< Mateusza 23 >

1 Tedy Jezus rzekł do ludu i do uczniów swoich, mówiąc:
Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake:
2 Na stolicy Mojżeszowej usiedli nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie.
“Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Mose,
3 Przetoż wszystkiego, czegokolwiek by wam rozkazali przestrzegać, przestrzegajcie i czyńcie, ale według uczynków ich nie czyńcie; albowiem oni mówią, ale nie czynią.
hivyo inawapasa kuwatii na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini msifuate yale wanayotenda, kwa sababu hawatendi yale wanayohubiri.
4 Bo wiążą brzemiona ciężkie i nieznośne, i kładą je na ramiona ludzkie, lecz palcem swoim nie chcą ich ruszyć.
Wao hufunga mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata kuinua kidole ili kuisogeza.
5 A wszystkie uczynki swoje czynią, aby byli widziani od ludzi, i rozszerzają bramy swoje, i rozpuszczają podołki płaszczów swoich.
“Wao hutenda mambo yao yote ili waonekane na watu. Hupanua vikasha vyao vyenye maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya mavazi yao.
6 Nadto miłują pierwsze miejsca na wieczerzach, i pierwsze stołki w bóżnicach.
Wanapenda kukalia viti vya heshima katika karamu, na vile viti maalum sana katika masinagogi.
7 I pozdrawiania na rynkach, i aby je nazywali ludzie: Mistrzu, mistrzu!
Hupenda kusalimiwa masokoni na kutaka watu wawaite ‘Rabi.’
8 Ale wy nie nazywajcie się mistrzami; albowiem jeden jest mistrz wasz, Chrystus; ale wy jesteście wszyscy braćmi.
“Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi,’ kwa sababu mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu.
9 I nikogo nie zówcie ojcem waszym na ziemi; albowiem jeden jest Ojciec wasz, który jest w niebiesiech.
Nanyi msimwite mtu yeyote ‘Baba,’ hapa duniani, kwa maana mnaye Baba mmoja, naye yuko mbinguni.
10 A niechaj was nie zowią mistrzami, gdyż jeden jest mistrz wasz, Chrystus.
Wala msiitwe ‘Mwalimu,’ kwa maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.
11 Ale kto z was największy jest, będzie sługą waszym.
Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.
12 A kto by się wywyższał, będzie poniżony; a kto by się poniżał, będzie wywyższony.
Kwa kuwa yeyote anayejikweza atashushwa, na yeyote anayejinyenyekeza atakwezwa.
13 Lecz biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iż zamykacie królestwo niebieskie przed ludźmi; albowiem tam sami nie wchodzicie, ani tym, którzy by wnijść chcieli, wchodzić nie dopuszczacie.
“Lakini ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Kwa maana mnawafungia watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka kuingia mnawazuia. [
14 Biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iż pożeracie domy wdów, a to pod pokrywką długich modlitw, dlatego cięższy sąd odniesiecie.
Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo hukumu yenu itakuwa kuu zaidi.]
15 Biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iż obchodzicie morze i ziemię, abyście uczynili jednego nowego Żyda; a gdy się stanie, czynicie go synem zatracenia, dwakroć więcej niżeliście sami. (Geenna g1067)
“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja mwongofu, lakini baada ya kumpata, mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili kuliko ninyi! (Geenna g1067)
16 Biada wam, wodzowie ślepi! którzy powiadacie: kto by przysiągł na kościół, nic nie jest: ale kto by przysiągł na złoto kościelne, winien jest.
“Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi mwasema, ‘Mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’
17 Głupi i ślepi! albowiem cóż jest większego, złoto czy kościół, który poświęca złoto?
Ninyi vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi: ni ile dhahabu, au ni lile Hekalu linaloifanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18 A kto by przysiągł na ołtarz, nic nie jest; lecz kto by przysiągł na dar, który jest na nim, winien jest.
Pia mnasema, ‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, amefungwa kwa kiapo chake’
19 Głupi i ślepi! albowiem cóż większego jest? dar, czyli ołtarz, który poświęca dar?
Ninyi vipofu! Ni kipi kikuu zaidi: ni sadaka, au ni madhabahu yanayoifanya hiyo sadaka kuwa takatifu?
20 Kto tedy przysięga na ołtarz, przysięga na niego, i na to wszystko, co na nim jest;
Kwa hiyo, mtu aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hayo madhabahu na vitu vyote vilivyo juu yake.
21 A kto przysięga na kościół, przysięga na niego, i na tego, który w nim mieszka;
Naye mtu aapaye kwa Hekalu, huapa kwa hilo Hekalu na kwa huyo akaaye ndani yake.
22 I kto przysięga na niebo, przysięga na stolicę Bożą, i na tego, który siedzi na niej.
Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketiye juu ya kiti hicho.
23 Biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iż dawacie dziesięcinę z miętki i z anyżu i z kminu, a opuszczacie poważniejsze rzeczy w zakonie, sąd i miłosierdzie i wiarę; te rzeczy mieliście czynić, a onych nie opuszczać.
“Ole wenu walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu zaidi ya sheria, yaani haki, huruma na uaminifu. Iliwapasa kufanya haya makuu ya sheria bila kupuuza hayo matoleo.
24 Wodzowie ślepi! którzy przecedzacie komara, i wielbłąda połykacie.
Ninyi viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini mnameza ngamia!
25 Biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iż oczyszczacie kubek z wierzchu i misę, a wewnątrz pełne są drapiestwa i zbytku.
“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnasafisha kikombe na sahani kwa nje, lakini ndani mmejaa unyangʼanyi na kutokuwa na kiasi.
26 Faryzeuszu ślepy! oczyść pierwej to, co jest wewnątrz w kubku i w misie, aby i to, co jest z wierzchu, czystem było.
Ewe Farisayo kipofu! Safisha ndani ya kikombe na sahani kwanza, ndipo nje itakuwa safi pia.
27 Biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iżeście podobni grobom pobielanym, które się zdadzą z wierzchu być cudne, ale wewnątrz pełne są kości umarłych i wszelakiej nieczystości.
“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo yanapendeza kwa nje, lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu.
28 Także i wy z wierzchu zdacie się być ludziom sprawiedliwi; ale wewnątrz jesteście pełni obłudy i nieprawości.
Vivyo hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29 Biada wam, nauczeni w Piśmie i Faryzeuszowie obłudni! iż budujecie groby proroków, i zdobicie nagrobki sprawiedliwych,
“Ole wenu, walimu wa sheria na Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.
30 I mówicie: Byśmy byli za dni ojców naszych, nie bylibyśmy uczestnikami ich we krwi proroków.
Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki katika kumwaga damu ya manabii!’
31 A tak świadczycie sami przeciwko sobie, że jesteście synowie tych, którzy proroki pozabijali.
Hivyo mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.
32 I wy też dopełniacie miary ojców waszych.
Haya basi, kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu!
33 Wężowie! rodzaju jaszczurczy! i jakoż będziecie mogli ujść przed sądem ognia piekielnego? (Geenna g1067)
“Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanamu? (Geenna g1067)
34 Przetoż oto ja posyłam do was proroki, i mędrce, i nauczone w Piśmie, a z nich niektóre zabijecie i ukrzyżujecie, a niektóre z nich ubiczujecie w bóżnicach waszych, i będziecie je prześladować od miasta do miasta;
Kwa sababu hii, tazameni, natuma kwenu manabii na wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha, na wengine wao mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu na kuwafuatia kutoka mji mmoja hadi mji mwingine.
35 Aby przyszła na was wszystka krew sprawiedliwa, wylana na ziemi, ode krwi Abla sprawiedliwego aż do krwi Zacharyjasza, syna Barachyjaszowego, któregoście zabili między kościołem i ołtarzem.
Hivyo ile damu ya wenye haki wote iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya Zekaria mwana wa Barakia, mliyemuua kati ya patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu.
36 Zaprawdę powiadam wam: Przyjdzie to wszystko na ten naród.
Amin, nawaambia, haya yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
37 Jeruzalem! Jeruzalem! które zabijasz proroki, i które kamionujesz te, którzy do ciebie byli posyłani: ilekroć chciałem zgromadzić dzieci twoje, tak jako zgromadza kokosz kurczęta swoje pod skrzydła, a nie chcieliście?
“Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka!
38 Oto wam dom wasz pusty zostanie.
Tazama nyumba yenu imeachwa ukiwa.
39 Albowiem powiadam wam, że mię nie ujrzycie od tego czasu, aż rzeczecie: Błogosławiony, który idzie w imieniu Pańskiem.
Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’”

< Mateusza 23 >