< Psalmów 149 >

1 Halleluja. Śpiewajcie Panu pieśń nową; chwała jego niechaj zabrzmi w zgromadzeniu świętych.
Msifuni Bwana. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 Wesel się, Izraelu! w Twórcy swoim; synowie Syońscy! radujcie się w królu swoim.
Israeli na washangilie katika Muumba wao, watu wa Sayuni na wafurahi katika Mfalme wao.
3 Chwalcie imię jego na piszczałkach; na bębnie i na harfie grajcie mu.
Na walisifu jina lake kwa kucheza na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 Albowiem się kocha Pan w ludu swym; pokornych zbawieniem uwielbia.
Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake, anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 Radować się będą święci w chwale Bożej, a śpiewać będą w pokojach swych.
Watakatifu washangilie katika heshima hii, na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 Wysławiania Boże będą w ustach ich, a miecz na obie strony ostry w rękach ich,
Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 Aby wykonywali pomstę nad poganami, a karali narody;
ili walipize mataifa kisasi na adhabu juu ya mataifa,
8 Aby wiązali pętami królów ich, a szlachtę ich okowami żelaznemi;
wawafunge wafalme wao kwa minyororo, wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 Aby postąpili z nimi według prawa zapisanego. Tać jest sława wszystkich świętych jego. Halleluja.
ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao. Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote. Msifuni Bwana.

< Psalmów 149 >