< Mateusza 13 >

1 A dnia onego wyszedłszy Jezus z domu, usiadł nad morzem:
Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya nyumba, akaketi kando ya bahari.
2 I zebrał się do niego wielki lud, tak iż wstąpiwszy w łódź, siedział, a wszystek lud stał na brzegu.
Umati mkubwa mno wa watu ukakusanyika kumzunguka, hata ikabidi aingie katika chombo na kuketi humo, nao watu wote wakawa wamesimama ukingoni mwa bahari.
3 I mówił do nich wiele w podobieństwach i rzekł: Oto wyszedł rozsiewca, aby rozsiewał;
Ndipo akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
4 A gdy on rozsiewał, niektóre padło podle drogi; i przyleciały ptaki, a podziobały je.
Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
5 Drugie zasię padło na miejsce opoczyste, gdzie nie miało wiele ziemi; i wnet weszło, iż nie miało głębokości ziemi.
Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
6 Ale gdy słońce weszło, wygorzało, a iż nie miało korzenia, uschło.
Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
7 A drugie padło między ciernie, i wzrosły ciernie, a zadusiły je.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea.
8 A drugie padło na ziemię dobrą i wydało pożytek, jedno setny, drugie sześćdziesiątny, a drugie trzydziestny.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, nyingine mara sitini, na nyingine mara thelathini.
9 Kto ma uszy ku słuchaniu, niechaj słucha.
Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
10 Tedy przystąpiwszy uczniowie, rzekli mu: Dlaczegoż im w podobieństwach mówisz?
Wanafunzi wake wakamwendea, wakamuuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa mifano?”
11 A on odpowiadając, rzekł im: Wam dano wiedzieć tajemnicę królestwa niebieskiego, ale onym nie dano;
Akawajibu, “Ninyi mmepewa kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini wao hawajapewa.
12 Albowiem kto ma, będzie mu dano, i obfitować będzie, ale kto nie ma, i to, co ma, będzie od niego odjęto.
Kwa maana yule aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.
13 Dlategoć im w podobieństwach mówię, iż widząc nie widzą, i słysząc nie słyszą, ani rozumieją.
Hii ndiyo sababu nasema nao kwa mifano: “Ingawa wanatazama, hawaoni; wanasikiliza, lakini hawasikii, wala hawaelewi.
14 I pełni się w nich proroctwo Izajaszowe, które mówi: Słuchem słuchać będziecie, ale nie zrozumiecie; i widząc widzieć będziecie, ale nie ujrzycie;
Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema: “‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama lakini hamtaona.
15 Albowiem zatyło serce ludu tego, a uszyma ciężko słyszeli, i oczy swe zamrużyli, żeby kiedy oczyma nie widzieli i uszyma nie słyszeli, a sercem nie zrozumieli, i nie nawrócili się, a uzdrowiłbym je.
Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
16 Ale oczy wasze błogosławione, że widzą, i uszy wasze, że słyszą;
Lakini heri macho yenu kwa sababu yanaona, na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
17 Bo zaprawdę powiadam wam, iż wiele proroków i sprawiedliwych żądało widzieć to, co wy widzicie, ale nie widzieli, i słyszeć to, co słyszycie, ale nie słyszeli.
Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye haki walitamani kuona yale mnayoyaona lakini hawakuyaona, na walitamani kusikia yale mnayoyasikia lakini hawakuyasikia.
18 Wy tedy słuchajcie podobieństwa onego rozsiewcy.
“Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa mpanzi:
19 Gdy kto słucha słowa o tem królestwie, a nie rozumie, przychodzi on zły i porywa to, co wsiano w serce jego; tenci jest on, który podle drogi posiany jest.
Mtu yeyote anaposikia neno la Ufalme naye asilielewe, yule mwovu huja na kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake. Hii ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
20 A na opoczystych miejscach posiany, ten jest, który słucha słowa i zaraz je z radością przyjmuje;
Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na mara hulipokea kwa furaha.
21 Ale nie ma korzenia w sobie, lecz doczesny jest; a gdy przychodzi ucisk, albo prześladowanie dla słowa, wnet się gorszy.
Lakini kwa kuwa hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, yeye mara huchukizwa.
22 A między ciernie posiany, ten jest, który słucha słowa; ale pieczołowanie świata tego i omamienie bogactw zadusza słowo, i staje się bez pożytku. (aiōn g165)
Ile mbegu iliyopandwa katika miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini masumbufu ya maisha haya na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda. (aiōn g165)
23 A na dobrej ziemi posiany, jest ten, który słucha słowa i rozumie, tenci pożytek przynosi; a przynosi jeden setny, drugi sześćdziesiątny, a drugi trzydziestny.
Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na kulielewa. Naye hakika huzaa matunda, akizaa mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya mbegu iliyopandwa.”
24 Drugie podobieństwo przełożył im, mówiąc: Podobne jest królestwo niebieskie człowiekowi, rozsiewającemu dobre nasienie na roli swojej.
Yesu akawaambia mfano mwingine, akasema: “Ufalme wa Mbinguni unaweza kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake.
25 A gdy ludzie zasnęli, przyszedł nieprzyjaciel jego, i nasiał kąkolu między pszenicą, i odszedł.
Lakini wakati kila mtu alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 A gdy urosła trawa i pożytek przyniosła, tedy się pokazał i kąkol.
Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu nayo yakatokea.
27 Tedy przystąpiwszy słudzy gospodarscy, rzekli mu: Panie! izaliś dobrego nasienia nie nasiał na roli twojej? Skądże tedy ma kąkol?
“Watumishi wa yule mwenye shamba wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu yametoka wapi?’
28 A on im rzekł: Nieprzyjaciel człowiek to uczynił. I rzekli słudzy do niego: A chceszże, iż pójdziemy, a zbierzemy go?
“Akawajibu, ‘Adui ndiye alifanya jambo hili.’ “Wale watumishi wakamuuliza, ‘Je, unataka twende tukayangʼoe?’
29 A on rzekł: Nie! byście snać zbierając kąkol, nie wykorzenili zaraz z nim i pszenicy.
“Lakini akasema, ‘Hapana, msiyangʼoe, kwa maana wakati mkingʼoa magugu mnaweza mkangʼoa na ngano pamoja nayo.
30 Dopuśćcie obojgu społem rość aż do żniwa; a czasu żniwa rzekę żeńcom: Zbierzcie pierwej kąkol, a zwiążcie go w snopki ku spaleniu; ale pszenicę zgromadźcie do gumna mojego.
Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto; kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu.’”
31 Insze podobieństwo przełożył im, mówiąc: Podobne jest królestwo niebieskie ziarnu gorczycznemu, które wziąwszy człowiek, wsiał na roli swojej.
Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua, akaipanda shambani mwake.
32 Które najmniejszeć jest ze wszystkich nasion; ale kiedy urośnie, największe jest ze wszystkich jarzyn, i staje się drzewem, tak iż ptaki niebieskie przylatując, gniazda sobie czynią na gałązkach jego.
Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, hadi ndege wa angani wanakuja na kutengeneza viota katika matawi yake.”
33 Insze podobieństwo powiedział im: Podobne jest królestwo niebieskie kwasowi, który wziąwszy niewiasta, zakryła we trzy miary mąki, ażby wszystka skwaśniała.
Akawaambia mfano mwingine, “Ufalme wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo mwanamke aliichukua akaichanganya katika kiasi kikubwa cha unga mpaka wote ukaumuka.”
34 To wszystko mówił Jezus w podobieństwach do ludu, a bez podobieństwa nie mówił do nich;
Yesu alinena mambo haya yote kwa makutano kwa mifano. Wala hakuwaambia lolote pasipo mfano.
35 Aby się wypełniło, co powiedziano przez proroka mówiącego: Otworzę w podobieństwach usta moje, wypowiem skryte rzeczy od założenia świata.
Hii ilikuwa ili kutimiza lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii aliposema: “Nitafungua kinywa changu niseme nao kwa mifano; nitahubiri mambo yaliyofichika tangu kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.”
36 Tedy rozpuściwszy on lud, przyszedł Jezus do domu; i przystąpili do niego uczniowie jego, mówiąc: Wyłóż nam podobieństwo o kąkolu onej roli.
Kisha Yesu akaagana na makutano, akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia wakamwambia, “Tueleze maana ya ule mfano wa magugu shambani.”
37 A on odpowiadając, rzekł im: Ten, który rozsiewa dobre nasienie, jest Syn człowieczy;
Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
38 A rola jest świat, a dobre nasienie są synowie królestwa; ale kąkol są synowie onego złego;
Shamba ni ulimwengu na mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu.
39 Nieprzyjaciel zasię, który go rozsiał, jestci dyjabeł, a żniwo jest dokonanie świata, a żeńcy są Aniołowie. (aiōn g165)
Yule adui aliyepanda magugu ni ibilisi. Mavuno ni mwisho wa dunia, nao wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
40 Jako tedy zbierają kąkol, a palą go ogniem, tak będzie przy dokonaniu świata tego. (aiōn g165)
“Kama vile magugu yangʼolewavyo na kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. (aiōn g165)
41 Pośle Syn człowieczy Anioły swoje, a oni zbiorą z królestwa jego wszystkie zgorszenia, i te, którzy nieprawość czynią;
Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka Ufalme wake kila kitu kinachosababisha dhambi na watenda maovu wote.
42 I wrzucą je w piec ognisty, tam będzie płacz i zgrzytanie zębów.
Nao watawatupa katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
43 Tedy sprawiedliwi lśnić się będą jako słońce w królestwie Ojca swego. Kto ma uszy ku słuchaniu, niechaj słucha.
Ndipo wenye haki watangʼaa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio, na asikie.
44 Zasię podobne jest królestwo niebieskie skarbowi skrytemu w roli, który znalazłszy człowiek skrył, i od radości, którą miał z niego, odchodzi, i wszystko, co ma, sprzedaje, i kupuje onę rolę.
“Ufalme wa Mbinguni unafanana na hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa navyo, akalinunua lile shamba.”
45 Zasię podobne jest królestwo niebieskie człowiekowi kupcowi, szukającemu pięknych pereł;
“Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanyabiashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
46 Który znalazłszy jednę perłę bardzo drogą, odszedł, i posprzedawał wszystko, co miał, i kupił ją.
Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”
47 Zasię podobne jest królestwo niebieskie niewodowi zapuszczonemu w morze, i ryby wszelkiego rodzaju zagarniającemu.
“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu wa kuvua samaki uliotupwa baharini ukavua samaki wa kila aina.
48 Który gdy był pełen, wyciągnęli rybitwi na brzeg, a usiadłszy, wybierali dobre ryby w naczynia, a złe precz wyrzucali.
Ulipojaa, wavuvi wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini wale samaki wabaya wakawatupa.
49 Takci będzie przy dokonaniu świata; wynijdą Aniołowie, i wyłączą złe z pośrodku sprawiedliwych, (aiōn g165)
Hivi ndivyo itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenganisha watu waovu na watu wenye haki. (aiōn g165)
50 I wrzucą je w piec ognisty; tam będzie płacz i zgrzytanie zębów.
Nao watawatupa hao waovu katika tanuru la moto ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.”
51 Rzekł im Jezus: Wyrozumieliście to wszystko? Rzekli mu: Tak, Panie!
Yesu akauliza, “Je, mmeyaelewa haya yote?” Wakamjibu, “Ndiyo.”
52 A on im rzekł: Przetoż każdy nauczony w Piśmie, wyćwiczony w królestwie niebieskiem, podobny jest człowiekowi gospodarzowi, który wynosi z skarbu swego nowe i stare rzeczy.
Akawaambia, “Basi kila mwalimu wa sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa kutoka ghala yake mali mpya na mali ya zamani.”
53 I stało się, gdy Jezus dokończył tych podobieństw, puścił się stamtąd.
Yesu alipomaliza kutoa mifano hii, akaondoka.
54 A przyszedłszy do ojczyzny swojej, nauczał je w bóżnicy ich, tak iż się bardzo zdumiewali i mówili: Skądże temu ta mądrość, i ta moc?
Alipofika mji wa kwao, akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao wakastaajabu, wakauliza, “Mtu huyu amepata wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya miujiza?”
55 Izaż ten nie jest on syn cieśli? Izaż matki jego nie zowią Maryją, a bracia jego Jakób, i Jozes, i Szymon, i Judas?
“Huyu si yule mwana wa seremala? Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu zake si Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda?
56 A siostry jego izali wszystkie u nas nie są? Skądże tedy temu to wszystko?
Nao dada zake wote, hawako hapa pamoja nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya yote?”
57 I gorszyli się z niego; ale Jezus rzekł im: Nie jest prorok beze czci, tylko w ojczyźnie swojej i w domu swoim.
Wakachukizwa naye. Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake na nyumbani kwake.”
58 I nie uczynił tam wiele cudów dla niedowiarstwa ich.
Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa sababu ya kutokuamini kwao.

< Mateusza 13 >