< Jeremiasza 17 >

1 Grzech Judzki napisany jest piórem żelaznem, a ostrym dyjamentem wyryty jest na tablicy serca ich, i na rogach ołtarzów waszych;
“Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma, imeandikwa kwa ncha ya almasi, kwenye vibao vya mioyo yao na kwenye pembe za madhabahu zao.
2 Gdy wspominają synowie ich na ołtarze ich, i na gaje ich pod drzewem zielonem, na pagórkach wysokich.
Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao na nguzo za Ashera, kandokando ya miti iliyotanda na juu ya vilima virefu.
3 O góro, i pole moje! majętność twoję i wszystkie skarby twoje podam na rozszarpanie dla grzechu wyżyn twoich, które masz po wszystkich granicach twoich.
Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri na hazina zako zote nitazitoa ziwe nyara, pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.
4 A ty musisz zaniechać za przewinieniem twojem dziedzictwa twego, którem ci dał. I dam cię w niewolę nieprzyjaciołom twoim, i ziemi, której nie znasz; boście ogień rozniecili w popędliwości mojej, który aż na wieki gorzeć będzie.
Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza urithi niliokupa. Nitakufanya mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa umeiwasha hasira yangu, nayo itawaka milele.”
5 Tak mówi Pan: Przeklęty mąż, który ufa w człowieku, i który pokłada ciało ramieniem swojem, a od Pana odstępuje serce jego.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu, ategemeaye mwenye mwili kwa ajili ya nguvu zake, ambaye moyo wake umemwacha Bwana.
6 Albowiem stanie się jako wrzos na puszczy, który nie czuje, gdy co dobrego przychodzi, ale bywa na suchych miejscach na puszczy w ziemi słonej, i w której nikt nie mieszka.
Atakuwa kama kichaka cha jangwani; hataona mafanikio yatakapokuja. Ataishi katika sehemu zisizo na maji, katika nchi ya chumvi ambapo hakuna yeyote aishiye humo.
7 Błogosławiony mąż, który ufa w Panu, a Pan jest nadzieją jego.
“Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katika Bwana, ambaye matumaini yake ni katika Bwana.
8 Bo będzie jako drzewo wszczepione nad wodami, a nad strumieniem zapuszczające korzenie swoje, które nie czuje, gdy przychodzi gorącość, ale liść jego zostaje zielony, a roku suchego nie frasuje się, i nie przestaje przynosić owocu.
Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji uenezao mizizi yake karibu na kijito cha maji. Hauogopi wakati wa joto ujapo; majani yake ni mabichi daima. Hauna hofu katika mwaka wa ukame na hautaacha kuzaa matunda.”
9 Najzdradliwsze jest serce nadewszystko i najprzewrotniejsze, któż je pozna?
Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote, ni mwovu kupita kiasi. Ni nani awezaye kuujua?
10 Ja Pan, który się badam serca, i doświadczam nerek, tak abym każdemu oddał według drogi jego, i według owocu spraw jego.
“Mimi Bwana huchunguza moyo na kuzijaribu nia, ili kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake, kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”
11 Jako kuropatwa zgromadza jajka, ale ich nie wylęga: tak, kto zbiera bogactwa, a niesprawiedliwie, w połowie dni swoich opuści je, a na ostatek będzie głupim;
Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga, ndivyo alivyo mtu apataye mali kwa njia zisizo za haki. Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha, na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.
12 Ale miejsce świątnicy naszej, to jest stolica chwały Najwyższego, wiecznie trwa.
Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo, ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.
13 O nadziejo Izraelska, Panie! wszyscy, którzy cię opuszczają, niech będą zawstydzeni; którzy odstępują odemnie, niech na ziemi zapisani będą; albowiem opuścili źródło wód żywych, Pana.
Ee Bwana, uliye tumaini la Israeli, wote wakuachao wataaibika. Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini kwa sababu wamemwacha Bwana, chemchemi ya maji yaliyo hai.
14 Uzdrów mię, Panie! a będę uzdrowiony: zbaw mię, a będę zbawiony; albowiemeś ty chwała moja.
Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe nami nitaokoka, kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.
15 Oto oni do mnie mówią: Gdzież jest to słowo Pańskie? Niechże już przyjdzie;
Wao huendelea kuniambia, “Liko wapi neno la Bwana? Sasa na litimie!”
16 Chociażem Ja tego nie zabiegał, abym był pasterzem twoim, anim dnia boleści pragnął, ty wiesz, cokolwiek wyszło z ust moich, przed obliczem twojem jest.
Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako; unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa. Kile kipitacho midomoni mwangu ki wazi mbele yako.
17 Nie bądźże mi na postrach; tyś nadzieja moja w dzień utrapienia.
Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu; wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.
18 Niech będą pochańbieni, którzy mię prześladują, a ja niech nie będę zawstydzony; niech się oni lękają, a ja niech się nie lękam; przywiedź na nich dzień utrapienia, a dwojakiem skruszeniem skrusz ich.
Watesi wangu na waaibishwe, lakini nilinde mimi nisiaibike; wao na watiwe hofu kuu, lakini unilinde mimi na hofu kuu. Waletee siku ya maafa; waangamize kwa maangamizi maradufu.
19 Tak Pan rzekł do mnie: Idź, a stań w bramie synów ludu tego, którą wchodzą królowie Judzcy, i którą wychodzą, i we wszystkich bramach Jeruzalemskich,
Hili ndilo Bwana aliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.
20 I rzecz do nich: Słuchajcie słowa Pańskiego, królowie Judzcy, i wszystek Judo, i wszyscy obywatele Jeruzalemscy, którzy chadzacie temi bramami!
Waambie, ‘Sikieni neno la Bwana, enyi wafalme wa Yuda, nanyi watu wote wa Yuda, na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.
21 Tak mówi Pan: Strzeżcie pilnie dusz waszych, a nie noście brzemion żadnych w dzień sabatu, ani ich wnoście bramami Jeruzalemskiemi;
Hili ndilo asemalo Bwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.
22 Ani wynaszajcie brzemion z domów waszych w dzień sabatu, ani żadnej roboty odprawujcie, ale święćcie dzień sabatu, jakom rozkazał ojcom waszym.
Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yoyote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.
23 Wszakże nie usłuchali, ani nakłonili ucha swego, owszem, zatwardzili kark swój, nie słuchając ani przyjmując nauki.
Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao, na hawakutaka kusikia wala kukubali adhabu.
24 A jeźli mię pilnie słuchać będziecie, mówi Pan, tak, żebyście nie wnosili brzemion bramami miasta tego w dzień sabatu, ale święcili dzień sabatu, nie odprawując weń żadnej roboty;
Lakini mkiwa waangalifu kunitii, asema Bwana, nanyi msipoleta mzigo wowote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,
25 Tedy wchodzić będą bramami miasta tego królowie i książęta siedzący na stolicy Dawidowej, jeżdżąc na wozach i na koniach, oni i książęta ich, mężowie Judzcy i obywatele Jeruzalemscy, i stać będzie to miasto aż na wieki.
ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi wataingia kupitia malango ya mji huu, pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.
26 I zbieżą się z miast Judzkich i z okolicznych miejsc Jeruzalemskich, i z ziemi Benjaminowej, i z równin, i z tej góry, i od południa, przynosząc całopalenie, i ofiarę, i dar, i kadzidło, także i dziękczynienie niosąc do domu Pańskiego.
Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba ya Bwana.
27 Ale jeźli mię nie usłuchacie, abyście święcili dzień sabatu, a nie nosili brzemion, wchodząc bramami Jeruzalemskiemi w dzień sabatu, tedy rozniecę ogień w bramach jego, który pożre pałace Jeruzalemskie, a nie będzie ugaszony.
Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wowote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’”

< Jeremiasza 17 >