< Rzymian 6 >

1 Cóż tedy rzeczemy? Zostaniemyż w grzechu, aby łaska obfitowała?
Tuseme nini basi? Tuendelee katika dhambi ili neema iongezeke?
2 Nie daj tego Boże! albowiem którzyśmy umarli grzechowi, jakoż jeszcze w nim żyć będziemy?
La hasha. Sisi tuliokufa katika dhambi, tunawezaje tena kuishi katika hiyo?
3 Azaż nie wiecie, iż którzykolwiek ochrzczeni jesteśmy w Chrystusa Jezusa, w śmierć jego ochrzczeni jesteśmy?
Je hamjui ya kuwa wale waliobatizwa katika Kristo walibatizwa katika mauti yake?
4 Pogrzebieniśmy tedy z nim przez chrzest w śmierć, aby jako Chrystus wzbudzony jest z martwych przez chwałę ojcowską, tak żebyśmy i my w nowości żywota chodzili.
Tulikuwa tumezikwa pamoja naye kupitia ubatizo katika kifo. Hii ilifanyika ili kwamba kama vile Kristo alivyoinuliwa kutoka mauti kupitia utukufu wa Baba, ili kwamba nasi tuweze kutembea katika upya wa maisha.
5 Bo jeźliżeśmy z nim wszczepieni w podobieństwo śmierci jego, tedy też i w podobieństwo zmartwychwstania wszczepieni z nim będziemy.
Maana ikiwa tumeunganishwa pamoja naye katika mfano wa kifo chake, pia tutaunganishwa katika ufufuo wake.
6 To wiedząc, że stary nasz człowiek pospołu jest z nim ukrzyżowany, aby ciało grzechu było zniszczone, żebyśmy już więcej nie służyli grzechowi;
Sisi tunajua hivi, utu wetu wa zamani ulisulubiwa pamoja naye, ili kwamba mwili wa dhambi uharibiwe. Hii ilitokea ili kwamba tusiendelee kuwa watumwa wa dhambi.
7 Bo ktoć umarł, usprawiedliwiony jest od grzechu.
Yeye aliyekufa amefanywa mwenye haki kulingana na dhambi.
8 Jeźliśmy tedy z Chrystusem umarli, wierzymy, iż też z nim żyć będziemy,
Lakini kama tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pamoja naye pia.
9 Wiedząc, że Chrystus powstawszy z martwych, więcej nie umiera i śmierć mu więcej nie panuje.
Tunajua kwamba Kristo amefufuliwa kutoka katika wafu, na kwamba si mfu tena. Kifo hakimtawali tena.
10 Bo iż umarł, grzechowi raz umarł, a iż żyje, żyje Bogu.
Maana kwa habari ya kifo alichokufa kwa dhambi, alikufa mara moja kwa ajili ya wote. Hata hivyo, maisha anayoishi, anaishi kwa ajili ya Mungu.
11 Tak też i wy rozumiejcie, żeście wy umarłymi grzechowi, aleście żywymi Bogu w Chrystusie Jezusie, Panu naszym.
Kwa njia iyo hiyo, nanyi pia mnapaswa kujihesabu kuwa wafu katika dhambi, bali hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
12 Niechże tedy nie króluje grzech w śmiertelnem ciele waszem, żebyście mu posłuszni byli w pożądliwościach jego.
Kwa sababu hiyo usiruhusu dhambi itawale mwili wako ili kusudi uweze kuzitii tamaa zake.
13 Ani stawiajcie członków waszych orężem niesprawiedliwości grzechowi: ale stawiajcie siebie samych Bogu, jako z umarłych żywi, i członki wasze orężem sprawiedliwości Bogu.
Usitoe sehemu za mwili wako katika dhambi kama vyombo visivyo na haki, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu, kama walio hai kutoka mautini. Na zitoeni sehemu za miili yenu kama vyombo vya haki kwa Mungu.
14 Albowiem grzech panować nad wami nie będzie; bo jesteście nie pod zakonem, ale pod łaską.
Msiiruhusu dhambi iwatawale. Kwa kuwa hamko chini ya sheria, bali chini ya neema.
15 Cóż tedy? Będziemyż grzeszyli, żeśmy nie pod zakonem, ale pod łaską? Nie daj tego Boże!
Nini basi? Tutende dhambi kwa kuwa hatupo chini ya sheria, bali chini ya neema? La hasha.
16 Azaż nie wiecie, że komu się stawiacie za sługi ku posłuszeństwu, tegoście sługami, komuście posłuszni; bądź grzechowi ku śmierci, bądź posłuszeństwu ku sprawiedliwości?
Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa wenyewe kama watumishi ndiye ambaye ninyi mnakuwa watumishi wake, yeye mnayepaswa kumtii? Hii ni kweli hata kama ninyi ni watumwa katika dhambi ambayo inapelekea mauti, au watumwa wa utii unaopelekea haki.
17 Ale chwała Bogu, że bywszy sługami grzechu, usłuchaliście z serca sposobu onej nauki, którejście się poddali.
Lakini ashukuriwe Mungu! Kwa kuwa mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mmetii kutoka moyoni ile namna ya fundisho mliopewa.
18 A będąc uwolnieni od grzechu, staliście się niewolnikami sprawiedliwości.
Mmefanywa huru kutoka kwenye dhambi, na mmefanywa watumwa wa haki.
19 Po ludzku mówię dla mdłości ciała waszego. Albowiem jakoście stawiali członki wasze na służbę nieczystości i nieprawości ku czynieniu nieprawości: tak teraz stawiajcie członki wasze na służbę sprawiedliwości ku poświęceniu.
Ninazungumza kama mtu kwa sababu ya madhaifu ya miili yenu. Kwa maana kama vile mlivyotoa viungo vya miili yenu kuwa watumwa kwa uchafu na uovu, kwa jinsi iyo hiyo, sasa toeni viungo vya miili yenu kuwa watumwa wa haki kwa utakaso.
20 Bo pókiście byli sługami grzechu, byliście wolnymi od sprawiedliwości:
Kwa kuwa mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na haki.
21 Jakiżeście tedy naonczas pożytek mieli onych rzeczy, za które się teraz wstydzicie? Bo koniec onych jest śmierć.
Kwa wakati huo, mlikuwa na tunda lipi kwa mambo ambayo kwa sasa mnaona aibu kwayo? Kwa kuwa matokeo ya mambo hayo ni kifo.
22 Lecz teraz, będąc uwolnieni od grzechu, a zniewoleni Bogu, macie pożytek swój ku poświęceniu, a koniec żywot wieczny. (aiōnios g166)
Lakini kwa kuwa sasa mmefanywa huru mbali na dhambi na mmefanyika watumwa kwa Mungu, mna tunda kwa ajili ya utakaso. Tokeo ni uzima wa milele. (aiōnios g166)
23 Albowiem zapłata za grzech jest śmierć; ale dar z łaski Bożej jest żywot wieczny, w Chrystusie Jezusie, Panu naszym. (aiōnios g166)
Kwa kuwa mshahara wa dhambi ni mauti, bali zawadi ya bure ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōnios g166)

< Rzymian 6 >