< Jozuego 8 >
1 Potem rzekł Pan do Jozuego: Nie bój się, ani się lękaj; weźmij z sobą wszystek lud wojenny, a wstawszy ciągnij do Haj, otom dał w ręce twoje króla Haj, i lud jego, i ziemię jego.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Usiogope, wala usivunjike moyo. Chukua jeshi lote la vita uende pamoja nalo kuishambulia Ai. Kwa kuwa nimeshamweka mikononi mwako mfalme wa Ai, pamoja na watu wake, mji wake na nchi yake.
2 A uczynisz Hajowi i królowi jego, jakoś uczynił Jerychu i królowi jego, wszakże łupy jego, i bydła jego rozbierzecie między się; uczyńże zasadzkę na miasto z tyłu jego.
Utafanya Ai na mfalme wake kama ulivyofanya kwa mji wa Yeriko na mfalme wake, isipokuwa mnaweza kuchukua mateka wake na mifugo wake, kwa ajili yenu. Weka waviziaji upande wa nyuma ya mji.”
3 A tak wstał Jozue i wszystek lud waleczny, aby ciągnęli ku Haj; i przebrał Jozue trzydzieści tysięcy mężów bardzo mocnych, i posłał je nocą.
Basi Yoshua na jeshi lote wakainuka kushambulia Ai. Akachagua watu mashujaa elfu thelathini walio bora miongoni mwa wapiganaji wake, akawapeleka wakati wa usiku
4 I rozkazał im, mówiąc: Patrzajcie wy, abyście uczynili zasadzkę za miastem; nie oddalajcie się od miasta daleko bardzo, a bądźcie wszyscy pogotowiu.
akiwaagiza: “Sikilizeni kwa makini. Mtavizia nyuma ya mji. Msiende mbali sana na mji. Wote kuweni macho.
5 A ja, i wszystek lud, który ze mną jest, przyciągniemy pod miasto; a gdy oni wynijdą przeciwko nam, jako pierwej ucieczemy przed nimi.
Mimi na watu walio pamoja nami, tutaukabili mji, kisha itakuwa hapo watu watakapotoka nje kupigana nasi, kama walivyofanya hapo kwanza, sisi tutawakimbia.
6 A oni pójdą za nami, aż je uwiedziemy od miasta; bo rzeką: Uciekają przed nami, jako i pierwej, gdyż uciekać będziemy przed nimi.
Watatufuatilia mpaka tutakapokuwa tumewavuta mbali na mji kwa kuwa watasema, ‘Wanatukimbia, kama walivyofanya hapo awali.’ Hivyo tutakapowakimbia,
7 Tedy wy wstaniecie z zasadzki, i wyprzecie ostatek ludu z miasta, i da je Pan, Bóg wasz, w rękę waszę.
ninyi inawapasa mwinuke mtoke huko mafichoni na kuuteka mji. Bwana Mungu wenu atautia mkononi mwenu.
8 A wziąwszy miasto, zapalicie je ogniem, według słowa Pańskiego uczynicie; patrzajcież, rozkazałem wam.
Mtakapokuwa mmeuteka mji, uteketezeni kwa moto. Fanyeni kama vile Bwana alivyoamuru. Angalieni, nimewaagiza.”
9 Posłał je tedy Jozue, i szli na zasadzkę; a zostali między Betel, i między Haj na zachód Hajowi; a Jozue przez onę noc został w pośrodku ludu.
Ndipo Yoshua akawatuma watu, nao wakaenda mahali pa kujificha, wakawa wanavizia kati ya Betheli na Ai, kuelekea upande wa magharibi wa Ai, lakini Yoshua akalala miongoni mwa watu usiku huo.
10 Potem wstawszy Jozue bardzo rano, obliczył lud, a szedł sam i starsi z Izraela przed ludem przeciw Haj.
Asubuhi na mapema siku iliyofuatia, Yoshua akawakutanisha watu wake, na yeye na viongozi wa Israeli wakawa mbele ya watu kwenda Ai.
11 Wszystek też lud wojenny, który z nim był, ruszyli się, i przyciągnąwszy przyszli pod miasto, i położyli się obozem na stronie północnej ku Haj; a była dolina między nim, i między Haj.
Watu wote wa vita waliokuwa pamoja naye walipanda, wakakaribia na kufika mbele ya mji. Wakapiga kambi kaskazini mwa Ai, pakiwa na bonde kati yao na huo mji.
12 Nadto wziął około pięciu tysięcy mężów, które postawił na zasadzce między Betel, i między Haj, od strony zachodniej miasta.
Yoshua alikuwa amewachukua watu wapatao elfu tano, akawaweka katika uavizi kati ya Betheli na Ai, upande wa magharibi wa mji.
13 I przybliżył się lud, to jest, wszystko wojsko, które było od północy miasta, i którzy byli na zasadzce jego od zachodu miasta; i przyciągnął Jozue onej nocy w pośrodek doliny.
Wakawaweka askari katika maeneo yao: wale wote waliokuwa kambini wakawa kaskazini ya mji na wale waliokuwa wakivizia wakawa upande wa magharibi. Usiku huo Yoshua akaenda katika lile bonde.
14 I stało się, gdy je ujrzał król Haj, pospieszyli się i wstali rano, i wyszli ludzie z miasta przeciw Izraelowi ku bitwie, sam król, i wszystek lud jego, na czas naznaczony przed równinę, nie wiedząc, że zasadzka była uczyniona nań za miastem.
Mfalme wa Ai alipoona jambo hili, yeye pamoja na watu wote wa mji wakatoka kwa haraka asubuhi na mapema, ili kukutana na Israeli katika vita mahali fulani panapotazamana na Araba. Lakini hakujua kwamba kulikuwa kumewekwa waviziaji dhidi yake nyuma ya mji.
15 Tedy Jozue i wszystek Izrael, jakoby od nich porażeni, uciekali drogą ku puszczy.
Yoshua na Israeli wote wakaruhusu kurudishwa nyuma mbele yao, na kuelekea jangwani.
16 I zwołany jest wszystek lud, który był w mieście, aby je gonili, i gonili Jozuego; i tak uwiedzieni byli od miasta.
Watu wote wa Ai wakaitwa ili kuwafuatia, nao wakavutwa kumfuatia Yoshua mbali na mji.
17 I nie został nikt w Haj i w Betel, któryby nie wyszedł za Izraelem; i zostawili miasto otworzone, a gonili Izraela.
Hakuna hata mwanaume mmoja aliyebakia Ai wala Betheli ambaye hakufuatia Israeli. Wakauacha mji wazi na kuwafuatia Israeli.
18 Tedy rzekł Pan do Jozuego: Podnieś chorągiew, którą masz w ręce swej, przeciwko Haj; bo je w ręce twoje dam. I podniósł Jozue chorągiew, którą miał w ręce swej, przeciwko miastu.
Ndipo Bwana akamwambia Yoshua, “Inua huo mkuki ulio mkononi mwako kuuelekeza Ai, kwa kuwa nitautia huo mji mkononi mwako.” Hivyo Yoshua akauelekeza mkuki wake Ai.
19 A oni, co byli na zasadzce, wstawszy prędko z miejsca swego; bieżali, gdy on podniósł rękę swą, a ubieżawszy miasto, wzięli je, i zaraz je zapalili ogniem.
Mara tu alipofanya hivi, wale watu waliokuwa mavizioni wakaondoka upesi kutoka mahali pao na kukimbilia mbele. Wakaingia ndani ya mji, wakauteka na kuutia moto kwa haraka.
20 A obejrzawszy się mężowie miasta Haj ujrzeli, a oto, wstępował dym miasta ku niebu, i nie mieli miejsca do uciekania, ani tam, ani sam; bo lud, który uciekał ku puszczy, obrócił się na one, co je gonili.
Watu wa Ai wakaangalia nyuma, wakauona moshi wa huo mji ukielekea angani lakini hawakuwa na nafasi ya kutoroka kwa upande wowote, kwa kuwa wale Waisraeli waliokuwa wanawakimbia kuelekea jangwani walikuwa wamegeuka nyuma kuwakabili wakimbizaji wao.
21 Tedy Jozue i wszystek lud Izraelski, widząc, iż oni, co byli na zasadzce, wzięli miasto, a iż wychodził dym z miasta, obrócili się i pobili męże miasta Haj.
Basi Yoshua na Israeli wote walipoona kwamba waviziaji wameshauteka mji na moshi ulikuwa unapaa juu kutoka kwenye mji, wakawageukia watu wa Ai na kuwashambulia.
22 Oni też drudzy wyszli z miasta przeciwko nim, i obtoczyli je Izraelczycy, jedni stąd, a drudzy zowąd, i porazili je tak, iż z nich żaden nie został, ani uszedł.
Wale waviziaji nao pia wakatoka nje ya mji dhidi yao, hivi kwamba wakashikiwa katikati, Waisraeli wakiwa pande zote mbili. Israeli wakawaua, bila kuwaachia yeyote aliyenusurika wala aliyetoroka.
23 Tamże króla Haj pojmali żywo, i przywiedli go przed Jozuego.
Lakini wakamchukua mfalme wa Ai akiwa hai na kumleta kwa Yoshua.
24 Gdy tedy Izraelczycy pobili wszystkie obywatele Haj na polu przy puszczy, tedy za nimi szli w pogoń, a polegli oni wszyscy od miecza, aż wygładzeni są; obrócili się wszyscy Izraelczycy do Haj, i wysiekli je ostrzem miecza.
Israeli ilipomaliza kuwaua wanaume wote wa Ai katika mashamba na jangwani walipokuwa wamewafukuzia, na baada ya kila mmoja wao kuuawa kwa upanga, Waisraeli wote wakarudi Ai na kuwaua wale waliokuwa wamebakia mjini.
25 I było wszystkich, którzy polegli dnia onego, od męża aż do niewiasty dwanaście tysięcy, wszystkich obywateli Haj.
Watu kumi na mbili elfu, waume kwa wake, waliangamia siku ile, yaani watu wote wa Ai.
26 A Jozue nie spuścił ręki swej, którą był podniósł z chorągwią, aż pobił wszystkie obywatele Haj.
Kwa maana Yoshua hakuurudisha ule mkono wake uliokuwa umeuinua mkuki hadi alipomaliza kuwaangamiza wote walioishi Ai.
27 Tylko bydło, i łupy miasta onego rozebrali między się Izraelczycy według słowa Pańskiego, które rozkazał Jozuemu.
Lakini Israeli wakajichukulia mifugo na nyara za mji huu, kama vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Yoshua.
28 Tedy zapalił Jozue Haj, i uczynił je mogiłą wieczną, i pustynią aż do dnia tego.
Kwa hiyo Yoshua akauchoma moto mji wa Ai na kuufanya kuwa lundo la magofu la kudumu, mahali pa ukiwa hadi leo.
29 A króla Haj obwiesił na drzewie aż do wieczora; a gdy słońce zaszło, rozkazał Jozue, aby zdjęto trupa jego z drzewa, a porzucono go w samem wejściu bramy miejskiej, i namiotali nań kupę wielką kamieni, która jest aż do dnia tego.
Akamwangika mfalme wa Ai kwenye mti na kumwacha hapo mpaka jioni. Wakati wa jua kutua, Yoshua akawaamuru wautoe mwili wake kwenye mti na kuutupa kwenye ingilio la lango la mji. Kisha wakalundika mawe makubwa mengi juu yake, ambayo yamesalia mpaka leo.
30 Tedy Jozue zbudował ołtarz Panu, Bogu Izraelskiemu, na górze Hebal.
Kisha Yoshua akajenga madhabahu ya Bwana, Mungu wa Israeli, katika Mlima wa Ebali,
31 Jako był rozkazał Mojżesz, sługa Pański, synom Izraelskim, a jako napisano w księgach zakonu Mojżeszowego, ołtarz z całego kamienia, na którym żadne żelazo nie postało; i sprawowali na nim całopalenia Panu, ofiarowali też spokojne ofiary.
kama Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa amewaamuru Waisraeli. Akaijenga sawasawa na ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria ya Mose: madhabahu ya mawe yasiyochongwa, ambayo juu yake hakuna chombo cha chuma kilichotumika. Hapo juu yake wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa na kutoa sadaka za amani.
32 Tamże napisał na kamieniach powtórzenie zakonu Mojżeszowego, który napisał przed oblicznością synów Izraelskich.
Pale, mbele ya Waisraeli Yoshua akanakili juu ya hayo mawe sheria ya Mose, aliyokuwa ameiandika.
33 A wszystek Izrael, i starsi jego, i przełożeni, i sędziowie jego, stali po obu stronach skrzyni przed kapłanami Lewitami, którzy nosili skrzynię przymierza Pańskiego, tak przychodzień, jako w domu zrodzony, połowa ich przeciw górze Garyzym, a połowa ich przeciw górze Hebal, jako był przedtem rozkazał Mojżesz, sługa Pański, aby błogosławiono ludowi Izraelskiemu.
Israeli yote, wageni na wazawa sawasawa, wakiwa na wazee wao, maafisa na waamuzi, walikuwa wamesimama pande zote mbili za Sanduku la Agano la Bwana, wakiwaelekea wale waliokuwa wamelichukua, yaani makuhani, ambao ni Walawi. Nusu ya watu ilisimama mbele ya Mlima Gerizimu na nusu hiyo ingine ikasimama mbele ya Mlima Ebali, kama vile Mose mtumishi wa Bwana alivyokuwa ameamuru hapo mwanzo alipotoa maagizo ya kuwabariki watu wa Israeli.
34 A potem czytał wszystkie słowa zakonu, błogosławieństwo, i przeklęstwo, według wszystkiego, co napisano w księgach zakonu.
Hatimaye, Yoshua akasoma maneno yote ya sheria, yaani baraka na laana, kama vile ilivyoandikwa katika Kitabu cha Sheria.
35 Nie było i słowa ze wszystkiego, co rozkazał Mojżesz, czego by nie czytał Jozue przed wszystkiem zgromadzeniem Izraelskiem, przed niewiastami, i przed dziatkami, i przed przychodniami, którzy mieszkali między nimi.
Hakuna neno lolote katika yale yote ambayo Mose alikuwa ameamuru ambalo Yoshua hakulisomea kusanyiko lote la Israeli, ikiwa ni pamoja na wanawake na watoto, na wageni walioishi miongoni mwao.