< Jozuego 14 >

1 A toć jest, co dziedzictwem wzięli synowie Izraelscy w ziemi Chananejskiej, a co prawem dziedzicznem oddali im w osiadłość Eleazar kapłan i Jozue, syn Nunów, i przedniejsi z ojców z pokolenia synów Izraelskich.
Maeneo haya ya nchi ambayo watu wa Israeli waliyapokea kama urithi wao katika nchi ya Kanaani. Urith huu uligawanywa kwao na Eliazeri kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya mababu wa familia zao kati ya watu wa Israeli.
2 Losem dzieląc dziedzictwo ich, jako był rozkazał Pan przez Mojżesza, dziewięciorgu pokoleniu i połowie pokolenia.
Urithi wao ulichaguliwa kwa kupiga kura kwa makabila tisa na nusu, kama vile Yahweh alivyoagiza kwa mkono wa Musa.
3 Albowiem Mojżesz był oddał dziedzictwo dwom pokoleniom i połowie pokolenia za Jordanem; ale Lewitom nie dał był dziedzictwa między nimi.
Kwa kuwa Musa alikuwa amewapa urithi makabila mawili na nusu ng'ambo ya Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi wowote.
4 Bo było synów Józefowych dwa pokolenia, Manasesowe i Efraimowe; ani dali działu Lewitom w ziemi, oprócz miast ku mieszkaniu, z przedmieściami ich dla bydła ich i dla trzód ich.
Kabila la Yusufu kwa uhalisia yalikuwa makabila mawili, Manase na Efraimu. Na hakuna sehemu yoyote ya urithi waliyopewa Walawi katika nchi, lakini walipewa miji ya kuishi ndani yake pamoja na sehemu ya malisho ya mifugo yao na kwa ajili ya riziki zao.
5 Jako rozkazał Pan Mojżeszowi, tak uczynili synowie Izraelscy, i podzielili ziemię.
Watu wa Israeli walifanya hivyo kama vile Yahweh alivyomwagiza Musa, basi waliiganywa nchi.
6 Tedy przyszli synowie Judowi do Jozuego w Galgal; i rzekł do niego Kaleb, syn Jefuna Kenezejskiego: Ty wiesz, co mówił Pan do Mojżesza, męża Bożego, o mnie i o tobie w Kades Barnie.
Kisha kabila la Yuda lilikuja kwa Yoshua huko Giligali. Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi, akamwambia,”Unajua kile Yahweh alichomwambia Musa mtu wa Mungu juu yako na mimi huko Barnea.
7 Czterdzieści mi lat było, gdy mnie słał Mojżesz, sługa Pański, z Kades Barny ku przeszpiegowaniu ziemi, i odniosłem mu tę rzecz, jako było w sercu mojem.
Nilikuwa na umri wa miaka arobani wakati Musa mtumishi wa Yahweh aliponituma kutoka Kadeshi Barnea kuipeleleza nchi. Nilimletea taarifa tena kama nilivyotakiwa kufanya katika moyo wangu.
8 Lecz bracia moi, którzy chodzili ze mną, skazili serce ludowi; alem ja przecię szedł statecznie za Panem, Bogiem moim.
Lakini ndugu zangu walioenda pamoja nami waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa woga. Lakini mimi nilimfuata Yahweh kabisa.
9 I przysiągł Mojżesz dnia onego, mówiąc: Zaiste ziemia, którą deptała noga twoja, przyjdzie tobie w dziedzictwo, i synom twoim aż na wieki, przeto żeś statecznie chodził za Panem, Bogiem moim.
Musa aliapa katika siku hiyo akisema, “Hakika nchi ambayo miguu yako imetembea juu yake itakuwa urithi wako na kwa watoto wako milele, kwasababu umemfuata kabisa Yahweh Mungu wangu.
10 A teraz oto przedłużył żywota mego Pan, jako powiedział; już są czterdzieści i pięć lat od onego czasu, jako to mówił Pan do Mojżesza, a jako chodzili Izraelczycy po puszczy; a teraz oto ja dziś mam osiemdziesiąt i pięć lat:
Tazama! sasa, Yahweh amenihifadhi hai kwa miaka hii arobaini na tano, kama alivyosema - tangu kipindi kile Yahweh alivyomwambia Musa neno hili, wakati huo Waisraeli walikuwa wakitembea jangwani. Tazama! sasa katika siku hii ya leo nina miaka themanini na mitano.
11 A jeszcze i dziś takiem duży, jakom był w on czas, gdy mię wysłał Mojżesz; a jako moc moja była na on czas, taka jest moc moja i teraz ku bojowaniu, i ku wychodzeniu i przychodzeniu.
Bado hata siku hii ya leo nina nguvu kama nilivyokuwa katika siku ile ambayo Musa alinituma. Nguvu zangu za sasa ni sawa na nguvu zangu za kipindi kile, kwa ajili ya vita na kwa kwenda na kwa kuja.
12 A tak teraz daj mi tę górę, o której powiedział Pan dnia onego; boś ty słyszał dnia onego, iż tam są Enakitowie, i miasta wielki a obronne; będzieli Pan ze mną, wypędzę je, jako mi obiecał Pan.
Sasa basi, nipe nchi hii ya milima, ambayo Yahweh aliniahidi katika siku hiyo. Kwa kuwa ulisikia katika siku hiyo kuwa Wanakimu walikuwa huko katika miji yenye ngome. Itakuwa kwamba Yahweh atakuwa pamoja nami na ya kwamba nitawafukuzia mbali, kama vile Yahweh alivyosema.”
13 I błogosławił mu Jozue, a dał Hebron Kalebowi, synowi Jefunowemu, w dziedzictwo.
Kisha Yoshua alimbariki Kalebu mwana wa Yefune na alimpa Hebroni kama urithi wake.
14 A tak dostał się Hebron Kalebowi, synowi Jefuna Kenezejskiego, w dziedzictwo aż do dnia tego, przeto że statecznie chodził za Panem, Bogiem Izraelskim.
Hivyo Hebroni ikawa urithi wa Kalebu mwana wa Yefune Mkenizi hata leo, kwasababu alimfuata kabisa Yahweh, Mungu wa Israeli.
15 A zwano przedtem Hebron miasto Arba, który Arba był człowiekiem wielkim między Enakity; i uspokoiła się ziemia od wojen
Basi, jina la Hebroni hapo mwanzo lilikuwa ni Kiriathi Arba ( Arba ambaye alikuwa ni mtu mkuu miongoni mwa Wanakim). Kisha nchi ikawa na raha bila vita.

< Jozuego 14 >