< Jeremiasza 48 >
1 Przeciwko Moabowi. Tak mówi Pan zastępów, Bóg Izraelski: Biada miastu Nebo, bo spustoszone będzie; pohańbione i wzięte będzie Karyjataim; zawstydzone będzie miasto na miejscu wysokiem, i bać się będzie.
Kuhusu Moabu: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: “Ole wake Nebo, kwa maana utaharibiwa. Kiriathaimu utaaibishwa na kutekwa; Misgabu itaaibishwa na kuvunjavunjwa.
2 Nie będzie się więcej chlubił Moab z Hesebonu; myślą złe przeciwko niemu, mówiąc: Pójdźcie, a wytraćmy ich z narodu. I ty, Madmenie! wykorzeniony będziesz, miecz pójdzie za tobą.
Moabu haitasifiwa tena; huko Heshboni watu watafanya shauri baya la anguko lake: ‘Njooni na tuangamize taifa lile.’ Wewe nawe, ee Madmena, utanyamazishwa; upanga utakufuatia.
3 Głos krzyku z Choronaim: O spustoszenie i zburzenie wielkie!
Sikiliza kilio kutoka Horonaimu, kilio cha maangamizi makuu na uharibifu.
4 Starty będzie Moab, słyszany będzie krzyk maluczkich jego,
Moabu utavunjwa, wadogo wake watapiga kelele.
5 Przeto, że na drodze Luchytskiej będzie ustawiczny płacz, a którędy zstępują do Choronaim, nieprzyjaciele krzyk zburzenia słyszeć będą,
Wanapanda kwenda njia ya kuelekea Luhithi, wakilia kwa uchungu wanapotembea, kwenye njia inayoshuka kwenda Horonaimu, kilio cha uchungu kwa ajili ya uharibifu kinasikika.
6 Mówiących: Uciekajcie, wybawcie duszę swoję, a stańcie się jako wrzos na puszczy.
Kimbieni! Okoeni maisha yenu, kuweni kama kichaka jangwani.
7 Bo dlatego, że masz nadzieję w dostatku twoim, i w skarbach twoich, będziesz też wzięte, i Chamos pójdzie w pojmanie, kapłani jego, także i książęta jego.
Kwa kuwa mmetumainia matendo yenu na mali zenu, ninyi pia mtachukuliwa mateka, naye Kemoshi atakwenda uhamishoni, pamoja na makuhani wake na maafisa wake.
8 Bo burzyciel przyjdzie na każde miasto, a żadne miasto nie ujdzie; zginie i dolina, i równiny spustoszone będą, jako mówi Pan.
Mharabu atakuja dhidi ya kila mji, wala hakuna mji utakaookoka. Bonde litaangamizwa na uwanda utaharibiwa, kwa sababu Bwana amesema.
9 Dajcie skrzydła Moabowi, niech prędko uleci; bo miasta jego przyjdą w spustoszenie, tak, że nie będzie w nich obywatela.
Wekeni chumvi kwa ajili ya Moabu, kwa kuwa ataangamizwa; miji yake itakuwa ukiwa, pasipo kuwa na mtu atakayeishi ndani yake.
10 Przeklęty, kto zdradliwie czyni sprawę Pańską; przeklęty także, kto hamuje miecz swój ode krwi.
“Alaaniwe yeye afanyaye kazi ya Bwana kwa hila! Alaaniwe yeye auzuiaye upanga wake usimwage damu!
11 Miałci Moab pokój od dzieciństwa swego, i usadził się na drożdżach swoich, ani był przelewany z naczynia w naczynie, to jest, w pojmanie nie chodził, dla czego został w nim smak jego, a woń jego nie zmieniła się.
“Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.
12 Przetoż oto dni idą, mówi Pan, że poślę nań tych, którzy wtargnienia czynią, a pojmają go, i naczynia jego wypróżnią, a łagwie jego potłuką.
Lakini siku zinakuja,” asema Bwana, “nitakapotuma watu wamiminao kutoka kwenye magudulia, nao watamimina; wataacha magudulia yake yakiwa matupu na kuvunja mitungi yake.
13 I zawstydzony będzie Moab od Chamosa, jako zawstydzony jest dom Izraelski od Betel, nadziei swojej.
Kisha Moabu atamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile nyumba ya Israeli walivyoona aibu walipotegemea mungu wa Betheli.
14 Jakoż mówicie: Mocniśmy, a mężowie duży do boju?
“Mwawezaje kusema, ‘Sisi ni mashujaa, watu jasiri katika vita’?
15 Zburzony będzie Moab, i z miast swoich wynijdzie, a wyborni młodzieńcy jego pójdą na zabicie, mówi król, Pan zastępów imię jego.
Moabu ataangamizwa na miji yake itavamiwa, vijana wake waume walio bora sana watachinjwa,” asema Mfalme, ambaye jina lake ni Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
16 Blisko jest zginienie Moabowe, i przyjdzie; a nieszczęście jego prędko się pospieszy.
“Kuanguka kwa Moabu kumekaribia, janga kubwa litamjia kwa haraka.
17 Użalcie się go wszyscy, którzy mieszkacie około niego, i wszyscy, którzy znacie imię jego, mówcie: Jakoż się złamała laska mocy, i kij ozdobny?
Ombolezeni kwa ajili yake, ninyi nyote mnaomzunguka, ninyi nyote mnaojua sifa zake, semeni, ‘Tazama jinsi ilivyovunjika fimbo ya kifalme yenye nguvu, tazama jinsi ilivyovunjika fimbo iliyotukuka!’
18 Zstąp z sławy, a siądź w pragnieniu, obywatelko, córko Dybońska! bo zburzyciel Moabu przyciągnie przeciwko tobie, rozrzuci twierdze twoje.
“Shuka kutoka fahari yako na uketi katika ardhi iliyokauka, enyi wenyeji wa Binti wa Diboni, kwa maana yeye aangamizaye Moabu atakuja dhidi yako, na kuangamiza miji yako iliyozungushiwa maboma.
19 Stań na drodze a przypatrz się pilnie, obywatelko Aroer! pytaj tego, który ucieka, i tej, która uchodzi, mówiąc: Co się dzieje?
Simama kando ya barabara na utazame, wewe unayeishi Aroeri. Muulize mwanaume anayekimbia na mwanamke anayetoroka, waulize, ‘Kumetokea nini?’
20 Zawstydzony jest Moab, bo jest potarty; narzekajcie a wołajcie, opowiadajcie w Arnon, że pustoszą Moaba.
Moabu amefedheheshwa, kwa kuwa amevunjavunjwa. Lieni kwa huzuni na kupiga kelele! Tangazeni kando ya Arnoni kwamba Moabu ameangamizwa.
21 Bo sąd przyszedł na ziemię tej równiny, na Holon, i na Jassa, i na Mefaat,
Hukumu imefika kwenye uwanda wa juu: katika Holoni, Yahasa na Mefaathi,
22 I na Dybon, i na Nebo, i na Bet Dyblataim,
katika Diboni, Nebo na Beth-Diblathaimu,
23 I na Kiryjataim, i na Betgamul, i Betmehon.
katika Kiriathaimu, Beth-Gamuli na Beth-Meoni,
24 I na Karyjot, i na Bocrę, i na wszystkie miasta ziemi Moabskiej, dalekie i bliskie.
katika Keriothi na Bosra; kwa miji yote ya Moabu, iliyoko mbali na karibu.
25 Odcięty będzie róg Moabski, i ramię jego będzie starte, mówi Pan.
Pembe ya Moabu imekatwa, mkono wake umevunjwa,” asema Bwana.
26 Opójcie go, ponieważ się przeciw Panu podniósł; niech się wala Moab w blwocinach swoich, niech będzie i on na pośmiech.
“Mlevye, kwa kuwa amemdharau Bwana. Moabu na agaegae katika matapishi yake, yeye na awe kitu cha dhihaka.
27 Bo azaż w pośmiewisku nie był u ciebie Izrael? Izali go między złodziejami zastano? że, ilekroć mówisz o nim, wyskakujesz.
Je, Israeli hakuwa kitu chako cha kudhihakiwa? Je, alikamatwa miongoni mwa wezi, kiasi cha kutikisa kichwa chako kwa dharau kila mara unapozungumza juu yake?
28 Opuszczajcie miasta a mieszkajcie na skale, obywatele Moabscy! a bądźcie jako gołębica, która ściele gniazdo swoje na kraju dziury.
Ondokeni kwenye miji yenu, mkaishi katikati ya miamba, enyi mnaoishi Moabu. Kuweni kama huwa ambaye hutengeneza kiota chake kwenye mdomo wa pango.
29 Słyszeliśmy o pysze Moabowej, że jest bardzo pyszny; o wysokomyślności jego, i o hardości jego, i o nadętości jego, i o wyniosłości serca jego.
“Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu: kutakabari kwake kwa kiburi na majivuno, kiburi chake na ufidhuli wake, na kujivuna kwa moyo wake.
30 Znamci Ja, mówi Pan, zagniewanie jego; lecz nie ma siły; kłamstwa jego nie dowiodą tego.
Ninaujua ujeuri wake, lakini ni bure,” asema Bwana, “nako kujisifu kwake hakumsaidii chochote.
31 Dlatego nad Moabczykami narzekam, a nade wszystkim Moabem wołam, a dla obywateli Kircheres wzdycha serce moje.
Kwa hiyo namlilia Moabu, kwa ajili ya Moabu yote ninalia, ninaomboleza kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi.
32 Bardziej niż płakano Jazerczyków, płaczę nad tobą, o winna macico Sabama! Latorośli twoje dostaną się za morze, aż do morza Jazer dosięgną; na letnie owoce twoje, i na zbieranie wina twego burzyciel przypadnie.
Ninalia machozi kwa ajili yenu, kama Yazeri aliavyo, enyi mizabibu ya Sibma. Matawi yako yameenea hadi baharini; yamefika hadi bahari ya Yazeri. Mharabu ameyaangukia matunda yako yaliyoiva na mizabibu yako iliyoiva.
33 I ustanie wesele i radość nad polem urodzajnem w ziemi Moabskiej, a winu z prasy wstręt uczynię; nie będą go tłoczyć z wykrzykaniem, a wykrzykanie nie będzie wykrzykaniem.
Shangwe na furaha vimetoweka kutoka bustani na mashamba ya Moabu. Nimekomesha kutiririka kwa divai kutoka mashinikizo; hakuna hata mmoja ayakanyagaye kwa kelele za shangwe. Ingawa kuna kelele, sio kelele za shangwe.
34 Bardziej krzyczeć będą niż Hesebończycy; aż do Eleale, aż do Jazy wydadzą głos swój, od Zoar aż do Choronaim, jako jałowica trzecioletnia; bo też i wody Nimrym zniszczeją.
“Sauti ya kilio chao inapanda kutoka Heshboni hadi Eleale na Yahazi, kutoka Soari hadi Horonaimu na Eglath-Shelishiya, kwa kuwa hata maji ya Nimrimu yamekauka.
35 I uczynię, mówi Pan, że ustanie w Moabie ofiarujący na wyżynach, i kadzący bogom swoim.
Nitakomesha wale wote katika Moabu watoao sadaka mahali pa juu, na kufukiza uvumba kwa miungu yao,” asema Bwana.
36 Przetoż serce moje nad Moabem jako piszczałki piszczeć będzie; także nad obywatelami w Kircheres serce moje jako piszczałki piszczeć będzie, i dlatego, że i zboże zgromadzone wniwecz się obróci.
“Kwa hiyo moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi; unaomboleza kama filimbi kwa ajili ya watu wa Kir-Haresethi. Utajiri waliojipatia umetoweka.
37 Bo na każdej głowie będzie łysina, i każda broda ogolona będzie; na wszystkich rękach będą szramy, a na biodrach wór.
Kila kichwa kimenyolewa na kila mwenye ndevu zimekatwa; kila mkono umekatwa na kila kiuno kimefunikwa kwa nguo ya gunia.
38 Po wszystkich dachach Moabskich i po ulicach jego, wszędy nic nie będzie, tylko narzekanie; bom skruszył Moaba jako naczynie nieużyteczne, mówi Pan.
Juu ya mapaa yote katika Moabu na katika viwanja hakuna kitu chochote isipokuwa maombolezo, kwa kuwa nimemvunja Moabu kama gudulia ambalo hakuna mtu yeyote anayelitaka,” asema Bwana.
39 Narzekać będą, mówiąc: Jakoć jest starty! Jako tył podał Moab z hańbą! i jest Moab pośmiewiskiem, i postrachem wszystkim, którzy są około niego.
“Tazama jinsi alivyovunjikavunjika! Jinsi wanavyolia kwa huzuni! Tazama jinsi Moabu anavyogeuka kwa aibu! Moabu amekuwa kitu cha kudhihakiwa, kitu cha kutisha kwa wale wote wanaomzunguka.”
40 Bo tak mówi Pan: Oto nieprzyjaciel jako orzeł przyleci, a rozciągnie skrzydła swe na Moaba.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Tazama! Tai anashuka chini, akitanda mabawa yake juu ya Moabu.
41 Karyjot wzięte będzie, i zamki wzięte będą, a serce mocarzów Moabskich dnia onego będzie jako serce niewiasty bolejącej.
Miji itatekwa na ngome zake zitatwaliwa. Katika siku hiyo, mioyo ya mashujaa wa Moabu itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wa kuzaa.
42 I wygładzony będzie Moab z ludu; bo się przeciwko Panu podnosił.
Moabu ataangamizwa kama taifa kwa sababu amemdharau Bwana.
43 Strach i dół, i sidło nad tobą, o obywatelu Moabski! mówi Pan.
Hofu kuu, shimo na mtego vinawangojea, enyi watu wa Moabu,” asema Bwana.
44 Kto uciecze przed strachem, wpadnie w dół; a kto wynijdzie z dołu, sidłem ułapiony będzie; bo przywiodę nań, to jest na Moaba, rok nawiedzienia jego, mówi Pan.
“Yeyote atakayeikimbia hiyo hofu kuu ataanguka ndani ya shimo, yeyote atakayepanda kutoka shimoni, atanaswa katika mtego, kwa sababu nitaletea Moabu mwaka wa adhabu yake,” asema Bwana.
45 W cieniu Hesebon stawali ci, którzy uciekali przed gwałtem; ale ogień wynijdzie z Hesebonu, i płomień z pośrodku Sehonu, i pożre kąt Moabski, i wierzch głowy tych, którzy go burzą.
“Katika kivuli cha Heshboni, wakimbizi wamesimama pasipo msaada, kwa kuwa moto umezimika huko Heshboni, mwali wa moto kutoka katikati ya Sihoni; unaunguza vipaji vya nyuso za Moabu, mafuvu yao wenye kujivuna kwa kelele.
46 Biada tobie, Moabie! zaginieć lud Chamosowy; bo synowie twoi zabrani będą w niewolę, i córki twoje do więzienia.
Ole wako, ee Moabu! Watu wa Kemoshi wameangamizwa; wana wako wamepelekwa uhamishoni na binti zako wamechukuliwa mateka.
47 Wszakże zasię przywrócę więźniów Moabskich w ostateczne dni, mówi Pan. Aż dotąd sąd o Moabie.
“Lakini nitarudisha mateka wa Moabu, katika siku zijazo,” asema Bwana. Huu ndio mwisho wa hukumu juu ya Moabu.