< Przysłów 26 >

1 Jako śnieg w lecie, i jako deszcz we żniwa; tak głupiemu nie przystoi chwała.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 Jako się ptak tam i sam tuła, i jako jaskółka lata: tak przeklęstwo niezasłużone nie przyjdzie.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Bicz na konia, ogłów na osła, a kij potrzebny jest na grzbiet głupiego.
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 Nie odpowiadaj głupiemu według głupstwa jego, abyś mu i ty nie był podobny.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 Odpowiedz głupiemu według głupstwa jego, aby się sobie nie zdał być mądrym.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Jakoby nogi obciął, tak się bezprawia dopuszcza, kto się głupiemu poselstwa powierza.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Jako nierówne są golenie u chromego: tak jest powieść w ustach głupich.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Jako kiedy kto przywiązuje kamień drogi do procy: tak czyni ten, który uczciwość głupiemu wyrządza.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Jako ciernie, gdy się dostaną w rękę pijanego: tak przypowieść jest w ustach głupich.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Wielki Pan stworzył wszystko, a daje zapłatę głupiemu, daje także zapłatę przestępcom.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Jako pies wraca się do zwrócenia swego: tak głupi powtarza głupstwo swoje.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 Ujrzyszli człowieka, co się sobie zda być mądrym, nadzieja o głupim lepsza jest, niżeli o nim.
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Leniwy mówi: lew na drodze, lew na ulicach.
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 Jako się drzwi obracają na zawiasach swoich: tak leniwiec na łóżku swojem.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Leniwiec rękę kryje do zanadrzy swych, a ciężko mu jej podnosić do ust swoich.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Leniwiec zda się sobie być mędrszym, niżeli siedm odpowiadających z rozsądkiem.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Jakoby też psa za uszy łapał, kto się mimo idąc w cudzą zwadę wdaje.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Jako szalony wypuszcza iskry i strzały śmiertelne:
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 Tak jest każdy, który podchodzi przyjaciela swego, a mówi: Azam ja nie żartował?
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Gdy niestaje drew, gaśnie ogień; tak gdy nie będzie klatecznika, ucichnie zwada.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Jako węgiel martwy służy do rozniecenia, i drwa do ognia; tak człowiek swarliwy do rozniecenia zwady.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Słowa obmówcy są jako słowa zranionych; a wszakże przenikają do wnętrzności żywota.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 Wargi nieprzyjacielskie i serce złe są jako srebrna piana, którą polewają naczynie gliniane.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 Ten, co kogo nienawidzi, za inszego się udaje wargami swemi; ale w sercu swojem myśli o zdradzie.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Gdyć się ochotnym mową swą ukazuje, nie wierz mu: bo siedmioraka obrzydliwość jest w sercu jego.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Nienawiść zdradliwie bywa pokryta; ale odkryta bywa złość jej w zgromadzeniu.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Kto drugiemu dół kopie, wpada weń; a kto kamień toczy, na niego się obraca.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 Człowiek języka kłamliwego ma utrapienie w nienawiści, a usta łagodne przywodzą do upadku.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Przysłów 26 >