< Micheasza 7 >
1 Biada mnie! żem jako ostatki po sprzątanieniu owoców letnich, jako pozostałe grona po zbieraniu wina; niemasz grona ku zjedzeniu, pierwocin z owocu pragnie dusza moja.
Taabu gani hii niliyo nayo! Nimefanana na yule akusanyaye matunda ya kiangazi, aokotaye masazo baada ya kuvunwa shamba la mizabibu; hakuna kishada chenye matunda ya kula, hakuna hata ile tini ya mwanzoni ninayoitamani.
2 Pobożny z ziemi zginął, a szczerego niemasz między ludźmi; wszyscy zgoła o wylaniu krwi myślą, każdy łowi siecią brata swego.
Wanaomcha Mungu wameondolewa kutoka nchi; hakuna mtu mnyofu hata mmoja aliyebaki. Watu wote wanavizia kumwaga damu, kila mmoja anamwinda ndugu yake kwa wavu.
3 Co złego robią rękoma, chcą, aby to za dobre uszło; książę podatków żąda, a sędzia z datku sądzi, a kto możny jest, ten mówi przewrotność duszy swojej, i w gromadę ją plotą.
Mikono yote miwili ni hodari katika kufanya ubaya, mtawala anadai zawadi, hakimu anapokea rushwa, wenye nguvu wanaamuru wanachotaka: wote wanafanya shauri baya pamoja.
4 Najlepszy z nich jest jako oset, najszczerszy przechodzi ciernie; dzień stróżów twoich i nawiedzenia twego przychodzi; już nastanie powikłanie ich.
Aliye mwema kupita wote kati yao ni kama mchongoma, anayeonekana mnyofu zaidi miongoni mwao ni mbaya kuliko uzio wa miiba. Siku ya walinzi wako imewadia, siku atakayokutembelea Mungu. Sasa ni wakati wao wa kuchanganyikiwa.
5 Nie wierzcie przyjacielowi, ani ufajcie wodzowi; przed tą, która leży na łonie twojem, strzeż drzwi ust swoich.
Usimtumaini jirani; usiweke matumaini kwa rafiki. Hata kwa yule alalaye kifuani mwako uwe mwangalifu kwa maneno yako.
6 Bo syn lekce waży ojca, a córka powstaje przeciwko matce swej, synowa przeciwko świekrze swej, a nieprzyjaciele każdego są domownicy jego.
Kwa kuwa mwana humdharau baba yake, naye binti huinuka dhidi ya mama yake, mkwe kuwa kinyume na mama mkwe wake: adui wa mtu ni wale wa nyumbani mwake hasa.
7 Przetoż ja na Pana patrzyć będę, oczekiwać będę Boga zbawienia mego; Bóg mój wysłucha mię.
Lakini mimi, namtazama Bwana kwa matumaini, namngoja Mungu Mwokozi wangu; Mungu wangu atanisikia mimi.
8 Nie wesel się ze mnie, nieprzyjaciółko moja! jeźlim upadła, powstanę; jeźli siedzę w ciemnościach, Pan jest światłością moją.
Usifurahie msiba wangu, ee adui yangu! Ingawa nimeanguka, nitainuka. Japo ninaketi gizani, Bwana atakuwa nuru yangu.
9 Gniew Pański poniosę: bom przeciwko niemu zgrzeszył, aż się wżdy zastawi o sprawę moję, a wykona sąd mój: wywiedzie mię na światło, ujrzę sprawiedliwość jego.
Kwa sababu nimetenda dhambi dhidi yake, nitabeba ghadhabu ya Bwana, mpaka atakaponitetea shauri langu na kuithibitisha haki yangu. Atanileta nje kwenye mwanga, nami nitaiona haki yake.
10 Ujrzy to nieprzyjaciółka moja, a wstyd okryje tę, która do mnie mówi: Gdzież jest Pan, Bóg twój? Oczy moje na nią patrzyć będą, gdy jako błoto na ulicach podeptana będzie.
Kisha adui yangu ataliona naye atafunikwa na aibu, yule aliyeniambia, “Yu wapi Bwana Mungu wako?” Macho yangu yataona kuanguka kwake, hata sasa atakanyagwa chini ya mguu kama tope barabarani.
11 Dnia onego, którego pobudowane będą parkany twoje, dnia onego, mówię, daleko się wyrok rozejdzie.
Siku ya kujenga kuta zako itawadia, siku ya kupanua mipaka yako.
12 Onegoż dnia przychodzić będą do ciebie i z Assyryi aż do miast obronnych, i od miast obronnych aż do rzeki, i od morza aż do morza, i od góry aż do góry.
Siku hiyo watu watakuja kwako kutoka Ashuru na miji ya Misri, hata kutoka Misri hadi Frati na kutoka bahari hadi bahari na kutoka mlima hadi mlima.
13 Wszakże ta ziemia spustoszona będzie dla obywateli swoich, dla owocu wynalazków ich.
Dunia itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakazi wake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao.
14 Paśże lud twój laską twoją, trzodę dziedzictwa twego, która osobno mieszka w lesie i w pośród pola; niech wypasą Basan i Galaad jako za dni starodawnych.
Wachunge watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, ambalo linaishi peke yake msituni, katika nchi ya malisho yenye rutuba. Waache walishe katika Bashani na Gileadi kama ilivyokuwa siku za kale.
15 Ukażę mu dziwne rzeczy, jako za dni, którycheś wyszedł z ziemi Egipskiej.
“Kama siku zile mlipotoka Misri, nitawaonyesha maajabu yangu.”
16 Co widząc narody zawstydzą się nad wszystką mocą swoją, włożą rękę na usta, a uszy ich ogłuszeją
Mataifa yataona na kuaibika, waliondolewa nguvu zao zote. Wataweka mikono yao kwenye vinywa vyao na masikio yao yatakuwa na uziwi.
17 Proch jako wąż lizać będą, jako gadziny ziemskie ruszą się z lochów swoich, do Pana, Boga naszego, z strachem pobieżą, i bać się ciebie będą.
Wataramba mavumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya ardhi. Watatoka nje ya mapango yao wakitetemeka; watamgeukia Bwana Mungu wetu kwa hofu nao watakuogopa.
18 Któryż Bóg jest podobny tobie? Któryby nieprawość odpuszczał, i mijał przestępstwa ostatków dziedzictwa swego, któryby nie zatrzymywał na wieki gniewu swego, przeto, że się kocha w miłosierdziu.
Ni nani Mungu kama wewe, ambaye anaachilia dhambi na kusamehe makosa ya mabaki ya urithi wake? Wewe huwi na hasira milele, bali unafurahia kuonyesha rehema.
19 Nawróci się, a zmiłuje się nad nami; zatłumi nieprawości nasze i wrzuci w głębokość morską wszystkie grzechy nasze.
Utatuhurumia tena, utazikanyaga dhambi zetu chini ya nyayo zako, na kutupa maovu yetu yote katika vilindi vya bahari.
20 Pokażesz się Jakóbowi prawdomównym, a miłosiernym Abrahamowi, jakoś przysiągł ojcom naszym ode dni dawnych.
Utakuwa wa kweli kwa Yakobo, nawe utamwonyesha Abrahamu rehema, kama ulivyowaahidi kwa kiapo baba zetu siku za kale.