< Jana 20 >
1 A pierwszego dnia po sabacie Maryja Magdalena przyszła rano do grobu, gdy jeszcze było ciemno, i ujrzała kamień odwalony od grobu.
Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa kungali giza bado, Maria Magdalene alikwenda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
2 I bieżała, a przyszła do Szymona Piotra i do onego drugiego ucznia, którego miłował Jezus, i rzekła im: Wzięli Pana z grobu, a nie wiemy, gdzie go położyli.
Hivyo akaja akikimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
3 Tedy wyszedł Piotr i on drugi uczeń, a szli do grobu.
Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara kuelekea kaburini.
4 I bieżeli obaj społem; ale on drugi uczeń wyścignął Piotra i pierwej przyszedł do grobu.
Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5 A nachyliwszy się, ujrzał leżące prześcieradła; wszakże tam nie wszedł.
Alipofika, akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani mle ndani, lakini hakuingia.
6 Przyszedł też i Szymon Piotr, idąc za nim, i wszedł w grób, i ujrzał prześcieradła leżące,
Ndipo Simoni Petro akaja, akimfuata nyuma akaenda moja kwa moja hadi ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini
7 I chustkę, która była na głowie jego, nie z prześcieradłami położoną, ale z osobna na jednem miejscu zwiniętą.
na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Yesu. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa mahali pa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
8 Potem wszedł i on drugi uczeń, który był pierwej przyszedł do grobu, i ujrzał, a uwierzył.
Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini naye akaingia ndani, akaona, akaamini,
9 Albowiem jeszcze nie rozumieli Pisma, iż miał zmartwychwstać.
(kwa kuwa mpaka wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Yesu afufuke kutoka kwa wafu).
10 I odeszli zaś oni uczniowie do domu.
Kisha hao wanafunzi wakaondoka wakarudi nyumbani kwao.
11 Ale Maryja stała u grobu, na dworze płacząc; a gdy płakała, nachyliła się w grób.
Lakini Maria Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama, kuchungulia mle kaburini,
12 I ujrzała dwóch Aniołów w bieli siedzących, jednego u głowy, a drugiego u nóg, tam gdzie było położone ciało Jezusowe.
naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
13 Którzy jej rzekli: Niewiasto! czemu płaczesz? Rzekła im: Iż wzięli Pana mego, a nie wiem, gdzie go położyli.
Wakamuuliza Maria, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu na sijui walikomweka.”
14 A to rzekłszy, obróciła się nazad i ujrzała Jezusa stojącego; lecz nie wiedziała, iż Jezus był.
Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama, lakini hakumtambua.
15 Rzekł jej Jezus: Niewiasto! czemu płaczesz? kogo szukasz? A ona mniemając, że był ogrodnik, rzekła mu: Panie! jeźliś go ty wziął, powiedz mi, gdzieś go położył, a ja go wezmę.
Yesu akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Maria akidhani ya kuwa aliyekuwa anaongea naye ni mtunza bustani, kwa hiyo akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nionyeshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Rzekł jej Jezus: Maryjo! Która obróciwszy się, rzekła mu: Rabbuni! co się wykłada: Nauczycielu!
Yesu akamwita, “Maria!” Ndipo Maria akamgeukia Yesu na kusema naye kwa Kiebrania, “Rabboni!” (maana yake Mwalimu).
17 Rzekł jej Jezus: Nie dotykaj się mnie, bom jeszcze nie wstąpił do Ojca mego; ale idź do braci moich, a powiedz im: Wstępuję do Ojca mego i Ojca waszego, i do Boga mego i Boga waszego.
Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’”
18 Tedy przyszła Maryja Magdalena, oznajmując uczniom, że widziała Pana, a że jej to powiedział.
Kwa hiyo Maria Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Yesu, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Yesu alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
19 A gdy był wieczór dnia onego pierwszego po sabacie, a drzwi były zamknięte, gdzie byli uczniowie zgromadzeni dla bojaźni żydowskiej, przyszedł Jezus i stanął w pośrodku nich, i rzekł im: Pokój wam!
Ikawa jioni ya ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi. Naye Yesu aliwatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
20 A to rzekłszy pokazał im ręce i bok swój; a uradowali się uczniowie, ujrzawszy Pana.
Baada ya kusema haya, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana.
21 Rzekł im zasię Jezus: Pokój wam; jako mię posłał Ojciec, tak i ja was posyłam.
Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.”
22 A to rzekłszy tchnął na nie i rzekł im: Weźmijcie Ducha Świętego.
Naye alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Którymkolwiek grzechy odpuścicie, są im odpuszczone, a którymkolwiek zatrzymacie, są zatrzymane.
Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa, na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
24 A Tomasz, jeden ze dwunastu, którego zowią Dydymus, nie był z nimi, gdy był przyszedł Jezus.
Lakini Tomaso, aliyeitwa Didimasi, yaani Pacha, mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
25 I rzekli mu drudzy uczniowie: Widzieliśmy Pana. Ale im on rzekł: Jeźli nie ujrzę w ręku jego znaków gwoździ, a nie włożę palca mego w znaki gwoździ, a nie włożę ręki mojej w bok jego, nie uwierzę.
Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
26 A po ośmiu dniach byli zasię uczniowie jego w domu, i Tomasz z nimi. I przyszedł Jezus, gdy były drzwi zamknięte, a stanął w pośrodku nich, i rzekł: Pokój wam!
Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Yesu akaja milango ikiwa imefungwa na kusimama katikati yao akasema, “Amani iwe nanyi.”
27 Potem rzekł Tomaszowi: Włóż sam palec twój, a oglądaj ręce moje i ściągnij rękę twoję, i włóż ją w bok mój, a nie bądź niewiernym, ale wiernym.
Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
28 Tedy odpowiedział Tomasz i rzekł mu: Panie mój, i Boże mój!
Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
29 Rzekł mu Jezus: Żeś mię ujrzał, Tomaszu, uwierzyłeś; błogosławieni którzy nie widzieli, a uwierzyli.
Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
30 Wieleć i innych cudów uczynił Jezus przed oczyma uczniów swoich, które nie są napisane w tych księgach.
Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
31 Ale te są napisane, abyście wy wierzyli, że Jezus jest Chrystus, Syn Boży, a żebyście wierząc żywot mieli w imieniu jego.
Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.