< Objawienie 21 >

1 Potemem widział niebo nowe i ziemię nową; albowiem pierwsze niebo i pierwsza ziemia przeminęła, a morza już więcej nie było.
Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa kuwa mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza zimekwishapita, na bahari haikuwepo tena.
2 A ja Jan widziałem ono święte miasto, Jeruzalem nowe, zstępujące z nieba od Boga zgotowane, jako oblubienicę ubraną mężowi swemu.
Niliona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ambao ulikuja chini kutoka mbinguni kwa Mungu, ulioandaliwa kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
3 I słyszałem głos wielki z nieba mówiący: Oto przybytek Boży z ludźmi, i będzie mieszkał z nimi; a oni będą ludem jego, a sam Bóg będzie z nimi, będąc Bogiem ich.
Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema, “Tazama! Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao. Watakuwa watu wake, na Mungu mwenyewe atakuwa nao na atakuwa Mungu wao.
4 I otrze Bóg wszelką łzę z oczów ich; a śmierci więcej nie będzie, ani smutku, ani krzyku, ani boleści nie będzie; albowiem pierwsze rzeczy pominęły.
Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na hapatakuwa na kifo tena, au kuomboleza, au kulia, au maumivu. Mambo ya zamani yamekwishakupita.
5 I rzekł ten, który siedział na stolicy: Oto wszystko nowe czynię. I rzekł mi: Napisz: bo te słowa są wierne i prawdziwe.
Yeye ambaye alikuwa ameketi juu ya kiti cha enzi alisema, “Tazama! Nafanya mambo yote kuwa mapya.” Alisema, “Andika hili kwa sababu maneno haya ni ya hakika na kweli.”
6 I rzekł mi: Stało się. Jam jest Alfa i Omega, początek i koniec. Ja pragnącemu dam darmo ze źródła wody żywej.
Aliniambia, “Mambo haya yalikwisha kupita! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Kwa yeyote aonaye kiu nitampatia kinywaji bila gharama kutoka katika chemchemi za maji ya uzima.
7 Kto zwycięży, odziedziczy wszystko i będę mu Bogiem, a on mi będzie synem.
Yeye ashindaye atayarithi mambo haya, na nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
8 Lecz bojaźliwym i niewiernym, i obmierzłym, i mężobójcom, i wszetecznikom, i czarownikom, i bałwochwalcom, i wszystkim kłamcom część ich dana będzie w jeziorze gorejącem ogniem i siarką: Tać jest śmierć wtóra. (Limnē Pyr g3041 g4442)
Lakini kama ilivyo kwa waoga, wasioamini, wachukizao, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, sehemu yao itakuwa katika ziwa la moto wa kiberiti uunguzao. Hiyo ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr g3041 g4442)
9 Tedy przyszedł do mnie jeden z onych siedmiu Aniołów, którzy mieli siedm czasz napełnionych siedmioma plagami ostatecznemi, i mówił ze mną, i rzekł: Chodź sam, okażę ci oblubienicę, małżonkę Barankową.
Mmoja wa malaika saba alikuja kwangu, mmoja ambaye alikuwa na mabakuli saba yaliyojaa mapigo saba ya mwisho na alisema, “Njoo hapa. Nitakuonesha bibi harusi, mke wa mwana kondoo.”
10 I zaniósł mię w duchu na górę wielką i wysoką, i okazał mi miasto wielkie, ono święte Jeruzalem, zstępujące z nieba od Boga,
Kisha alinichukua mbali katika Roho kwenye mlima mkubwa na mrefu na alinionesha mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka chini kutoka mbinguni kwa Mungu.
11 Mające chwałę Bożą, którego światłość podobna była kamieniowi najkosztowniejszemu, jako kamieniowi jaspisowi, na kształt kryształu przezroczystemu;
Yerusalemu ulikuwa na utukufu wa Mungu, na uzuri wake ulikuwa kama kito cha thamani, kama jiwe la kioo safi la yaspi.
12 I mające mur wielki i wysoki, mające bram dwanaście, a na onych bramach dwanaście Aniołów i imiona napisane, które są dwanaście pokoleń synów Izraelskich.
Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye milango kumi na miwili, pamoja na malaika kumi na wawili milangoni. Juu ya milango palikuwa pameandikwa majina ya makabila kumi na mawili ya wana wa Israeli.
13 Od wschodu bramy trzy, od północy bramy trzy, od południa bramy trzy, od zachodu bramy trzy.
Upande wa mashariki palikuwa na milango mitatu, upande wa kusini milango mitatu, upande wa kaskazini milango mitatu, na upande wa magharibi milango mitatu.
14 A mur miasta miał gruntów dwanaście, a na nich dwanaście imion dwunastu Apostołów Barankowych.
Kuta za mji zilikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake palikuwa na majina kumi na mawili ya mitume kumi na wawili wa Mwana Kondoo.
15 A ten, co mówił ze mną, miał trzcinę złotą, a zmierzył miasto i bramy jego, i mur jego.
Mmoja aliyeongea nami alikuwa na kipimo cha fimbo iliyotengenezwa kwa dhahabu kwa ajili ya kupima mji, milango yake na kuta zake.
16 A położenie miasta onego jest czworograniaste, a długość jego taka jest, jako i szerokość. I pomierzył miasto ono trzciną na dwanaście tysięcy stajan; a długość i szerokość i wysokość jego równe są.
Mji uliwekwa ndani ya mraba; urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Alipima mji kwa kipimio cha fimbo, stadia 12, 000 kwa urefu (urefu wake, upana, na kimo vilifanana).
17 I zmierzył mur jego na sto czterdzieści cztery łokcie miary człowieczej, która jest miara Aniołowa.
Vilevile alipima ukuta wake, unene wake ulikuwa dhiraa 144 kwa vipimo vya kibinadamu (ambavyo pia ni vipimo vya malaika).
18 A było budowanie muru jego z jaspisu; a samo miasto było złoto czyste, podobne szkłu czystemu.
Ukuta ulikuwa umejengwa kwa yaspi na mji wenye dhahabu safi, kama kioo safi.
19 A grunty muru miasta ozdobione były wszelkim kamieniem drogim. Pierwszy grunt był jaspis, wtóry szafir, trzeci chalcedon, czwarty szmaragd.
Misingi ya ukuta ilikuwa imepambwa na kila aina ya jiwe la thamani. La kwanza lilikuwa yaspi, la pili lilikuwa yakuti samawi, la tatu lilikuwa kalkedon, la nne zumaridi,
20 Piąty sardoniks, szósty sardyjusz, siódmy chrysolit, ósmy beryllus, dziewiąty topazyjusz, dziesiąty chrysopras, jedenasty hijacynt, dwunasty ametyst.
la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolitho, la nane zabarajadi, la tisa yakuti ya manjano, la kumi krisopraso, la kumi na moja hiakintho, la kumi na mbili amethisto.
21 A dwanaście bram jest dwanaście pereł: a każda brama była z jednej perły, a rynek miasta złoto czyste jako szkło przezroczyste.
Milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili, kila mlango ulitengenezwa kutoka kwenye lulu moja. Mitaa ya mji ilikuwa dhahabu safi, ikionekana kama kioo safi.
22 Alem kościoła nie widział w niem; albowiem Pan, Bóg wszechmogący, jest kościołem jego, i Baranek.
Sikuona hekalu lolote ndani ya mji, kwa kuwa Bwana Mungu, ambaye anatawala juu ya vyote, na Mwana Kondoo ni hekalu lake.
23 A nie potrzebuje to miasto słońca ani księżyca, aby świeciły w niem; albowiem chwała Boża oświeciła je, a świecą jego jest Baranek.
Mji haukuhitaji jua au mwezi ili kungaza juu yake kwa sababu utukufu wa Mungu uliangaza juu yake, na taa yake ni Mwana Kondoo.
24 A narody, które będą zbawione, będą chodziły w świetle jego, a królowie ziemscy chwałę i cześć swoję do niego przyniosą.
Mataifa watatembea kwa mwanga wa mji huo. Wafalme wa dunia wataleta fahari zao ndani yake.
25 A bramy jego nie będą zamknięte we dnie; albowiem tam nocy nie będzie.
Milango yake haitafungwa wakati wa mchana, na hapatakuwa na usiku pale.
26 I wniosą do niego chwałę i cześć narodów.
Wataleta fahari na heshima ya mataifa ndani yake,
27 I nie wnijdzie do niego nic nieczystego i czyniącego obrzydliwość i kłamstwo, tylko ci, którzy są napisani w księgach żywota Barankowych.
na hakuna kichafu kitakachoingia ndani yake. Wala yeyote ambaye afanyaye jambo lolote la aibu au udanganyifu hataingia, bali ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana Kondoo.

< Objawienie 21 >