< Kapłańska 18 >

1 Rzekł jeszcze Pan do Mojżesza, mówiąc:
Yahweh akazungumza na Musa, akisema,
2 Mów do synów Izraelskich, i rzecz im: Jam jest Pan, Bóg wasz.
“Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, “Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
3 Według obyczajów ziemi Egipskiej, w którejście mieszkali, nie czyńcie, ani według obyczajów ziemi Chananejskiej, do której Ja was prowadzę, nie czyńcie, a w ustawach ich nie chodźcie.
Msitende mambo ambayo watu wa Misri huyatenda, mahali mlikokuwa mkiishi awali. Na ni lazima msitende mambo yale wanayoyatenda watu wa Kanaani, nchi ambayo ninawapeleka nyinyi. Msifuate desturi zao.
4 Sądy moje czyńcie, a ustaw moich strzeżcie, abyście chodzili w nich; Jam Pan, Bóg wasz.
Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika, kwa sababu Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.
5 Przestrzegajcież tedy ustaw moich i sądów moich: które zachowywając człowiek, będzie w nich żył; Jam Pan.
Kwa hiyo ni lazima mzitunze hukumu zangu na sheria zangu. Ikiwa mtu amezitii, ataishi kwa sababu ya hizo. Mimi Ndimi Yahweh.
6 Żaden człowiek do bliskiej pokrewnej swojej nie przystępuj, aby odkrył sromotę jej; Jam Pan.
Pasiwepo kwenu atakayelala na yeyote aliye na uhusiano wa karibu naye. Mimi ndimi Yahweh.
7 Sromoty ojca twego, także sromoty matki twojej nie odkryjesz; matką twoją jest, nie odkryjesz sromoty jej.
Usimfedheheshe baba yako kwa kulala na mama yako. Yeye ni mama yako! Haikupasi kumfedhehesha yeye.
8 Sromoty żony ojca twego nie odkryjesz; sromota ojca twego jest.
Usilale na yeyote wa wake za baba yako; Usimfedheheshe namna hiyo baba yako.
9 Sromoty siostry twej, córki ojca twego, także córki matki twojej, tak rodzonej, jako i przyrodniej, nie odkryjesz sromoty ich.
Usilale na yeyote aliye mmoja miongoni mwa dada zako, ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako, ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe. Usilale na dada zako.
10 Sromoty córki syna twego, także sromoty córki córki twojej, nie odkryjesz; bo to sromota twoja.
Usilale na binti ya mwanao, au binti ya binti yako. Hiyo ingekuwa aibu yako mwenyewe.
11 Sromoty córki żony ojca twego, która się narodziła z ojca twego, siostra twoja jest, nie odkryjesz sromoty jej.
Usilale na binti ya mke wa baba yako, aliyezaliwa kwa baba yako, yeye ni dada yako, na usilale naye.
12 Sromoty siostry ojca twego nie odkryjesz; bo jest pokrewna ojca twego.
Usilale na dada ya baba yako. Yeye ni ndugu wa karibu kwa baba yako.
13 Sromoty siostry matki twojej nie odkryjesz; bo pokrewna matki twojej jest.
Usilale na dada ya mama yako. Yeye ni ndugu wa mama yako.
14 Sromoty brata ojca twego nie odkryjesz, do żony jego nie wnijdziesz; żona stryja twego jest.
Usimfedheheshe ndug wa baba yako kwa kulala na mke wake. Usimkaribie kwa kusudi hilo; yeye ni shangazi yako.
15 Sromoty synowej twojej nie odkryjesz; żona jest syna twego, nie odkryjesz sromoty jej;
Usilale na binti- mkwe wako, Yeye ni mke wa mwanao; usilale naye.
16 Sromoty żony brata twego nie odkryjesz: sromota brata twego jest.
Usilale na mke wa kaka yako; usije ukamfedhesha yeye katika njia hii.
17 Sromoty żony, i córki jej, nie odkryjesz; córki syna jej, i córki córki jej nie pojmiesz, abyś odkrył sromotę jej; bo pokrewne są, i sprośna to rzecz jest.
Usilale na mwanamke kisha na binti yake, au binti wa mwanawe au binti wa binti yake. Hao ni ndugu zake wa karibu, na kulala nao lingekuwa ni uovu.
18 Siostry żony twej nie pojmuj, abyś jej nie trapił, odkrywając sromotę jej, póki ona żywa.
Usimwoe dada ya mke wako kuwa mke wako wa pili na kulala naye wakati bado mke wako wa kwanza angali hai.
19 Do niewiasty, gdy jest w odłączeniu nieczystości, nie przystępuj, abyś odkrył sromotę jej.
Usilale na mwanamke wakati wake wa hedhi.
20 Z żoną bliźniego twego obcować nie będziesz, bo byś się splugawił z nią,
Yeye ni najisi kwa wakati huo. Usilale na mke wa jilani yako na kujichafua mwenyewe kwake katika njia hii.
21 Z nasienia twego nie dopuszczaj ofiarować Molochowi, abyś nie splugawił imienia Boga twego; Jam Pan
Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto, ili kwamba muwatoe sadaka kwa Moleki, kwa sababu msije mkalinajisi jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Yahweh.
22 Z mężczyną nie będziesz obcował, jako z niewiastą; obrzydliwością to jest.
Usilale na mwanaume mwingine kama ulalavyo na mwanamke. Jambo hili lingekuwa uovu.
23 Także z bydlęciem żadnem obcować nie będziesz, abyś się z niem miał splugawiać. Niewiasta też niech nie podlega bydlęciu dla obcowania z nim; sprośna rzecz jest.
Usilale na myama yeyote na kujitia unajisi kwake. Haimpasi mwanamke kufikiria kulala na mnyama ye yote. Huo ungekuwa upotovu.
24 Nie plugawcież się temi wszystkiemi rzeczami; bo tem wszystkiem splugawili się poganie, które Ja wyrzucam przed obliczem waszem.
Msijichafue wenyewe katika njia hizi, kwa kuwa katika njia hizi mataifa yamechafuliwa, mataifa ambayo Nitayafukuza yatoke kwa ajili yenu.
25 Bo splugawiła się ziemia; przetoż nawiedzę nieprawość jej na niej, i wyrzuci ziemia obywatele swoje.
Ni kwa sababu nchi imenajisiwa, hivyo niliiadhibu dhambi yao, nayo nchi ikawatapika wakazi wake
26 A tak wy przestrzegajcie ustaw moich i sądów moich, a nie czyńcie żadnych obrzydliwości tych, w domu zrodzony, i przychodzień, który jest gościem w pośrodku was.
Kwa hiyo, yawapasa kuzishika amri zangu na maagiza yangu, na msifanye aina yoyote ya mambo haya ya machukizo, wala Mwisraeli mzaliwa au Mgeni aishie miongoni mwenu.
27 Albowiem wszystkie te obrzydliwości czynili ludzie tej ziemi, którzy byli przed wami, czem splugawiona jest ziemia.
Kwa kuwa ni uovu huu ambao watu wametenda, wale ambao waliishi hapa kabla yenu, na sasa nchi imenajisiwa.
28 Aby was nie wyrzuciła ziemia, gdybyście ją splugawili, jako wyrzuciła naród, który był przed wami.
Kwa hiyo, muwe waangalifu ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu waliokuwako kabla yenu.
29 Albowiem ktobykolwiek co uczynił z tych wszystkich obrzydliwości, zaiste wytracone będą dusze to czyniące z pośrodku ludu swego.
Yeyote anayefanya mambo haya ya kuchukiza, watu wafanyao mambo hayo ya kuchukiza lazima watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao.
30 Strzeżcież tedy ustaw moich, nie czyniąc ustaw obrzydliwych, które czyniono przed wami, ani się plugawcie niemi; Jam Pan, Bóg wasz.
Kw a hiyo inawapasa kuzishika amri zangu na sitende mojawapo ya desturi hizi zenyekuchukiza ambazo zilitendwa hapo kabla yenu, ili msijinajisi wenyewe kwa hizo. Mimi ndimi Yahweh Mungu wenu.

< Kapłańska 18 >