< Przysłów 20 >

1 Wino czyni pośmiewcę, a napój mocny zwajcę; przetoż każdy, co się w nim kocha, nie bywa mądrym.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 Strach królewski jest jako, ryk lwięcia; kto go rozgniewa, grzeszy przeciwko duszy swojej.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 Uczciwa rzecz każdemu, poprzestać zwady; ale głupim jest, co się w nią wdaje.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 Dla zimna leniwy nie orze; przetoż żebrać będzie we żniwa, ale nic nie otrzyma.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Rada w sercu męża jest jako woda głęboka: jednak mąż rozumny naczerpnie jej.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Większa część ludzi przechwala się uczynnością swoją; ale w samej rzeczy, któż takiego znajdzie?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 Sprawiedliwy chodzi w uprzejmości swojej; błogosławieni synowie jego po nim.
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 Król siedząc na stolicy sądowej rozgania oczyma swemi wszystko złe.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 Któż rzecze: Oczyściłem serce moje? czystym jest od grzechu mego?
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Dwojaki gwicht i dwojaka miara, to oboje obrzydliwością jest Panu.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Po zabawach swych poznane bywa i dziecię, jeźli czysty i prawy uczynek jego.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 Ucho, które słyszy, i oko, które widzi, Pan to oboje uczynił.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 Nie kochaj się w spaniu, byś snać nie zubożał, otwórz oczy swoje, a nasycisz się chlebem.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 Złe to, złe to, mówi ten, co kupuje, a odszedłszy, ali się chlubi.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Wargi umiejętne są jako złoto i obfitość pereł, i kosztowne klejnoty.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Weźmij szatę tego, któryć ręczył za obcego; a od tego, który ręczył za cudzoziemkę, weźmij zastaw jego.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Smaczny jest drugiemu chleb kłamstwa; ale potem piaskiem napełnione będą usta jego.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Myśli radami utwierdzaj, a wojnę prowadź opatrznie.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 Kto objawia tajemnicę, zdradliwie się obchodzi; przetoż z tymy, którzy pochlebiają wargami swemi, nie miej towarzystwa.
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Kto złorzeczy ojcu swemu albo matce swojej, zgaśnie pochodnia jego w gęstych ciemnościach.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 Dziedzictwu prędko z początku nabytemu naostatek błogosławić nie będą.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 Nie mów: Oddam złem. Oczekuj na Pana, a wybawi cię.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Obrzydliwością Panu dwojaki gwicht, a szale fałszywe nie podobają mu się.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 Od Pana bywają sprawowane drogi męża; ale człowiek jakoż zrozumie drogę jego?
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 Pożreć rzecz poświęconą, jest człowiekowi sidłem; a poślubiwszy co, tego zaś szukać, jakoby tego ujść.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 Król mądry rozprasza niezbożnych, i przywodzi na nich pomstę.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 Dusza ludzka jest pochodnią Pańską, która doświadcza wszystkich skrytości wnętrznych.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Miłosierdzie i prawda króla strzegą, a stolica jego miłosierdziem wsparta bywa.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 Ozdoba młodzieńców jest siła ich, a sędziwość poczciwością starców.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 Złemu są lekarstwem siności ran, i razy przenikające do wnętrzności żywota jego.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.

< Przysłów 20 >