< Rzymian 11 >

1 Mówię tedy: Izali Bóg odrzucił lud swój? Nie daj tego Boże! Albowiem i jam jest Izraelczyk z nasienia Abrahamowego, z pokolenia Benjaminowego.
Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
2 Nie odrzuciłci Bóg ludu swego, który przejrzał. Azaż nie wiecie, co mówi Pismo o Elijaszu? jako się przyczynia do Boga przeciwko Izraelowi mówiąc:
Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
3 Panie! Proroki twoje pomordowali i ołtarze twoje zburzyli, a zostałem ja sam i szukają duszy mojej.
“Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?”
4 Ale cóż mu mówi Boska odpowiedź? Zostawiłem sobie siedm tysięcy mężów, którzy nie skłonili kolana Baalowi.
Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: “Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali.”
5 Tak tedy i teraźniejszego czasu ostatki podług wybrania z łaski zostały.
Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
6 A ponieważ z łaski, tedyć już nie z uczynków, inaczej łaska już by nie była łaską; a jeźli z uczynków, jużci nie jest łaska; inaczej uczynek już by nie był uczynkiem.
Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
7 Cóż tedy? Czego Izrael szuka, tego nie dostąpił; ale wybrani dostąpili, a inni zatwardzeni są,
Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
8 (Jako napisano: Dał im Bóg ducha twardego snu, oczy, aby nie widzieli i uszy, aby nie słyszeli), aż do dzisiejszego dnia.
kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao.”
9 A Dawid mówi: Niechaj im będzie stół ich sidłem i ułowieniem i otrąceniem i odpłatą.
Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
10 Niech zaćmione będą oczy ich, aby nie widzieli, a grzbietu ich zawsze nachylaj.
Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!”
11 Mówię tedy: Azaż się potknęli, aby padli? Nie daj tego Boże! Ale przez ich upadek doszło zbawienie pogan, aby je do zawiści przywiódł.
Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
12 A ponieważ upadek ich jest bogactwem świata, a umniejszenie ich bogactwem pogan, jakoż daleko więcej ich zupełność?
Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
13 Albowiem mówię wam poganom, ilem ja jest Apostołem pogan, usługiwanie moje zalecam,
Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
14 Azażbym jako ku zawiści pobudził ciało moje i zbawiłbym niektóre z nich.
nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
15 Albowiem jeźlić odrzucenie ich jest pojednaniem świata, cóż będzie przyjęcie ich, tylko ożycie od umarłych?
Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
16 Ponieważ jeźli pierwiastki święte, tedyć i zaczynienie; a jeźli korzeń święty, tedyć i gałęzie.
Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
17 A jeźli niektóre z gałęzi odłamane są, a ty, któryś był płonną oliwą, jesteś wszczepiony zamiast nich i stałeś się uczestnikiem korzenia i tłustości oliwnego drzewa:
Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
18 Nie chlubże się przeciw gałęziom, bo jeźli się chlubisz, wiedzże, iż nie ty korzenia nosisz, ale korzeń ciebie.
Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
19 Ale rzeczesz: Odłamane są gałęzie, abym ja był wszczepiony.
Lakini utasema: “Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake.”
20 Dobrze; dla niedowiarstwa odłamane są, ale ty wiarą stoisz; nie bądźże hardej myśli, ale się bój.
Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
21 Albowiem jeźli Bóg przyrodzonym gałęziom nie przepuścił, wiedz, że i tobie nie przepuści.
Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
22 Obaczże tedy dobrotliwość i srogość Bożą; przeciwko tym wprawdzie, którzy upadli, srogość, ale przeciwko tobie dobrotliwość, jeźlibyś trwał w dobroci; inaczej i ty będziesz wycięty.
Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
23 Aleć i oni, jeźli nie będą trwali w niedowiarstwie, wszczepieni zaś będą, gdyż mocny jest Bóg one zasię wszczepić.
Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
24 Albowiem jeźliś ty jest wycięty z oliwy, z przyrodzenia płonnej, a przeciwko przyrodzeniu jesteś wszczepiony w dobrą oliwę, jakoż daleko więcej, którzy są według przyrodzenia, wszczepieni będą w swoję własną oliwę!
Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
25 Bo nie chcę, abyście nie mieli wiedzieć, bracia! tej tajemnicy, (żebyście nie byli sami u siebie mądrymi), iż zatwardzenie z części przyszło na Izraela, póki by nie weszła zupełność pogan.
Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
26 A tak wszystek Izrael będzie zbawiony, jako napisano: Przyjdzie z Syonu wybawiciel i odwróci niepobożności od Jakóba.
Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
27 A toć będzie przymierze moje z nimi, gdy odejmę grzechy ich.
Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
28 A tak według Ewangielii nieprzyjaciółmi są dla was; lecz według wybrania są miłymi dla ojców.
Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
29 Albowiem darów swoich i wezwania Bóg nie żałuje.
Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
30 Bo jako i wy niekiedy nie wierzyliście Bogu, ale teraz dostąpiliście miłosierdzia dla ich niedowiarstwa,
Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
31 Tak i oni teraz stali się nieposłusznymi, aby dla miłosierdzia wam okazanego i oni miłosierdzia dostąpili.
Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
32 Albowiem zamknął je Bóg wszystkie w niedowiarstwo, aby się nad wszystkimi zmiłował. (eleēsē g1653)
Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote. (eleēsē g1653)
33 O głębokości bogactwa i mądrości, i znajomości Bożej! Jako są niewybadane sądy jego i niedoścignione drogi jego!
Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
34 Bo któż poznał umysł Pański? albo kto był rajcą jego?
“Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
35 Albo kto mu co pierwej dał, a będzie mu zasię oddano?
Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?”
36 Albowiem z niego i przez niego i w nim są wszystkie rzeczy; jemu niech będzie chwała na wieki. Amen. (aiōn g165)
Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina. (aiōn g165)

< Rzymian 11 >