< Liczb 28 >

1 I rzekł Pan do Mojżesza mówiąc:
Bwana akamwambia Mose,
2 Rozkaż synom Izraelskim, a powiedz im: Ofiary mojej chleba mego, w ofiarach moich ognistych, na wdzięczność wonności mojej, przestrzegać będziecie, abyście mi je ofiarowali czasu swego.
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 I rzeczesz do nich: Tać jest ofiara ognista, którą ofiarować będziecie Panu: Baranki roczne zupełne dwa na każdy dzień, na całopalenie ustawiczne;
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 Baranka jednego ofiarować będziesz poranku, a baranka drugiego ofiarować będziesz między dwoma wieczorami.
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 Do tego dziesiątą część efy mąki pszennej na ofiarę śniedną, nagniatanej z oliwą czystą z czwartą częścią hynu.
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 Toć jest całopalenie ustawiczne, jakie było sprawowane na górze Synaj na wdzięczną wonność; ognista to ofiara Panu.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 A ofiara jej mokra będzie czwarta część hynu do każdego baranka; w świątnicy sprawować będziesz ofiarę mokrą z mocnego napoju Panu.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 A drugiego baranka ofiarować będziesz między dwoma wieczorami; jako ofiarę śniedną poranną, i jako ofiarę mokrą jej ofiarować będziesz na ofiarę ognistą ku wdzięcznej wonności Panu.
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 Ale w dzień sabatu ofiarować będziesz dwa baranki roczne zupełne, i dwie dziesiąte części efy mąki pszennej z oliwą nagniecionej na ofiarę śniedną i z mokrą jej ofiarą.
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 Toć jest całopalenie sobotnie w każdy sabat, oprócz całopalenia ustawicznego i mokrej ofiary jego.
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 A na nowiu miesiąców waszych ofiarować będziecie całopalenie Panu, cielców młodych dwa, i barana jednego, baranków rocznych siedem;
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 I trzy dziesiąte efy mąki pszennej nagniecionej z oliwą na ofiarę śniedną do każdego cielca, i dwie dziesiąte części pszennej mąki zagniecionej z oliwą na ofiarę śniedną do każdego barana;
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 A jedną dziesiątą część mąki pszennej zagniecionej z oliwą na ofiarę śniedną do każdego baranka, na całopalenie ku wdzięczności wonności na ofiarę ognistą Panu.
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 Także mokre ich ofiary z wina pół hynu będzie dla każdego cielca, a trzecia część hynu do barana, czwarta zaś część hynu do każdego baranka; toć jest całopalenie na nowiu miesiąca, każdego miesiąca przez rok.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 Kozła też jednego z stada za grzech ofiarować będziecie Panu oprócz ustawicznego całopalenia, i mokrej ofiary jego.
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 Ale miesiąca pierwszego w dzień czternasty tegoż miesiąca, święto przejścia będzie Panu.
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 A w piętnasty dzień tegoż miesiąca uroczyste święto będzie; przez siedem dni chleby przaśne jeść będziecie.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 Pierwszego dnia zgromadzenie święte; żadnej roboty służebniczej nie będziecie czynić weń.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 Ale ofiarować będziecie ofiarę ognistą na całopalenie Panu: dwóch cielców młodych, i barana jednego, i siedem baranków rocznych; zupełni niech wam będą.
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 A na ofiarę ich śniedną pszennej mąki nagniecionej z oliwą trzy dziesiąte części efy do każdego cielca, a dwie dziesiąte części do każdego barana ofiarować będziecie.
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
21 Jedną dziesiątą część ofiarować będziesz przy każdym baranku z onych siedmiu baranków;
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 Kozła też jednego na ofiarę za grzech ku oczyszczeniu was.
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 Nad całopalenie poranne, które ma być całopalenie ustawiczne, ofiarować to będziecie,
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 Tak ofiarować będziecie każdego dnia przez onych siedem dni pokarm ofiary ognistej na wdzięczną wonność Panu, oprócz całopalenia ustawicznego, i mokrej ofiary jego.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 A dnia siódmego święte zgromadzenie mieć będziecie; żadnej roboty służebniczej nie będziecie czynić.
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 W dzień zaś pierwocin; gdy będziecie ofiarowali nową śniedną ofiarę Panu, gdy się wypełnią tygodnie wasze, zgromadzenie święte mieć będziecie; żadnej roboty służebniczej czynić nie będziecie.
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 I ofiarować będziecie całopalenie ku wdzięczności wonności Panu: dwóch cielców młodych, barana jednego, siedem baranków rocznych.
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 A na ofiarę śniedną ich mąki pszennej nagniecionej z oliwą trzy dziesiąte części efy do każdego cielca, dwie dziesiąte części do każdego barana.
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
29 Jedną dziesiątą część do każdego baranka z onych siedmiu baranków.
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 Kozła jednego z kóz na oczyszczenie was.
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 Oprócz całopalenia ustawicznego i ofiary śniednej jego ofiarować to będziecie; te rzeczy zupełne niech wam będą, i z mokremi ofiarami ich.
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

< Liczb 28 >