
48 A ich bracia, Lewici, [byli] ustanowieni do wszelkiej posługi w przybytku domu Boga.
Ndugu zao wengine Walawi walipewa huduma nyingine za kuhudumia hema takatifu, nyumba ya Mungu.
49 Aaron zaś i jego synowie palili kadzidło na ołtarzu całopalenia i na ołtarzu kadzenia, [byli odpowiedzialni] za wszelką posługę w Miejscu Najświętszym i za dokonywanie przebłagania za Izraela według wszystkiego, co nakazał Mojżesz, sługa Boży.
Lakini Aroni na uzao wake ndio waliokuwa na wajibu wa kutoa sadaka katika madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na kwenye madhabahu ya kufukizia uvumba pamoja na yote yaliyofanyika pa Patakatifu, wakifanya upatanisho kwa ajili ya Israeli, sawasawa na yale yote aliyoagiza Mose mtumishi wa Mungu.
50 A oto synowie Aarona: jego syn Eleazar, jego syn Pinchas;
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Aroni: Aroni akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Finehasi, Finehasi akamzaa Abishua,
51 Jego syn Abiszua, jego syn Bukki, jego syn Uzzi, jego syn Zerachiasz;
Abishua akamzaa Buki, Buki akamzaa Uzi, Uzi akamzaa Zerahia,
52 Jego syn Merajot, jego syn Amariasz, jego syn Achitub;
Zerahia akamzaa Merayothi, Merayothi akamzaa Amaria, Amaria akamzaa Ahitubu,
53 Jego syn Sadok, jego syn Achimaas.
Ahitubu akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Ahimaasi.
54 A to są ich mieszkania według ich wieży w ich obszarze, [to jest] synów Aarona, według rodu Kehatytów. Był [to] bowiem ich los.
Zifuatazo ni sehemu walizopewa ziwe nchi yao kwa ajili ya makazi yao (walipewa wazao wa Aroni waliotoka katika ukoo wa Wakohathi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
55 Oddano im Hebron w ziemi Judy wraz z pastwiskami dokoła niego;
Walipewa Hebroni katika nchi ya Yuda pamoja na sehemu ya malisho inayouzunguka.
56 Lecz pola miasta i jego wsie dano Kalebowi, synowi Jefunnego.
Lakini mashamba pamoja na vijiji vilivyouzunguka mji alipewa Kalebu mwana wa Yefune.
57 Synom Aarona zaś dano spośród miast Judy [miasta] schronienia: Hebron, Libnę z jego pastwiskami, Jattir i Esztemoę wraz z ich pastwiskami;
Kwa hiyo wazao wa Aroni walipewa miji ifuatayo pamoja na eneo la malisho: Hebroni (mji wa makimbilio), Libna, Yatiri, Eshtemoa,
58 I Chilen z jego pastwiskami, Debir z jego pastwiskami;
Hileni, Debiri,
59 Aszan z jego pastwiskami i Bet-Szemesz z jego pastwiskami.
Ashani, Yuta na Beth-Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho.
60 A od pokolenia Beniamina: Geba z jego pastwiskami, Alemet z jego pastwiskami i Anatot z jego pastwiskami. Wszystkich ich miast było trzynaście według ich rodzin.
Kutoka kabila la Benyamini walipewa Gibeoni, Geba, Alemethi na Anathothi, pamoja na maeneo yake ya malisho. Miji hii kumi na mitatu iligawanywa miongoni mwa koo za Wakohathi.
61 A pozostałym synom Kehata, spośród rodziny tego pokolenia, przypadło losem dziesięć miast od połowy pokolenia Manassesa.
Wazao waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za nusu ya kabila la Manase.
62 A synom Gerszoma według ich rodzin przypadło od pokolenia Issachara, od pokolenia Aszera, od pokolenia Neftalego i od pokolenia Manassesa w Baszanie – trzynaście miast.
Wazao wa Gershoni, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na mitatu kutoka kwa makabila ya Isakari, Asheri na Naftali kutoka sehemu ya kabila la Manase huko Bashani.
63 Synom Merariego według ich rodzin przypadło losem od pokolenia Rubena, od pokolenia Gada i od pokolenia Zebulona – dwanaście miast.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
64 Synowie Izraela dali Lewitom te miasta wraz z ich pastwiskami.
Kwa hiyo Waisraeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yake ya malisho.
65 A dali przez los od pokolenia synów Judy, od pokolenia synów Symeona i od pokolenia synów Beniamina te miasta, którym nadali ich imiona.
Kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini walipewa miji iliyotajwa hapo juu.
66 A ci, którzy pochodzili z rodu synów Kehata, mieli miasta w granicach pokolenia Efraima.
Baadhi ya koo za Wakohathi walipewa kama nchi yao miji kutoka kabila la Efraimu.
67 Dano im z miast schronienia: Sychem z jego pastwiskami na górze Efraim i Gezer z jego pastwiskami;
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji wa makimbilio) na Gezeri,
68 Jokmeam z jego pastwiskami, Bet-Choron z jego pastwiskami;
Yokmeamu, Beth-Horoni,
69 Ajjalon z jego pastwiskami i Gat-Rimmon z jego pastwiskami.
Aiyaloni na Gath-Rimoni, pamoja na maeneo yake ya malisho.
70 Od połowy pokolenia Manassesa: Aner z jego pastwiskami, Bileam z jego pastwiskami. [Dano to] rodzinie pozostałych synów Kehata.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, Waisraeli waliwapa koo za Wakohathi waliobaki miji ya Aneri na Bileamu pamoja na maeneo yake ya malisho.
71 Synom Gerszoma [dano] od połowy pokolenia Manassesa Golan w Baszanie z jego pastwiskami i Asztarot z jego pastwiskami;
Wagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho: Katika nusu ya kabila la Manase: walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.
72 Od pokolenia Issachara – Kedesz z jego pastwiskami, Daberat z jego pastwiskami;
Kutoka kabila la Isakari walipokea Kedeshi, Daberathi,
73 Ramot z jego pastwiskami i Anem z jego pastwiskami.
Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
74 Od pokolenia Aszera: Maszal z jego pastwiskami, Abdon z jego pastwiskami;
Kutoka kabila la Asheri walipokea Mashali, Abdoni,
75 Chukok z jego pastwiskami i Rechob z jego pastwiskami.
Hukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.
76 Od pokolenia Neftalego: Kedesz w Galilei z jego pastwiskami, Chammon z jego pastwiskami i Kiriataim z jego pastwiskami.
Kutoka kabila la Naftali walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
77 Pozostałym synom Merariego [dano] od pokolenia Zebulona Rimmon z jego pastwiskami i Tabor z jego pastwiskami.
Wamerari (Walawi waliobakia) walipokea miji ifuatayo: kutoka kabila la Zabuloni walipokea Yokneamu, Karta, Rimoni na Tabori pamoja na maeneo yake ya malisho.
78 A po drugiej stronie Jordanu koło Jerycha, na wschód od Jordanu, [dano] od pokolenia Rubena: Beser na pustyni z jego pastwiskami, Jahazę z jej pastwiskami;
Kutoka kabila la Reubeni, ngʼambo ya Yordani mashariki mwa Yeriko walipokea Bezeri ulioko jangwani, Yahasa,
79 Kedemot z jego pastwiskami i Mefaat z jego pastwiskami.
Kedemothi na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
80 Od pokolenia Gada: Ramot w Gileadzie z jego pastwiskami, Machanaim z jego pastwiskami;
Na kutoka kabila la Gadi walipokea Ramothi huko Gileadi, Mahanaimu,
81 Cheszbon z jego pastwiskami i Jazer z jego pastwiskami.
Heshboni na Yazeri, pamoja na maeneo yake ya malisho.

< I Kronik 6 >