< Hioba 41 >

1 Wyciągnieszże wędą wieloryba? albo sznurem utopionym w języku jego?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 Izali zawleczesz kolce przez nozdrza jego? albo hakiem przekoleszli czeluść jego?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 Izalić się będzie wiele modlił, albo z tobą łagodnie mówić będzie?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 Izali uczyni przymierze z tobą, a przyjmiesz go za sługę wiecznego?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 Izali z nim będziesz igrał jako z ptaszkiem, a uwiążesz go dziatkom twoim?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 Sprawiże sobie nad nim towarzystwo ucztę, a podzielą go między kupców?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 Izali zawadzisz hakami za skórę jego, a widelcami rybackiemi za głowę jego?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 Połóż tylko nań rękę twą, ślubujęć, że nie wspomnisz więcej na bitwę.
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 Oto nadzieja ułowienia jego omylna jest; izali i wejrzawszy nań człowiek nie upada?
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 Niemasz tak śmiałego, coby go obudził; owszem któż się stawi przed twarzą moją?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 Któż mi co dał, abym mu oddał? cokolwiek jest pod wszystkiem niebem, moje jest.
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 Nie zamilczę członków jego, ani silnej mocy jego, a grzecznego kształtu jego.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 Któż odkryje wierzch odzienia jego? z dwoistemi wędzidłami swemi któż przystąpi do niego?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 Wrota gęby jego któż otworzy? bo strach około zębów jego.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 Łuski jego mocne jako tarcze, bardzo ściśle spojone.
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 Jedna z drugą tak spojona, że wiatr nie wchodzi między nie.
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 Jedna do drugiej przylgnęła, ujęły się, a nie dzielą się.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 Kichanie jego czyni blask, a oczy jego są jako powieki zorzy.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 Z ust jego lampy wychodzą, a iskry ogniste wyrywają się.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 Z nozdrzy jego wychodzi dym, jako z garnca wrzącego, albo kotła.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 Dech jego węgle rozpala, a płomień z ust jego wychodzi.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 W szyi jego przemieszkuje moc, a boleść przed nim ucieka.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 Sztuki ciała jego spoiły się, całowite są w nim, że się nie porusza.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 Serce jego twarde jako kamień, tak twarde, jako sztuka spodniego kamienia młyńskiego.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 Gdy się podnosi, drżą mocarze, a od strachu oczyszczają się.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 Miecz, który go sięga, nie ostoi się, ani drzewce, ani strzała, ani pancerz.
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 Żelazo poczyta sobie za plewę, a miedź za drzewo zbótwiałe.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 Nie upłoszy go strzała, a jako źdźbło są u niego kamienie z procy.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Strzelbę sobie poczyta jako słomę, a pośmiewa się z szermowania włócznią.
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 Pod nim są ostre skorupy; ściele sobie na rzeczach ostrych jako na błocie.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 Czyni, że wre głębokość jako garniec, a że się mąci morze jako w moździerzu.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 Za sobą jasną ścieszkę czyni, tak, że się zdaje, iż przepaść ma siwiznę.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 Niemasz na ziemi równego mu, który tak stworzony jest, że się niczego nie boi.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 Wszelką rzecz wysoką lekce waży; on jest królem nad wszystkiemi srogiemi zwierzętami.
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”

< Hioba 41 >