< Filipian 1 >

1 Paweł i Tymoteusz, słudzy Jezusa Chrystusa, wszystkim świętym w Chrystusie Jezusie, którzy są w mieście Filipis, z biskupami i z dyjakonami.
Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
2 Łaska wam i pokój niech będzie od Boga, Ojca naszego, i od Pana Jezusa Chrystusa.
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
3 Dziękuję Bogu memu, ilekroć na was wspominam,
Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
4 (Zawsze w każdej modlitwie mojej za wszystkich was z radością prośbę czyniąc).
Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
5 Za społeczność waszę w Ewangielii, od pierwszego dnia aż dotąd;
kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
6 Pewien tego będąc, iż ten, który począł w was dobrą sprawę, dokona aż do dnia Jezusa Chrystusa.
Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
7 Jakoż sprwiedliwa jest, abym ja to rozumiał o was wszystkich, dlatego iż was mam w sercu mojem i w więzieniu mojem, i w obronie, i w utwierdzeniu Ewangielii, was, mówię, wszystkich, którzy jesteście ze mną uczestnikami łaski.
Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
8 Albowiem świadkiem mi jest Bóg, jako was wszystkich pragnę we wnętrznościach Jezusa Chrystusa.
Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
9 I o to się modlę, aby miłość wasza im dalej tem więcej pomnażała się w znajomości i we wszelkim zmyśle,
Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
10 Abyście mogli rozeznać rzeczy różne, żebyście byli szczerymi i bez obrażenia na dzień Chrystusowy,
ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
11 Będąc napełnieni owocami sprawiedliwości, które przynosicie przez Jezusa Chrystusa ku sławie i chwale Bożej.
mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
12 A chcę, bracia! abyście wiedzieli, iż to, co się ze mną dzieje, na większe pomnożenie Ewangielii wyszło.
Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
13 Tak iż związki moje dla Chrystusa rozgłoszone są po wszystkim pałacu cesarskim i u wszystkich inszych.
Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
14 A wiele ich z braci w Panu serca nabywszy z moich związek, śmielszymi są, bez bojaźni mówić słowo.
Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
15 Wszakże niektórzy z zazdrości i z sporu, a niektórzy też z dobrej woli Chrystusa każą.
Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
16 A ci, którzy z sporu Chrystusa opowiadają nieszczerze, mniemają, iż przydawają ucisku związkom moim;
Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
17 A którzy z miłości, wiedzą, żem jest wystawiony ku obronie Ewangielii,
Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
18 Ale cóż na tem? Owszem jakimkolwiek sposobem, lub postawnie, lub w prawdzie Chrystus bywa opowiadany, i z tego się raduję, i jeszcze się radować będę;
Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
19 Gdyż wiem, iż mi to wynijdzie na zbawienie przez modlitwę waszę i pomoc Ducha Jezusa Chrystusa,
kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
20 Według troskliwego oczekiwania i nadziei mojej, iż się w niczem nie zawstydzę; ale z wszelakiem bezpieczeństwem, jako zawsze, tak i teraz, uwielbionym będzie Chrystus w ciele mojem, lub przez żywot, lub przez śmierć.
Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
21 Albowiem mnie życiem jest Chrystus, a umrzeć zysk.
Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
22 A jeźliż żyć w ciele jest mi to owocem pracy mojej, jednak nie wiem, co bym obrać miał.
Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
23 Albowiem jestem ściśniony od tego obojga, pragnąc być rozwiązany, a być z Chrystusem, bo to daleko lepiej:
Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
24 Ale zostać w ciele potrzebniej jest dla was.
Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
25 A będąc tego pewien, wiem, iż zostanę i z wami wszystkimi pomieszkam ku waszemu pomnożeniu i weselu wiary,
Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
26 Aby obfitowała chluba wasza w Chrystusie Jezusie ze mnie, gdy do was zasię przybędę.
Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
27 Tylko się tak sprawujcie, jako przystoi Ewangielii Chrystusowej, abym, lub przyjdę i oglądam was, lub nie przyjdę, słyszał o was, iż stoicie w jednym duchu, jednomyślnie bojując w wierze Ewangielii.
Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
28 Ani w czem nie strachając się przeciwników, co onym jest pewnym znakiem zginienia, a wam zbawienia, a to od Boga;
wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
29 Gdyż wam to dane dla Chrystusa, abyście nie tylko weń wierzyli, ale abyście też dla niego cierpieli,
Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
30 Tenże bój mając, jakiście widzieli we mnie, i jaki teraz o mnie słyszycie.
kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.

< Filipian 1 >