< Jozuego 16 >
1 Padł też los synom Józefowym od Jordanu ku Jerychu przy wodach Jerycha na wschód słońca, puszcza, która idzie od Jerycha przez górę Betel.
Mgawanyo wa Yosefu ulianzia Yordani ya Yeriko, mashariki mwa miji ya Yeriko na kutoka hapo ulipanda kupitia jangwani na kuingia katika nchi ya vilima ya Betheli.
2 A wychodzi od Betel do Luzy, a idzie do granicy Archy, do Attarot.
Ukaendelea kutoka Betheli (ndiyo Luzu), ukavuka kuingia eneo la Waariki huko Atarothi,
3 Potem się ciągnie ku morzu do granicy Jaflety, aż do granicy Bet Horonu dolnego, i aż do Gazer, a kończy się aż u morza.
ukateremkia kuelekea magharibi hadi eneo la Wayafleti ukienea hadi eneo la Beth-Horoni ya Chini hadi Gezeri, ukiishia baharini.
4 I wzięli dziedzictwo synowie Józefowi, Manase i Efraim.
Kwa hiyo Manase na Efraimu, wazao wa Yosefu, walipokea urithi wao.
5 A była granica synów Efraimowych według domów ich; była mówię granica dziedzictwa ich na wschód słońca od Attarot Adar aż do Bet Horon wyższego.
Hili ndilo lilikuwa eneo la Efraimu, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao ulianzia Ataroth-Adari upande wa mashariki hadi Beth-Horoni ya Juu,
6 I wychodzi ta granica do morza od Machmeta ku północy, a idzie kołem ta granica pod wschód słońca do Tanat Selo, i przechodzi ją od wschodu aż do Janoe;
na kuendelea mpaka baharini. Kutoka Mikmeta upande wa kaskazini ulipinda kuelekea mashariki hadi Taanath-Shilo, ukiupita hadi Yanoa upande wa mashariki.
7 I ciągnie się od Janoe do Attarot i Naarata, a przychodzi do Jerycha, a wychodzi ku Jordanowi.
Kisha uliteremka kutoka Yanoa hadi Atarothi na Naara, ukagusa Yeriko na kutokea katika Mto Yordani.
8 Od Tafua bieży ta granica ku zachodowi do potoku Kana, a kończy się przy morzu. Toć jest dziedzictwo pokolenia synów Efraimowych według domów ich.
Kutoka Tapua mpaka ulikwenda magharibi hadi Bonde la Kana na kuishia baharini. Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Waefraimu, ukoo kwa ukoo.
9 Miasta też oddzielone synom Efraimowym były w pośród dziedzictwa synów Manasesowych, wszystkie miasta i wsi ich.
Pia ulijumuisha miji yote na vijiji vyake ambavyo vilitengwa kwa ajili ya Waefraimu ndani ya urithi wa kabila la Manase.
10 I nie wygnali Chananejczyka, mieszkającego w Gazer; i mieszkał Chananejczyk w pośrodku Efraimitów aż do dnia tego, i hołdował im, dań dawając.
Hawakuwatoa Wakanaani waishio Gezeri; mpaka leo Wakanaani wanaishi miongoni mwa watu wa Efraimu lakini wanatakiwa kufanya kazi ngumu za kulazimishwa.