< Nehemiasza 3 >

1 Potem powstał Elijasyb, kapłan najwyższy, i bracia jego kapłani, i budowali bramę owczą. I zbudowali ją, i przyprawili wrota do niej; aż do wieży Mea zbudowali ją, i aż do wieży Chananeel.
Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
2 A podle niego budowali mężowie z Jerycha, a podle nich budował Zachur, syn Immrego.
Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
3 A bramę rybną budowali synowie Senaa, którzy ją też przykryli i przyprawili wrota do niej, i zamki jej, i zawory jej.
Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
4 A podle nich poprawiał Meremot, syn Uryjasza, syna Kosowego; a podle nich poprawiał Mesullam, syn Barachyjaszowy, syna Mesezabelowego; a podle nich poprawiał Sadok, syn Baany.
Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
5 Podle nich zasię poprawiali Tekuitczycy; ale ci, co byli zacniejsi z nich, nie podłożyli szyi swej pod robotę pana swego.
Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
6 A bramę starą poprawiali Jojada, syn Faseachowy, i Mesullam, syn Besodyjaszowy; ci ją przykryli, i przyprawili wrota do niej, i zamki jej, i zawory jej.
Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
7 A podle nich poprawiał Melatyjasz Gabaonitczyk, Jadon Meronitczyk, mężowie z Gabaon i z Masfa, aż do stolicy książęcej, z tej strony rzeki.
Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
8 Podle nich poprawiał Husyjel, syn Charchajaszowy, z złotnikami; a podle niego poprawiał Chananijasz, syn aptekarski; a Jeruzalemu zaniechali aż do muru szerokiego.
Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
9 A podle nich poprawiał Rafajasz, syn Churowy, przełożony nad połową powiatu Jeruzalemskiego.
Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
10 A podle nich poprawiał Jedajasz, syn Harumafowy, i przeciw swemu domowi; a podle niego poprawiał Hattus, syn Hasbonijaszowy.
Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
11 Części zaś drugiej poprawiał Malchyjasz, syn Harymowy, i Hasub, syn Pachatmoabowy, także i wieżę Tannurym.
Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
12 A podle niego poprawiał Sallum, syn Hallochesowy, przełożony nad połową powiatu Jeruzalemskiego, sam i córki jego.
Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
13 Bramy nad doliną poprawiał Chanun, i obywatele Zanoe; cić ją budowali, i przyprawili wrota do niej, zamki jej, i zawory jej; i na tysiąc łokci muru aż do bramy gnojowej.
Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
14 Bramy zaś gnojowej poprawiał Melchyjasz, syn Rechaby, przełożony nad powiatem Betcherem; tenci ją zbudował, i przyprawił wrota do niej, zamki jej, i zawory jej,
Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
15 Dotego bramy żródła poprawiał Sallon, syn Cholhozowy, przełożony nad powiatem Masfa; a ten ją zbudował, i przykrył ją, i przyprawił wrota do niej, i zamki jej, i zawory jej, i mur nad stawem Selach ku ogrodowi królewskiemu aż do schodu, po którym schodzą z miasta Dawidowego.
Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
16 Zatem poprawiał Nehemijasz, syn Hasbuka, przełożony nad połową powiatu Betsur, aż przeciwko grobom Dawidowym i aż do stawu urobionego, i aż do domu mocarzów.
Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
17 Za nim poprawiali Lewitowie Rehum, syn Bani; podle niego poprawiał Hasabijasz, przełożony nad połową powiatu Ceile z powiatem swoim.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
18 Za nim zasię poprawiali bracia ich, Bawaj, syn Chenadadowy, przełożony nad połową powiatu Ceile.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
19 A podle niego poprawiał Eser, syn Jesui, przełożony nad Masfą, części drugiej przeciw miejscu, kędy chodzą do zbrojowni nazwanej Mikzoa.
Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
20 Po nim wzruszony gorliwością poprawiał Baruch, syn Zabbajowy, części drugiej od Mikzoa aż do drzwi domu Elijasyba, najwyższego kapłana.
Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
21 Za nim poprawiał Meremot, syn Uryjasza, syn Kosowego, części drugiej, ode drzwi domu Elijasybowego aż do końca domu jego.
Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
22 A za nim poprawiali kapłani, którzy mieszkali w równinie.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
23 Za nimi poprawiał Benjamin i Hasub, przeciw domom swoim; za nimi poprawiał Azaryjasz, syn Maasejasza, syna Ananijaszowego, podle domu swego.
Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
24 Za nim poprawiał Bennui, syn Chenadadowy, części drugiej od domu Azaryjaszowego aż do Mikzoa, i aż do rogu.
Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
25 Palal, syn Uzajego przeciw Mikzoa, i wieży wysokiej, wywiedzionej z domu królewskiego, która była w sieni więzienia; po nim poprawiał Fadajasz, syn Farosowy.
Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
26 A Netynejczycy, co mieszkali w Ofel, poprawiali aż na przeciwko bramie wodnej na wschód słońca, i wieży wysokiej.
na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
27 Za nimi poprawiali Tekuitczykowie drugą część przeciw wieży wielkiej i wysokiej aż do muru Ofel.
Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
28 Od bramy końskiej poprawiali kapłani, każdy przeciw domowi swemu.
Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
29 Za nimi poprawiał Sadok, syn Immerowy, przeciw domowi swemu, a za nim poprawiał Semejasz, syn Sechenijaszowy, stróż barmy wschodniej.
Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
30 Za nim poprawiał Chananijasz, syn Selemijaszowy, i Chanun, syn Salafowy szósty, części drugiej; za nim poprawiał Mesullam, syn Berechyjaszowy, przeciw gmachowi swemu.
Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
31 Za nim poprawiał Malchijasz, syn złotniczy, aż do domu Netynejczyków, i kupców, przeciw bramie sądowej, i aż do sali narożnej.
Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
32 A między salą narożną aż do bramy owczej poprawiali złotnicy i kupcy.
Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.

< Nehemiasza 3 >