< Kapłańska 14 >

1 Potem rzekł Pan do Mojżesza, mówiąc:
Bwana akamwambia Mose,
2 Tać jest ustawa około trędowatego w dzień oczyszczenia jego: przywiedziony będzie do kapłana.
“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
3 A wynijdzie kapłan precz za obóz: a obaczyli kapłan, że oto uleczona jest zaraza trądu, trądem zarażonego,
Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
4 Tedy rozkaże kapłan temu, który się oczyszcza, aby wziął dwa wróble żywe i zdrowe, i drzewo cedrowe, i jedwabiu karmazynowego, i hizopu.
kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
5 I rozkaże kapłan zabić jednego wróbla nad naczyniem glinianem, nad wodą żywą.
Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
6 Wróbla tedy żywego weźmie, i drzewo cedrowe, i jedwab karmazynowy i hizop, a omoczy to wszystko z wróblem żywym we krwi wróbla zabitego nad wodą żywą.
Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 I pokropi tego, który się oczyszcza od trądu, siedem kroć, i ogłosi go być czystym, a puści wróbla żywego w pole.
Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
8 A ten, który się oczyszcza, upierze szaty swoje, i ogoli wszystkie włosy swoje, a umyje się wodą, i czystym będzie. Potem wnijdzie do obozu, a będzie mieszkał przed namiotem swoim przez siedem dni.
“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
9 Potem dnia siódmego ogoli wszystkie włosy swe, głowę swą, i brodę swą, i brwi nad oczyma swemi, i wszystkie inne włosy swe ogoli; przytem upierze szaty swe, i ciało swe omyje wodą, a tak oczyszczon będzie.
Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
10 A dnia ósmego weźmie dwu baranków zupełnych, i owcę jednę roczną, zupełną, i trzy dziesiąte części efy mąki pszennej na ofiarę śniedną, zmieszaną z oliwą, i miarkę oliwy,
“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
11 Tedy kapłan, który oczyszcza człowieka, który ma być oczyszczony, postawi z temi rzeczami przed Panem, u drzwi namiotu zgromadzenia.
Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
12 Potem weźmie kapłan barana jednego, i będzie go ofiarował na ofiarę za występek, z oną miarką oliwy, i będzie to tam i sam obracał na ofiarę obracania przed obliczem Pańskiem.
“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
13 Zabije też baranka onego na miejscu, gdzie biją ofiary za grzech i ofiarę całopalenia, na miejscu świętem; bo jako ofiara za grzech tak ofiara za występek należy kapłanowi; rzecz najświętsza jest.
Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
14 I weźmie kapłan krwi z ofiary za występek, i pomaże kapłan koniec ucha prawego onemu, który się oczyszcza; także palec wielki u prawej ręki jego i palec wielki u prawej nogi jego.
Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
15 Weźmie też kapłan z onej miarki oliwy, a naleje na dłoń swoję lewą;
Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
16 A omoczy palec swój prawy w oliwie, która jest na lewej dłoni jego, i pokropi oliwą z palca swego siedem kroć przed obliczem Pańskiem.
na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
17 A z ostatku oliwy, która jest na dłoni jego, pomaże kapłan koniec ucha prawego onemu, który się oczyszcza, i wielki palec prawej ręki jego, także wielki palec prawej nogi jego z onejże krwi, która jest ofiarą za występek.
Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
18 A coby zostało oliwy, która jest na dłoni kapłanowej, pomaże tem głowę onego, który się oczyszcza; i tak go oczyści kapłan przed obliczem Pańskiem.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
19 Uczyni także kapłan ofiarę za grzech, i oczyści tego, który się oczyszcza, od nieczystości jego, a potem zabije ofiarę całopalenia.
“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
20 I ofiarować będzie kapłan ofiarę całopalenia, i ofiarę śniedną na ołtarzu; tak oczyści go kapłan, i czystym będzie.
na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
21 A jeźliby kto był tak ubogi, iżby tego nie przemógł, tedy weźmie baranka jednego na ofiarę za występek na podnoszenie dla oczyszczenia swego, i jednę dziesiątą część efy mąki pszennej zagniecionej z oliwą na ofiarę śniedną i miarkę oliwy.
“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
22 Nad to dwie synogarlice, albo dwoje gołąbiąt, czego dostać może, z których jedno będzie na ofiarę za grzech, a drugie na ofiarę całopalenia;
na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23 I przyniesie je w ósmy dzień oczyszczenia swego do kapłana, do drzwi namiotu zgromadzenia, przed obliczność Pańską.
“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
24 Weźmie tedy kapłan baranka ofiary za występek, i miarkę oliwy; i będzie to obracał tam i sam kapłan na ofiarę obracania przed Panem.
Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 A zabije baranka na ofiarę za występek: a wziąwszy kapłan ze krwi ofiary za występek, pomaże koniec ucha prawego temu, który się oczyszcza; i palec wielki prawej ręki jego, i palec wielki prawej nogi jego.
Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
26 Oliwy także naleje kapłan na lewą dłoń swoję.
Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
27 I kropić będzie kapłan palcem swoim prawym z oliwy, która jest na lewej ręce jego siedem kroć przed obliczem Pańskiem.
na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
28 Pomaże też kapłan oną oliwą, która jest na dłoni jego, koniec ucha prawego temu, który się oczyszcza; także wielki palec prawej ręki jego, i wielki palec prawej nogi jego na miejscu krwi z ofiary za występek;
Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
29 A ostatkiem oliwy, która jest na dłoni kapłana, pomaże głowę onego, który się oczyszcza, aby go oczyścił przed Panem.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
30 Także uczyni z jedną synogarlicą, albo z jednem gołębięciem, czegokolwiek z tych dostać może.
Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
31 Czego dostać mógł, jedno z tych będzie ofiarą za grzech, a drugie na ofiarę całopalenia z ofiarą śniedną; a tak oczyści kapłan tego, który się oczyszcza przed obliczem Pańskiem.
mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
32 A tać jest ustawa o tym, na którym by była zaraza trądu, który wszystkiego mieć nie może ku oczyszczeniu swemu.
Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
33 Rzekł potem Pan do Mojżesza i do Aarona, mówiąc:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
34 Gdy wnijdziecie do ziemi Chananejskiej, którą Ja wam dawam w osiadłość, a dopuściłbym zarazę trądu na który dom osiadłości waszej:
“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
35 Tedy on, którego dom jest, przyjdzie i opowie to kapłanowi, mówiąc: Jakoby zaraza trądu zda mi się być w domu moim,
ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
36 Rozkaże tedy kapłan wyprzątnąć dom pierwej niż sam wnijdzie, aby oglądał zarazę onę, iżby się nic nie splugawiło, coby było w domu, a potem kapłan wnijdzie, aby oglądał on dom.
Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
37 A oglądając onę zarazę, ujrzeli zarazę na ścianie domu, jakoby dołki czarne, przyzieleńszym, albo przyczerwieńszym, a na spojrzeniu byłoby głębsze niż ściana.
Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
38 Tedy wynijdzie kapłan z domu onego przede drzwi, i zamknie on dom przez siedem dni.
kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
39 Wróci się potem kapłan dnia siódmego i obejrzy; a jeźli się rozszerzyła zaraza na ścianach domu onego,
Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
40 Rozkaże kapłan wyłamać ono kamienie, na którem by była zaraza, i wyrzucić je precz za miasto na miejsce nieczyste;
ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
41 A dom rozkaże wewnątrz oskrobać wszędy w około; i wyrzucą on proch który oskrobali, precz za miasto na miejsce nieczyste;
Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
42 I wezmą kamienie insze i wprawią na miejsce innych kamieni; i wapna też inszego wezmą a potynkują dom.
Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43 A jeźliby się odnowiła ona zaraza, i rozszerzyła się po domu po wyrzuceniu kamienia, i po wyskrobaniu domu i po tynkowaniu jego:
“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
44 Tedy wnijdzie kapłan; a ujrzeli, że się rozszerzyła ona zaraza po domu, trąd jest jadowity w domu onym, nieczysty jest.
kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
45 Zatem rozwalą on dom, kamienie jego, i drzewo jego i wszystko wapno domu onego, a wyniosą precz za miasto na miejsce nieczyste.
Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
46 A ten kto by wszedł do domu onego, po wszystkie dni, póki był zawarty, nieczystym będzie aż do wieczora.
“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
47 A kto by spał w onym domu, upierze szaty swoje; także kto by jadł w tymże domu, upierze szaty swoje.
Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
48 Lecz jeźliby wyszedłszy kapłan obaczył, iż się nie szerzy zaraza po domu po tynkowaniu jego, tedy osądzi kapłan, że dom on jest czysty; bo uleczona jest zaraza ona.
“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
49 A weźmie na oczyszczenie onego domu dwu wróblów, i drzewo cedrowe, i jedwabiu, karmazynu, i hizopu;
Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
50 I zabije wróbla jednego nad naczyniem glinianem, nad wodą żywą;
Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
51 A wziąwszy drzewo cedrowe i hizop, i jedwab karmazynowy, i wróbla żywego, omoczy to wszystko we krwi wróbla zabitego i w wodzie żywej, a pokropi ten dom siedem kroć.
Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
52 I tak oczyści on dom krwią wróbla onego, i wodą żywą i wróblem żywym i drzewem cedrowem, i hizopem, i jedwabiem czerwonym.
Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
53 Potem puści wróbla żywego precz za miasto w pole; tak oczyści on dom, i czystym będzie.
Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
54 Tać jest ustawa o każdej zarazie trądu, i plamy czarnej:
Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
55 I o trądzie na szacie i na domu;
upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
56 I o sadzelu, i o świerzbie, i o białej plamie,
kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
57 Żeby poznać, gdy kto jest nieczystym, i gdy kto czystym. Tać jest ustawa około trądu.
kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

< Kapłańska 14 >