< Nehemiasza 8 >

1 Zebrał się tedy wszystek lud jednostajnie na ulicę, która jest przed bramą wodną, i rzekli do Ezdrasza, nauczonego w Piśmie, aby przyniósł księgi zakonu Mojżeszowego, który był przykazał Pan Izraelowi.
watu wote wakakusanyika kama mtu mmoja kwenye uwanja mbele ya Lango la Maji. Wakamwambia Ezra mwandishi alete Kitabu cha Sheria ya Mose, ambacho Bwana aliamuru kwa ajili ya Israeli.
2 Tedy przyniósł Ezdrasz kapłan zakon przed ono zgromadzenie mężów i niewiast, i wszystkich, którzyby rozumnie słuchać mogli; a działo się to dnia pierwszego, miesiąca siódmego.
Basi katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba, kuhani Ezra akaleta Sheria mbele ya kusanyiko, ambamo walikuwamo wanaume, wanawake na watu wote walioweza kufahamu.
3 I czytał w nim na onej ulicy, która jest przed bramą wodną, od poranku aż do południa przed mężami i niewiastami, i którzy zrozumieć mogli, a uszy wszystkiego ludu obrócone były do ksiąg zakonu.
Akaisoma kwa sauti kubwa tangu mapambazuko mpaka adhuhuri, akiwa ameuelekea uwanja uliokuwa mbele ya Lango la Maji mbele ya wanaume, wanawake na wengine ambao waliweza kufahamu. Watu wote wakasikiliza kwa makini kile Kitabu cha Sheria.
4 I stanął Ezdrasz nauczony w Piśmie na kazalnicy, którą byli zgotowali na to, a podle niego stał Matytyjasz, i Sema, i Ananijasz, i Uryjasz, i Helkijasz, i Maasyjasz, po prawej ręce jego, a po lewej ręce jego Fedajasz, i Misael, i Malchyjasz, i Chasum, i Chasbadana, Zacharyjasz i Mesullam.
Mwandishi Ezra alikuwa amesimama juu ya jukwaa la miti lililojengwa kwa kusudi hilo. Karibu naye upande wa kuume alisimama Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya. Upande wake wa kushoto walikuwepo Pedaya, Mishaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu.
5 Otworzył tedy Ezdrasz księgi przed oczyma wszystkiego ludu, bo stał wyżej niż wszystek lud; a gdy je otworzył, wszystek lud powstał.
Ezra akakifungua kile kitabu. Watu wote waliweza kumwona kwa sababu alikuwa amesimama juu zaidi, naye alipokifungua watu wote wakasimama.
6 I błogosławił Ezdrasz Panu, Bogu wielkiemu, a wszystek lud odpowiadał: Amen! Amen! podnosząc ręce swoje; a nachyliwszy głowy, kłaniali się Panu twrzą ku ziemi.
Ezra akamsifu Bwana, Mungu mkuu, nao watu wote wakainua mikono yao na kuitikia, “Amen! Amen!” Kisha wakasujudu na kumwabudu Bwana hali nyuso zao zikigusa ardhi.
7 Także i Jesua, i Bani, i Serebijasz, Jamin, Chakub, Sabbetaj, Hodyjasz, Maasyjasz, Kielita, Azaryjasz, Jozabad, Chanan, Felajasz, i Lewitowie nauczali ludu zakonu, a lud stał na miejscu swem.
Watu wakiwa wamesimama pale, Walawi wafuatao waliwafunza ile Sheria: Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi, Hanani na Pelaya.
8 Bo czytali w księgach zakonu Bożego wyraźnie, a wykładając zmysł objaśniali to, co czytali.
Walisoma kutoka kile Kitabu cha Sheria ya Mungu, wakiifafanua na kuwapa maelezo ili watu waweze kufahamu kile kilichokuwa kikisomwa.
9 Zatem Nehemijasz (ten jest Tyrsata) i Ezdrasz kapłan, nauczony w Piśmie, i Lewitowie, którzy uczyli lud, rzekli do wszystkiego ludu: Ten dzień poświęcony jest Panu, Bogu waszemu, nie smućcież się, ani płaczcie. (Bo płakał wszystek lud, słysząc słowa zakonu.)
Ndipo Nehemia aliyekuwa mtawala, Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliokuwa wakiwafundisha watu wakawaambia wote, “Siku hii ni takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msiomboleze wala msilie.” Kwa kuwa watu wote walikuwa wakilia walipokuwa wakisikiliza maneno ya ile Sheria.
10 I rzekł im: Idźcież, jedzcie rzeczy tłuste a pijcie napój słodki, a posyłajcie cząstki tym, którzy sobie nic nie nagotowali; albowiem święty jest dzień Panu naszemu. Przetoż się nie frasujcie; albowiem wesele Pańskie jest siłą waszą,
Nehemia akasema, “Nendeni mkafurahie chakula kizuri na vinywaji vitamu, na mpeleke sehemu kwa wale ambao hawana chochote cha kula. Siku hii ni takatifu kwa Bwana. Msihuzunike, kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”
11 A gdy Lewitowie uczynili milczenie między wszystkim ludem, mówiąc: Milczcież, bo dzień święty jest, a nie smućcie się:
Walawi wakawatuliza watu wote wakisema, “Kuweni watulivu, kwa kuwa hii ni siku takatifu. Msihuzunike.”
12 Tedy odszedł wszystek lud, aby jedli i pili, i aby innym cząstki posyłali. I weselili się bardzo, przeto, że zrozumieli słowa, których i nauczano.
Kisha watu wote wakaondoka kwenda kula na kunywa, na kupeana sehemu ya chakula, na wakaadhimisha kwa furaha kubwa, kwa sababu sasa walifahamu maneno yale waliyokuwa wameelezwa.
13 Potem zebrali się dnia drugiego przedniejsi domów ojcowskich ze wszystkiego ludu, kapłani i Lewitowie, do Ezdrasza nauczonego w Piśmie, aby wyrozumieli słowa zakonu.
Katika siku ya pili ya mwezi, wakuu wa mbari zote, pamoja na makuhani na Walawi, walikusanyika wakimzunguka Ezra mwandishi ili wapate kusikiliza kwa makini maneno ya Sheria.
14 I znaleźli napisane w zakonie, że rozkazał Pan przez Mojżesza, aby mieszkali synowie Izraelscy w kuczkach w święto uroczyste miesiąca siódmego;
Wakakuta imeandikwa katika ile Sheria, ambayo Bwana aliiamuru kupitia kwa Mose, kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda wakati wa sikukuu ya mwezi wa saba,
15 A iżby to opowiedziano i obwołano we wszystkich miastach ich, i w Jeruzalemie, mówiąc: Wynijdźcie na górę, a nanoście gałęzia oliwnego, i gałęzia sosnowego, i gałęzia myrtowego, i gałęzia palmowego, i gałęzia drzewa gęstego, abyście poczynili kuczki, jako jest napisane.
na kwamba walipaswa kutangaza neno hili na kulieneza katika miji yao na katika Yerusalemu wakisema: “Enendeni katika nchi ya mlima na kuleta matawi kutoka miti ya mizeituni, mizeituni mwitu, mihadasi, mitende na miti ya kivuli, ili kutengeneza vibanda,” kama ilivyoandikwa.
16 Przetoż wyszedł lud, a nanosili i poczynili sobie kuczki, każdy na dachu swym, i w sieniach swych, i w sieniach domu Bożego, i na ulicy bramy wodnej, i na ulicy bramy Efraimowej.
Basi watu wakaenda na kuleta matawi, nao wakajijengea vibanda juu ya paa za nyumba zao, katika nyua zao, katika nyua za nyumba ya Mungu, na katika uwanja karibu na Lango la Maji na uwanja wa Lango la Efraimu.
17 A tak naczyniło kuczek wszystko zgromadzenie, które się wróciło z niewoli, i mieszkali w kuczkach, (choć tego nie czynili synowie Izraelscy ode dni Jozuego, syna Nunowego, aż do dnia onego; ) i było wesele bardzo wielkie.
Jamii yote ya watu waliorudi kutoka utumwani wakajenga vibanda na kuishi ndani yake. Tangu wakati wa Yoshua mwana wa Nuni mpaka siku ile, Waisraeli hawakuwahi kuiadhimisha namna hii. Furaha yao ilikuwa kubwa sana.
18 A Ezdrasz czytał w księgach zakonu Bożego na każdy dzień; od pierwszego dnia aż do dnia ostatniego; i obchodzili święto uroczyste przez siedm dni, a dnia ósmego było zgromadzenie według zwyczaju.
Siku baada ya siku, kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho, Ezra alisoma kutoka kwenye kile Kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakaiadhimisha sikukuu ile kwa siku saba, nayo siku ya nane, kufuatana na maagizo, kulikuwa na kusanyiko maalum.

< Nehemiasza 8 >