< Hioba 29 >
1 Jeszcze dalej Ijob prowadził rzecz swoję, i rzekł:
Ayubu akaendelea na hoja yake, akasema:
2 Któż mi to da, abym był jako za miesięcy dawnych, za dni onych, których mię Bóg strzegł;
“Tazama jinsi ninavyoitamani miezi iliyopita, zile siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda,
3 Gdy pochodnia jego świeciła nad głową moją, a przy świetle jego przechodziłem ciemności;
wakati taa yake iliniangazia kichwani changu, na kwa mwanga wake Mungu nikapita katikati ya giza!
4 Jakom był za dni młodości mojej, gdy była przytomność Boża nad przybytkiem moim;
Natamani siku zile nilizokuwa katika ustawi wangu, wakati urafiki wa Mungu wa ndani ulipoibariki nyumba yangu,
5 Gdy jeszcze Wszechmocny był ze mną, a około mnie dziatki moje;
wakati Mwenyezi alikuwa pamoja nami, nao watoto wangu walikuwa wamenizunguka,
6 Gdy ścieszki moje opływały masłem, a opoka wylewała mi źródła oliwy;
wakati njia yangu ilikuwa imenyweshewa siagi, nao mwamba ukanimiminia vijito vya mafuta ya zeituni.
7 Gdym wychodził do bramy przez miasto, a na ulicy kazałem sobie gotować stolicę moję.
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8 Widząc mię młodzi ukrywali się, a starcy powstawszy stali.
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9 Przełożeni przestawali mówić, a ręką zatykali usta swoje.
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10 Głos książąt ucichał, a język ich do podniebienia ich przylegał.
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11 Bo ucho słuchające błogosławiło mię, a oko widzące dawało o mnie świadectwo,
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
12 Żem wybawiał ubogiego wołającego, i sierotkę, i tego, który nie miał pomocnika.
kwa sababu nilimwokoa maskini aliyeomba msaada, naye yatima aliyekuwa hana wa kumsaidia.
13 Błogosławieństwo ginącego przychodziło na mię, a serce wdowy rozweselałem.
Mtu aliyekuwa karibu kufa alinibariki, nami niliufanya moyo wa mjane kuimba.
14 W sprawiedliwość obłoczyłem się, a ona zdobiła mię; sąd mój był jako płaszcz i korona.
Niliivaa haki kama vazi langu; uadilifu ulikuwa joho langu na kilemba changu.
15 Byłem okiem ślepemu, a nogą chromemu.
Nilikuwa macho ya kipofu na miguu kwa kiwete.
16 Byłem ojcem ubogich, a sprawy, którejm nie wiedział, wywiadywałem się.
Nilikuwa baba kwa mhitaji; nilimtetea mgeni.
17 I kruszyłem szczęki złośnika, a z zębów jego wydzierałem łup.
Niliyavunja meno makali ya waovu, na kuwapokonya wahanga kwenye meno yao.
18 Przetożem rzekł: W gniaździe swojem umrę, a jako piasek rozmnożę dni moje.
“Nikafikiri, ‘Nitafia katika nyumba yangu mwenyewe, nazo siku zangu zitakuwa nyingi kama chembechembe za mchanga.
19 Korzeń mój rozłoży się przy wodach, a rosa trwać będzie przez noc na gałązkach moich.
Mizizi yangu itafika mpaka kwenye maji, nao umande utakaa juu ya matawi yangu usiku kucha.
20 Chwała moja odmłodzi się przy mnie, a łuk mój w ręce mojej odnowi się.
Utukufu wangu utabakia kuwa mpya ndani yangu, upinde wangu daima utaendelea kuwa mpya mkononi mwangu.’
21 Słuchano mię, i oczekiwano na mię, a milczano na radę moję.
“Watu walinisikiliza kwa tumaini, wakingojea ushauri wangu kwa utulivu.
22 Po słowie mojem nie powtarzano, tak na nich kropiła mowa moja.
Baada ya mimi kuzungumza, hawakusema zaidi; maneno yangu yaliingia masikioni mwao kwa makini.
23 Bo mię oczekiwali jako deszczu, a usta swe otwierali jako na deszcz późny.
Waliningojea kama manyunyu ya mvua na kuyapokea maneno yangu kama ardhi inyonyavyo mvua ya vuli.
24 Jeźlim żartował z nimi, nie wierzyli, a powagi twarzy mojej nie odrzucali.
Walipokata tamaa niliwaonyesha uso wa furaha; nuru ya uso wangu ilikuwa ya thamani kwao.
25 Jeźlim kiedy do nich przyszedł, siadałem na przedniejszem miejscu, i mieszkałem jako król w wojsku, a jako ten, który smutnych cieszy.
Niliwachagulia njia na kukaa kama mkuu wao; niliishi kama mfalme katikati ya majeshi yake; nikawa kama yeye anayewafariji waombolezaji.